WALALAMIKA KWA KUTOTAJWA KATIKA FILAMU YA FURIOUS 7
The Rock, Vin Diesel na Paul Walker ni baadhi ya majina ambayo yametajwa mwishoni mwa filamu ya kusisimua ya "Furious 7" iliyoingia sokoni hivi karibuni ... tatizo ni kwamba kuna baadhi ya watu ambao walishiriki kikamilifu kwenye matukio muhimu ya filamu hiyo ambao hawakupewa 'credit' mwishoni.
Sehemu ya matukio waliyoshiriki watu hao.
Kundi hilo la watu waliosahaulika limeeleza kuwa lilitoa jumla ya watu 25 ambao walihatarisha maisha yao katika filamu hiyo japo hawajatajwa mwishoni mwa filamu hiyo iliyojizolea umaarufu na kufanya vizuri sokoni ndani ya muda mfupi tangu itolewe.
Filamu hiyo ilizinduliwa kwa mara ya kwanza huko Australia Aprili 2, 2015, na baadaye kuzinduliwa nchini Marekani Aprili 3, 2015, na baada ya hapo iliachiwa kimataifa katika mfumo wa 3D.
Post a Comment