Mwili wa Mama Celina Kombani tayari umeagwa Dar, safari imeanza kwa ajili ya Mazishi.
RIP Mama Celina Kombani… Usiku wa September 24 2015 taarifa ya Majonzi ilitufikia ambapo taarifa yenyewe ilikuwa inahusu msiba wa aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Mama Celina Kombani.
Mama Celina alifariki kutokana na maradhi ya Saratani, na alifariki akiwa India ambako alienda kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
Taarifa kuhusu Ratiba ya mwili kuwasili Dar es Salaam na shughuli za kuaga mwili pamoja na Ratiba ya Mazishi tayari ilitolewa.
Mwili wa Marehemu umewasili Dar na watu
mbalimbali wamejitokeza kuaga mwili ya Marehemu katika Viwanja vya
Karimjee, Dar es Salaam.
Post a Comment