ad

ad

Dk Mwaka Jeuri Kwisha...Serikali yazidi kumkaanga, biashara yake yadoda


Tabibu wa Kliniki ya Fore Plan, Mwaka Juma Mwaka, ‘Dk Mwaka’.

DAR ES SALAAM: Kufuatia tumbutumbua majipu inayoendelea katika sekta mbalimbali nchini, imebainika kuwa kitendo hicho kimemsababishia mtabibu wa Kliniki ya Fore Plan iliyopo Ilala-Bungoni jijini Dar, Mwaka Juma Mwaka, ‘Dk Mwaka’ apoteze wateja (wagonjwa) kwa madai ya kupoteza imani naye, Risasi Mchanganyiko linakupa stori kamili.
dk mwaka hospitalJengo la Kliniki ya Fore Plan.
SAKATA LILIPOANZIA
Sakata la Dk. Mwaka na serikali lilianza Desemba 14, mwaka jana baada ya daktari huyo kudaiwa kumkimbia Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamis Kigwangalla mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza kwenye kliniki yake.
KIGWANGALLA (4)Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamis Kigwangala.
NINI KILIFUATA?
Katika ziara hiyo, naibu waziri huyo aliagiza viongozi wa tiba asilia kukagua taaluma ya daktari huyo na ya washirika wake sambamba na aina ya dawa zinazotumika kituoni hapo.
Aidha, Dk. Kigwangala aliongeza kuwa, Dk. Mwaka amekuwa akiuka sheria za tiba asili kwa kujitangaza zaidi kupitia vyombo vya habari na kurusha vipindi vinavyoonesha akiuchambua mwili wa binadamu kana kwamba ni daktari, yote hayo yakiwa kinyume na taratibu za tiba asilia.

BIASHARA YADODA
Mara baada ya kauli hiyo ya serikali kutolewa na kuonesha kuwa ni dhahiri mtabibu huyo ana ‘figisufigisu’ kwenye huduma zake, taarifa kutoka kwa chanzo chetu zilieleza kuwa wagonjwa wameanza kupungua katika kliniki hiyo.
UMMY+21 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.
TUJIUNGE NA CHANZO
“Serikali ni kama iliwafungua wananchi maana kulikuwa na malalamiko ya chini kwa chini juu ya kutokuwa na imani na hizi huduma za kina Mwaka lakini ilikuwa ni za mtu mmojammoja sasa aliposema waziri, watu wameacha kwenda kwa wingi.
“Yani sasa hivi ukifika huduma zinaendelea lakini watu ni wachache sana. Zamani ilikuwa si mchezo. Ukifika pale mapokezi hupati hata nafasi lakini sasa nafasi ipo maana imani ya watu katika kliniki hiyo imepungua,” kilisema chanzo chetu.
MABENCHI MEUPEE
Mwandishi wetu alishuhudia mabenchi ya wagonjwa yakiwa ‘meupe’ tofauti na kipindi cha nyuma huku wahudumu wa kituo hicho wakiwa wamejipanga getini na kuonesha ukarimu wa hali ya juu kwa wagonjwa wachache waliojitokeza kituoni hapo.
SERIKALI YAZIDI KUMKAANGA
Ukiachana na kauli ya awali ya serikali, wiki iliyopita, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alisema vituo vingi vya tiba asili ikiwemo cha Dk. Mwaka havina sifa za kutoa tiba asili na mbadala.
Alisema havina sifa kwa sababu vinajiendesha kinyume na taratibu za tiba asilia ambapo alipiga marufuku dawa zote zisizosajiliwa na kutolewa katika vituo vya tiba asilia na mbadala kwa sababu zina hatari kwa afya ya binadamu.
KIGWANGALA TENA!
Kama hiyo haitoshi, kwa mara nyingine Dk. Kigwangala alizidi kupigilia msumari suala hilo kwa kusema Dk. Mwaka amekuwa akitoa tiba pasipokuwa na dawa ya aina yoyote iliyosajiliwa na Ofisi ya Mkemia Mkuu wala TFDA.
WANANCHI WANENA
Mkazi mmoja wa Ilala Dar es Salaam aliyetimbulisha kwa jina moja la Juma, alisema serikali imechelewa kubaini tatizo hilo kwani kama wamegundua kuna matatizo katika tiba hizo, tayari watu wameshaathirika kwa muda mrefu.
“Serikali ilikuwa wapi siku zote. Haioni kwamba tayari kuna Watanzania wengi tu wameshaathirika? Yani kwa kweli hili ni janga,” alisema Juma.
MWAKA ANASEMAJE?
Mwanahabari wetu alipotaka kuonana na Dk. Mwaka ili aweze kuzungumzia sakata hilo alikutana na mmoja wa manesi aliyejitambulisha kwa jina moja la Agnes na kusema kuwa Dk. Mwaka hakuwepo kituoni hapo na kumtaka mwandishi wetu kuacha mawasiliano na maswali ya kumuuliza pindi atakapofika.
“Siruhusiwi kuzungumza chochote mpaka nitakapozungumza na mkuu wangu wa kazi. Wewe acha namba zako na maswali yako, nitamfikishia,” alisema Agnes.

CHANZO: RISASI

No comments

Powered by Blogger.