ad

ad

Michirizi Ya Damu - 17


“Please! Don’t kill me,” (usiniue tafadhali) alisema padri huku akipiga magoti.
“Do you?” (unaikumbuka?)
“I saw you a while ago,” (nilikuona muda mfupi uliopita)
“Okey! I came to kill you,” (Sawa! Nimekuja kukuua) alisema Fareed huku akimwangalia padri huyo.
“I’ve done nothing! Please! Have mercy, I have done nothing,” (sijafanya lolote! Tafadhali nihurumie! Sifanya lolote) alisema Padri huyo huku akiwa amepiga magoti.
Fareed akaanza kumkumbusha padri huyo kila kitu kilichokuwa kimetokea kuhusu wao. Alianzia mbali, jinsi alivyokuwa ameathirika kwa vitendo vya kishoga mpaka kufikia hatua ya kwenda kanisani hapo kwa ajili ya kuungama dhambi zake.
Padri Luke akakumbuka, akamwangalia vizuri Fareed, akamkumbuka. Akazidi kulia na kuomba msamaha zaidi kwamba kile alichokifanya ni shetani tu ndiye aliyempitia.
Fareed hakutaka kumuelewa, hapohapo akamchukua na kuelekea naye ndani ya chumba kile cha kuungamia dhambi, kama alimfanyia vitendo hivyo ndani ya chumba kile basi alitaka kumuua ndani ya chumba hicho hicho.
Hakutaka kupoteza muda, hapohapo akamchoma visu vitatu tumboni na kifuani mwake, padri akaugulia kwa maumivu makali, akaanguka chini, akatoka damu nyingi na hapohapo Fareed kumburuza na kuacha michirizi ya damu pale sakafuni.
Hakuishia hapo, alitaka kuijulisha dunia kwamba yeye ndiye aliyefanya mauaji ya watu hao watatu hivyo kuchukua karatasi na kuuacha ujumbe uliosomeka C'est fait yakiwa na maana ya kukamilika kwa jambo au ‘done’ kwa Lugha ya Kiingereza. Hakutaka kupoteza muda, alipoona amekamilisha kila kitu, akaondoka mahali hapo haraka sana.
****
FBI walishindwa kujua ni kwa namna gani wangeweza kumpata muuaji wa mauaji hayo, walisambaza picha za Fareed kila kona lakini hawakuwa wamefanikiwa. Walijua kwamba kijana huyo alikuwa nchini Marekani lakini kitu cha ajabu kabisa hawakuweza kumuona.
Walichokifanya ni kuweka dau kwamba kwa mtu yeyote ambaye angefanikisha kupatikana kwake basi angezawadia zawadi nono ya dola elfu hamsini, zaidi ya milioni mia moja lakini napo zoezi hilo likaonekana kuwa gumu.


Watu ambao walionekana kufanana nja Fareed walikamatwa na kupelekwa katika vituo vya polisi, kila mmoja alikuwa na uchungu wa kupata pesa hizo ambazo zilikuwa nyingi, pesa ambazo zingeweza kuwatoa katika hali waliyokuwa nayo na kuwapeleka sehemu nyingine kimaisha.
Siku zikakatika, hakukuwa na mtu aliyejua mahali mtu huyo alipokuwa. Walitoa taarifa katika hoteli zote hapo Marekani kuhakikisha kwamba mtu huyo anakamatwa mara baada ya kuingia hotelini lakini zoezi hilo lote lilionekana kuwa gumu kwani bado mtu huyo hakuwa amepatikana mpaka muda huo.
“Where the hell is he?” (yupo wapi?) aliuliza jamaa mmoja, kama walivyokuwa wenzake, hata yeye mwenyewe alikuwa amechanganyikiwa.


“I don’t know! Everyone wants to get the damn money bro,” (sijui! Kila mmoja anaitaka pesa kaka) alisema jamaa mwingine, walikuwa Wamarekani weusi ambao hata kwa kuwasikia jinsi Kiingereza chao walivyokuwa wakiongea, haikuwa ngumu kugundua kama walikuwa wao.
Wakati Marekani ikiendelea kusumbuka kumtafuta Fareed, katika nchi nyingine, zile zilizokuwa na uadui mkubwa na Marekani walikuwa na furaha mno. Walifurahi kuona nchi hiyo ikiwa imeshambuliwa na watu kadhaa kuuawa.


Nchini Urusi, mpaka watu wakawa wanashangilia baa, waliwachukia majirani zao hao na muda wowote ule walitamani kuona nchi hiyo ikipotea katika uso wa dunia.
Uarabuni, katika nchi mbalimbali watu walikuwa wakifurahia, kundi la kigaidi la Al Qaida lilijitangaza hadharani kwamba wao ndiyo walikuwa wamewatuma watu kupeleka mabomu na kulipua kituo hicho, kilichowashangaza ni sababu ya mtu wao mmoja kukimbia kwani lengo lilikuwa ni kuwaua wote.


