REAL MADRID YATHIBITISHA KUONDOKA KWA CASILLAS
Real Madrid imetangaza rasmi kuwa kipa wake mkongwe Iker Casillas anajiunga na Porto.
Miamba hiyo ya Hispania imetangaza kupitia mtandao wao rasmi kuwa kipa huyo mwenye umri wa miaka 34 anaondoka Real Madrid na ikamshukuru kwa huduma yake.
"Tumekubali uhamisho wa Casillas kwenda Porto ya Ureno," imeeleza taarifa hiyo ya Real Madrid.
"Huyu si miongoni mwa makipa bora wa Real Madrid - Ni kipa bora katika hitoria ya Real Madrid na Hispania kwa ujumla wake.
Kuondoka kwa Casillas kunazidi kuhanikiza tetesi za kipa wa Manchester United David de Gea kutua Real Madrid.
Real Madrid imetangaza kuondoka kwa Iker Casillas
Real Madrid imeweka picha hii Twitter kama sehemu ya kumshukuru Casillas kwa huduma zake kwenye klabu hiyo
Casillas alishinda mataji matatu ya Champions League na mataji matano ya La Liga katika kipindi alichoidakia Real Madrid
Kuondoka kwa Casillas kunafungua njia ya David de Gea kutua Real Madrid
CREDIT: SALUTI 5.COM

Post a Comment