ad

ad

MBATIA AJIBU MAMBO ALIYOSEMA DR. SLAA JANA

Mwenyekiti mwenza wa UKAWA James Mbatia ameongea mchana huu na waandishi wa habari na kujibu baadhi ya mambo aliyosema Dr. Slaa

Mbatia: Napenda kuwaomba Watanzania tusimame wote kupata Katiba mpya ambayo ndiyo ajenda ya mgombea wetu Lowassa. ‪#‎MbatiaAnaongea‬

Mbatia: Watanzania naomba waelewe UKAWA tunasimamia utu, uzalendo, uadilifu, umoja, uwazi, uwajibikaji ndani ya Tanzania.

Mbatia: Wanasiasa hasa wale wa CCM Mwakyembe na Sita, wanaotaka midahalo waje waongee na mimi wasimsumbue Mgombea wetu Lowassa sio saizi yao.

Mbatia: Hivi ni ashiria kwamba CCM wameshindwa hoja, mara kuleta mambo ya udini, mara wanaibua hili mara lile. wanataka kuchafua amani yetu kwa kuigiza masuala ya dini

Mbatia: Wagombea wetu urais walikaa na Dokta Slaa alisema mimi ni bora kuliko wote,leo hii anasema hajawahi kutia nia,kweli?

Mbatia: Tukisema tuibue masuala yote na kashifa za kuuzwa kwa nyumba, kuna mtu atabaki salama?

Mbatia: Eti Lowassa akija ndani ya Ukawa atakuja na Wenyeviti wa CCM..hakuwahi kusema..kayasemea wapi?

Mbatia: Wewe unasema ni muadilifu ulipewa Milioni 500 mwaka 2008 unakuja kusema leo baada ya miaka 7? Tuwe wakweli.

Mbatia: Eti suala la rushwa zaidi ya miaka 7 usiripoti halafu uje useme leo, kusema uongo ni kazi sana.

Mbatia: Napenda kuwaomba watanzania wote ambao ni zaidi ya milioni 46, wasiruhusu nchi yetu ikaharibiwa na watu 100.

Mbatia: Wakenya walisema hata kama ana makosa, walisema huyo huyo tunamtaka, wakampigia kura na leo ni Rais wao.

Mbatia: Watu wachache wanaotaka eti kwa lolote lile lazima waendelee kubaki madarakani, tunasema hapana.

Mbatia: Lazima tufute mfumo huu uondoke tuwe na Tanzania mpya.

Mbatia: Napenda kuwaomba wale Viongozi wa dini walionewa kwa yale ya jana, wasamehe na waachane nayo.

Mbatia: Lowassa hajawahi kutamka kuwa nikija ndani ya UKAWA nitakuja na wabunge 50, wenyeviti wa CCM na Makatibu nk.

Mbatia: Kama hana faida haya mafuriko tungepata wapi? Nyota ya Lowassa inang'aa hata wafanye nini hawamuwezi huyu jamaa

Mbatia: Hatuna haja ya kuanza kumjadili, hiyo ni kulipasua Taifa la Tanzania kwa maslahi binafsi

Mbatia: Kilichotusikitisha ni yeye kuhusisha watu wengine wasiohusika kwenye jamii yetu, viongozi wa dini wenye heshima zao, acha sisi vyama vya siasa tusuguane wenyewe.

Mbatia: Zimebaki siku 50 na kitu, haki itendeki na nchi yetu ibaki na amani siku zote

Mbatia: Anasema kaja kupambana na Lowassa kwakuwa anagombea urais, sasa Sumaye naye anagombea urais?
Powered by Blogger.