Lulu Diva: Nili-date na mume wa mtu, yakanikuta!
Video Queen Lulu Abasi ‘Lulu Diva’.
Lulu Diva: Ni fani iliyokuwa kwenye damu. Napenda sana mambo ya umodo, ndiyo maana nikaja huku nikiamini nitatimiza ndoto zangu. Ijumaa: Mavideo Queen wengi hujikuta wakitembea na wanamuziki ambao wanashiriki kwenye kazi zao, ni kwa nini? Wewe je ulishatoka na mwanamuziki uliyeshiriki kwenye video yake? Lulu Diva: Wapo baadhi wanaofanya hivyo na hiyo si lazima, inategemea na tabia ya mtu. Mimi sijawahi kutembea na mtu niliyefanya kazi yake.
Ijumaa: Kuna madai kuwa wewe ulishawahi kutembea na msanii Nasibu Abdul ‘Diamond’, unayazungumziaje madai hayo? Lulu Diva: Dah! Watu walihisi tu kwa sababu alikuwa ni mshkaji wangu, sijawahi kutoka naye. Ijumaa: Mavideo Queen wengi mmekuwa mkisumbuliwa na mapedeshee, kwako wewe umewahi kupata usumbufu huo?
Lulu Diva: Ni kweli wanasumbua sana na usipokuwa makini unaweza kujikuta unawapanga.
Ijumaa: Ulishawahi kuwa na uhusiano na mtu mzima ‘shugadadi’ katika mapito yako ya kimapenzi?
Lulu Diva: Ndiyo nilishakuwa naye alinipenda sana, tuliachana kwa sababu mkewe alijua, tukasumbuana sana, yaliyonikuta ni siri yangu.
Ijumaa: Je, mwanaume huyo alikuwa akifanya kazi gani?
Lulu Diva: Dah! Alikuwa ni mfanyabiashara mkubwa sana hapa Bongo.
Ijumaa: Maisha yako ya kimapenzi kwa sasa yakoje?
Lulu Diva: Niko kwenye uhusiano ambao siyo siriasi sana kwani bado tunachunguzana.
Ijumaa: Wasichana wengi kama wewe wanapenda wanaume wenye pesa, kwa upande wako hilo liko vipi?
Lulu Diva: Mimi pia napenda mwanaume mwenye pesa kwa sababu kila ninachokifanya kinataka pesa, hivyo nikimpata asiyekuwa na pesa nitamchiti tu.
Ijumaa: Ukiwa na mpenzi wako huwa unapenda kwenda naye wapi?
Lulu Diva: Napenda tujifungie ndani tu, hakuna kwenda popote.
Ijumaa: Pozi gani unalipenda ukiwa naye na ni mavazi gani unapendelea faragha?
Lulu Diva: Napenda anipakate kama mtoto. Kwa upande wa mavazi napenda kuvaa nguo za ndani tu au kanga moja. Ijumaa: Ni mwanamuziki gani unapenda sana kufanya naye video kwa hapa Bongo? Lulu Diva: Nampenda Christian Bella na kuna video nimefanya naye itatoka soon, ni kali sana.


Post a Comment