Rais Kikwete aitaka Tanesco kuwasha mitambo yote ili kupata umeme wakutosha
Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameridhishwa na ujenzi wa uwekezaji wa mradi wa kituo cha kufua umeme wa mitambo ya gesi asilia cha Kinyerezi One uliogharimu shilingi bilioni 400 na kulitaka shirika la umeme nchini kuhakikisha kazi ya kukamilisha kuwasha mitambo mitatu iliyobakia inakamilika haraka ili kuondoa malalamiko ya kukosekana kwa nishati ya umeme wa uhakika nchini.
Ameyasema hayo jijini Dar es Salaam alipotembelea mitambo hiyo na
chumba maalum cha wataalamu wanaoongoza mitambo hiyo na kuzindua mradiwa
mtambo wa kuzalisha umeme wa Kinyerezi One wenye uwezo wa megawati150
ambao ujenzi wake umekamilika kwa asilimia miamoja.
Aidha Dk Kikwete amelitaka shirika hilo kutumia vyanzo vya umeme wa
gesi asilia kama fursa ya kufanya biashara ndani na nje ya nchi.
Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa shirika la umeme nchini
Tanesco injinia Felsheslim pamoja na kuelezea mtambo huo kuwa ni wa
kisasa una uwezo wa kutumia gesi asilia ama mafuta mepesi ya kuendeshea
ndege amesema tayari umeme wa gesi umekwishaingia kwenye gridi ya taifa
kupitia nyaya zenye msongo wa kilovati 220 na katika ubora wake kamwe
hairuhusu kushindwa kuzalisha umeme.
Awali Tanesco iliwasha mitambo yake ya umeme wa gesi Septemba 17
katika kituo chake cha Ubungo jijini Dar es Salaam na tayari megawati
200 hadi sasa zimekwishaingia ambapo pia shirika la umeme Tanesco
likamzawadia rais Kikwete picha maalum yenye miradi mbalimbali ya umeme
ambayo ameitekeleza wakati wa kipindi chake cha uongozi kwa miaka kumi
ikiwa ni suluhisho la upatikanaji wa umeme wa uhakika hapa nchini.

Post a Comment