Mgombea urais wa Chadema kupitia UKAWA apokelewa kwa kishindo Mwanza
Jiji la kibiashara la Mwanza limejikuta likisimamisha shughuli zake
zote kupisha mkutano mkubwa wa hadhara uliokuwa ukiongozwa na mgombea
urais wa Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda umoja wa katiba
ya wananchi UKAWA Edward Lowassa huku zaidi ya wananchi 130 wakizimia.
Swali jepesi kabisa ambalo kwa sasa kila mtanzania anaweza kulijibu, lakini kwa jiji la Mwanza sauti imepaa zaidi.
Kishindo cha mgombea huyo wa nafasi ya urais Edward Lowassa ndani
ya uwanja wa Furahisha kikatikisa afya za wakazi wa jiji la Mwanza kwa
mujibu wa chama cha msalaba mwekundu.
Akiwa jiji Mwanza alikuwa na kazi rahisi zaidi ya kuomba kupigiwa
kura ya ushindi wa kishindo kwakuwa anania, ari na nguvu za kuhakikisha
Tanzania inapata uchumi imara huku akiwataka watanzania kujiandaa vema
na Oct 25 mwaka huu.
Wakati tume ya uchaguzi ikiwa tayari imekwisha weka bayana idadi ya
vituo vya kupigia kura, umoja wa katiba ya wananchi UKAWA umekwisha
kubaini tatizo ndani ya tume hiyo na kutoa rai kwa watanzania.
Baada ya kutumia muda wake wa miaka 61 ndani ya tanu na CCM, kabla
ya kukitosa chama chake cha CCM hivi karibuni, amemwagia sifa lukuki
mgombea urais Edward Lowassa kwani ni kiongozi imara mwenye ndoto na
Tanzania mpya, huku akitoa neno kwa watanzania.
.

Post a Comment