ad

ad

AZAM FC YATOA KAULI KUHISIANA NA UPUUZI MKUBWA WA JUMA NYOSSO, YAVISHUKURU VYOMBO VYA HABARI

Klabu ya Azam FC, imeeleza masikitiko yake kutokana na beki Juma Nyosso kumshika makalio nahodha wake, John Bocco kwa lengo la kumdhalilisha.


Msemaji wa Mbeya City, Jaffar Iddi amesema wamesikitishwa kwa kiasi kikubwa na kitendo hicho cha Nyosso ambacho kilinaswa na vyombo mbalimbali .

Nyosso alifanya makusudi kumdhalilisha Bocco hii ikiwa ni mara ya pili kunaswa na vyombo vya habari akifanya hivyo.
Msimu uliopita alimfanyia hivyo, Elius Maguri wakati akiitumikia Simba, akanaswa na blogu hii pamoja na gazeti namba moja la michezo nchini la CHAMPIONI.

“Vitendo kama hivyo kama alivyofanya Nyosso havikubaliki hata kidogo, tunaalani kwa nguvu zote kabisa.

“Lakini tunavishukuru vyombo vya habari kuhusiana na hilo, vimekuwa shahidi wa kila kitu. Lakini pia tunaiachia TFF, tunajua hadi Rais wa TFF, Jamal Malinzi hilo limemfikia.

“Tunaamini hatua kali zitachukulia kukomesha vitendo kama hivyo visivyo vya kiungwana,” alisema.


Baada ya kubainika alimfanyia hivyo Maguri, Nyosso ambaye ni beki wa zamani wa Simba, alifungiwa mechi nane.
Powered by Blogger.