Dkt Magufuli aahidi kurejesha viwanda vilivyo binafsishwa bila kuendelezwa
Chama
cha mapinduzi kimesema serikali ijayo ya awamu ya tano chini ya Dkt
John Pombe Magufuli kimejipanga kurejesha hadhi ya mji wa Arusha na
mikoa mingine iliyokuwa na hadhi ya kuwa na viwanda kwa kuvifufua
viwanda vya serikali na kurejesha vile vilivyobinafsishwa kwa wawekezaji
bila kuendelezwa na kutelekezwa ili viweze kuongeza ajira kwa
watanzania huku mgombea ubunge wa chama hicho katika jimbo la Monduli
akikanusha kukihama chama cha Mapinduzi.
Katibu mkuu wa chama cha mapinduzi CCM Komred Abdulrahaman Kinana
ameyasema hayo jijini Arusha, wakati akimnadi mgombea urais wa jamuhuri
ya mungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama hicho Dkt John Pombe
Magufuli, ambaye yuko katika mkoa wa Arusha akinadi sera za chama hicho
ili kupata ridhaa ya kuwaongoaza watanzania.
Akiwahutubia mamia kwa maelfu ya wakazi wa jiji la Arusha na viunga
vyake, mgombea huyo wa urasi kupitia CCM Dkt John Magufuli amesema,
mara atakapo pata ridhaa ya watanzania katika ngazi ya urasi atarejesha
serikalini viwanda vyote vilivyobinafsishwa bila kuendelezwa ikiwa ni
pamoja na kufufua viwanda na kujenga viwanda vingine ili kuondoa tatizo
la ajira kwa watanzania.
Akiwa mkoani Arusha mgombea uras Dkt John Magufuli alizuru kaburi
la aliyewahi kuwa waziri mkuu wa Tanzania enzi za Mwalimu Nyerere hayati
Edward Moringe Sokoine na kusifia uadilifu na utendaji kazi uliokuwa
ukifanywa na kiongozi huyo.
Mgombea ubunge wa jimbo la Monduli kupitia CCM Namelock Sokoine
amekanusha kukihama chama hicho na kujiunga na upinzani ambapo katika
mikutano iliyofanyika mtowa mbu, Monduli mjini, Longido na Arusha mjini
baadhi ya waliokuwa watia nia za kugombea ubunge kupitia vyama vya
Chadema na CUF wamejiunga na CCM.

Post a Comment