Maelezo hayo kidogo yakawafanya Wamarekani kufikiria mara mbili kwamba inawezekana mwanaume huyo hakuwa na lengo la kuulipua kituo hicho bali alishinikizwa na watu kufanya hivyo. Walitaka kujua, kama kweli alilipua kituo hicho na kukimbia, ilikuwa ni lazima wamtafute na kumpata ili kujua ni wakina nani walikuwa wamemtuma kushambulia kituo hicho na kwa sababu gani alikuwa akikimbia.


Fareed alichukiwa lakini FBI walikuwa wakimuhitaji kwa nguvu zote. Waliendelea kutangaza dau nono kupatikana kwa mtu huyo lakini ilishindikana ila baada ya siku nne, wakapigiwa simu na kuambiwa kwamba mtu huyo alikuwa katika Hospitali ya Britania Medical Center iliyokuwa hapohapo Pennslyvania hivyo walitakiwa kwenda kumuona huko.
“Hospitali?” aliuliza ofisa mmoja wa FBI.


“Ndiyo! Tumeambiwa yupo huko, hizo ni taarifa za chini, twendeni,” alisema Thomson, mwanaume yuleyule aliyekuwa na jukumu kubwa la kumtafuta Fareed kwa tukio alilokuwa amelifanya.
Akawakusanya maofisa wenzake wanne na kuanza kuelekea huko. Ilikuwa ni lazima wawahi kwani walijua fika kwamba kama wangechelewa basi inawezekana wangekuta ametoroka kwani kwa mtu kama yeye ambaye alikuwa akitafutwa kila kona ilikuwa ni lazima kutoroka ili kujificha asikamatwe.


Hawakuchukua muda mrefu wakafika mahali hapo, haraka sana wakateremka na kuanza kuelekea ndani ya hospitali hiyo. Walitembea harakaharaka kama watu waliokuwa wakiwahi kitu fulani. Walipofika mapokezi, kwanza wakaambiwa kwamba kweli mtu huyo alikuwa hospitalini hapo, alifikishwa baada ya kukutwa barabarani akiwa hoi kwani tumbo lilikuwa likimsumbua.
“Safi sana, hebu tupeleke,” alisema Thomson na nesi kuanza kuwapeleka katika chumba alichokuwepo Fareed.


****
Moyo wake ulikuwa na furaha tele, kitendo cha kumuua Padri Luke kilimaanisha kwamba kile alichokuwa amekihitaji kwa kipindi kirefu hatimaye alikuwa amekifanikisha.
Akaondoka, kila alipopita alikutana na picha zake, alikuwa akitafutwa kila kona huku kiasi cha dola elfu hamsini kimewekwa kama zawadi kwa mtu yeyote ambaye angefanikisha kupatikana kwake.
Moyo wake ukaogopa lakini wakati mwingine hakuona kama kulikuwa na tatizo kaka tu angekamatwa na kufikishwa katika kituo cha polisi. Alikuwa na kiasi kikubwa cha pesa, mwanaume yule, bilionea Williams alikuwa amemuwekea kiasi kingine cha pesa, alijiona kuwa milionea mkubwa ambaye kama angefika nchini Tanzania basi maisha yake yangekuwa katika levo nyingine kabisa.


Hakuwa na pa kulala na aliogopa sana kwenda hotelini, alichokifanya ni kubaki barabarani hapohapo Pennsylvania na kulala na masikini waliokuwa mitaani. Alijisikia amani zaidi kulala humo kuliko hata kulala katika hoteli kubwa huku akiwa na hofu tele.
Alikuwa akijifikiria ni kwa namna gani angeweza kurudi nchini Tanzania. Hakuwa na kibali chochote, kila kitu kilipotea katika ndege ile na mbaya zaidi alishindwa kwenda hata ubalozini kwani kila kona alikuwa akitafutwa.


Alilala mitaani na masikini, hakukuwa na mtu aliyejali, kila mmoja alikuwa na mambo yake, ilipofika siku ya nne huku akiwa mtaani na akiendelea kufanya harakati za kutafuta msaada wa siri kuuondoka nchini humo maumivu ya tumbo yakaanza tena.
Yalikuwa ni maumivu makali, alihisi tumbo lake kama likiungua moto, alitapika madonge makubwa ya damu, wakati mwingine mpaka kwenye makalio yake kulikuwa kukitoa damu hali iliyomuogopesha kupita kawaida.


Kilio chake cha maumivu ndicho kilichowashtua masikini waliokuwa mitaani, walipomfuata na kuona tatizo lake, wakaanza kumpeleka hospitalini huku akiwa hoi, kifua chake kilitapakaa damu kutokana na kukohoa madonge ya damu sana.


Akafikishwa katika Hospitali ya Britain Medical Center ambapo moja kwa moja akapelekwa katika chumba kimoja na kuanza kufanyiwa vipimo. Bado Fareed alikuwa akilia kwa maumivu makali, madaktari ambao walikuwa wakimwangalia hawakumgundua kama alikuwa Fareed, mwanaume aliyeua watu wengi kwa kuwalipua katika kituo cha treni.
ITAENDELEA KESHO JUMATATU FEB 5, 2018

No comments

Powered by Blogger.