ad

ad

JAMANI DADA MARTHA LOOO!-19



 
www.facebook.com/2jiachie
ILIPOISHIA:

“Yes baby…”

“Yule mwanamke pale uani alikuitaje?”

“Yupi?”

“Yule mama Anna.”

“Mama ni yupi kati ya wale?”

Roi alijizungusha huku akijua anazungumziwa nani.

JIACHIE MWENYEWE SASA…

“Yule mwenye umbo namba nane!”

“Mi sikumsikia, kwani alisemaje baby?”

“Ha! Una uhakika sweet? Mi nimemsikia akikusalimia kwa kukwambia sijui wewe baby?”

“Mh! Kweli anaweza kunisalimia hivyo mimi? Mbona sifahamiani naye zaidi ya hapa kwako. Sasa mimi niwe baby wake kivipi jamani?”

“Ndiyo nimeshangaa pale baby.”

***

Roi aliondoka kwenda kwenye shughuli zake, nyuma Martha aliamua kuumiza kichwa kuhusu mama Anna.

Kuna wakati alivizia mama Anna yuko bize, akamwingia mmoja wa wapangaji wenzake...

“Mambo shosti?”

“Poa, vipi Martha?”

“Poa. Hivi, asubuhi pale wewe si ulikuwepo uani wakati mgeni wangu anakwenda kuoga?”

“Nilikuwepo ndiyo, vipi kwani?”

“Hivi, mama Anna alimsalimia vipi mgeni wangu?” aliuliza Martha huku akimkazia macho mpangaji huyo.

“Alimsalimia kawaida tu. Alimwambia salama sijui wewe hapo?”

“Kweli?”

“Kweli. Kwani wewe ulisikiaje?”

“Mimi nilisikia akisema salama sijui wewe honey.”

“Hapana, alisema sijui wewe hapo.”

“Oke basi, lakini usimwambie chochote mama Anna.”

“Sawa, wala simwambii.”

***

Jioni, saa kumi na moja, Roi ndiye aliyeanza kumtumia meseji mama Anna ambapo mchana kutwa wa siku hiyo hawakuwasiliana...

“Mzima baby?”

“Mzima sweet, wewe?”

“Mzima. Wapi hiyo?”

“Niko home, wewe?”

“Mimi nipo njiani. Unapakumbuka vizuri nyumbani kwangu?”

“Ndiyo. Kumetokea nini kwani baby wangu?”

“Unaweza kuja?”

“Sasa hivi?”

“Yes, mimi naelekea huko muda si mrefu nitakuwa nimefika.”

“Poapoa.”

Mama Anna aliwafuata wenzake, akawatonya kuhusu kuitwa na bwana wa Martha nyumbani kwake...

“Safi sana. Nenda katese mwanamke mwenzetu.”

“Sawa, baadaye basi.”

Mama Anna alibeba nguo pea moja. Alipanga atakazovaa akienda siyo atakazovaa akirudi.

Wakati anatoka, Martha alikuwa amekaa nje na wapangaji wenzake...

“Mwenzetu mtoko wa wapi huo?” aliuliza Martha.

“Kwa shemeji yako.”

“Msalimie basi, siku nyingine mlete tumwone.”

“Wewe hujatuonesha wako lakini. Sanasana huyu wa sasa unasema ni kaka yako.”

“Ee! Kaka yangu jamani. Mjue ni kaka yangu, lakini mbona huwa mnamuita shemeji wakati niliwaambia ni kaka yangu!” alisisitiza Martha.

Walicheka wote, mama Anna akatokomea zake kwa kuchukua Bajaj hadi nyumbani kwa Roi. Anashuka tu, Roi naye anaegesha gari hapo.

Waliingia sambamba ndani huku Roi akimuuliza habari za alikotoka...

“Martha hajakuuliza kitu?”

“Hapana, kwani kuna kitu?”

“Aliniuliza asubuhi vile ulivyonisalimia kwa kuniita baby.”

“Kweli?” alishtuka mama Anna...

“Kweli, lakini usijali, yaliisha palepale. Alijua alisikia vibaya.”

Wawili hao hawakutaka kupoteza muda, waliingia chumbani, wakachojoana na wakapanda kitandani kuanza mechi.

Safari hii, mama Anna aliongeza gia namba kubwa zaidi kuliko jana yake. Mfano, wakiwa uwanjani, alimtoa kitandani Roi wakatembea mpaka bafuni na kurudi huku wakiendelea kucheka, Roi akapata ushindi wa kwanza ile anafika tu kitandani. Alianguka chini kwa jinsi alivyochokeshwa.

***

Martha kule nyumbani, akakumbuka kwamba alipanga kwenda kufanya usafi nyumbani kwa Roi, hivyo alijiandaa, akatoka akipanga kwamba atakapokaribia kufika ampigie simu Roi kumwambia ampitishie funguo za nyumba.

Share SIMULIZI HII LEO UTUMIWE INAYOFUATA MBELE
Powered by Blogger.