Kitanzi, Kisu au Bastola - 13........Mwishooooo
Taratibu fahamu za Salima zilianza kumrudia. Aliweza kukumbuka kila kitu kilichokuwa kimetokea. Mbali na kumbukumbu hizo pia alimkumbuka Dedan na Carolina. Wasiwasi ulianza kumjaa kila mara alipowaza uwezekano wa Dedan kurudiana na msichana huyo ambaye muda huo ndiyo kwanza alianza kumkumbuka kuwa aliwahi kuonana naye mara kadhaa alipokuwa ‘Serenity.’

Akiwa katika mawazo hayo, mara mlango wa wodi aliyolazwa ulifunguliwa. Ndani yake akaingia Dedan aliyeongozana na Carolina. Ikawa kama vile Salima alivyowaza. Kweli Dedan alikuwa mikononi mwa Carolina tena huku wakionekana wenye furaha juu ya maisha yao mapya, japokuwa walijitahidi kuificha hali hiyo mbele ya Salima.
“Salima unaendeleaje?” Carolina alitangulia kuuliza baada ya kumuona Dedan akisitasita kumsalimia Salima ambaye hakujibu chochote zaidi ya kufumba macho yake huku machozi yakimlengalenga.
“Salima, najua uliteseka sana juu yangu kiasi cha kujiingiza katika matatizo makubwa ili unisadie. Kwa moyo wangu wote, naomba radhi kwa hilo. Nipo tayari kurudisha wema wako kwa kukupatia chochote utakacho, tafadhali niambie nikupe nini ili angalau nirudishe nusu ya fadhila zako,” aliongea Dedan akijitahidi kuikaza sauti yake huku akijaribu kutoathiriwa na machozi ya Salima.
“Naomba unipe kitanzi, kisu au bastola!” alijibu Salima kwa hasira.
“Una maanisha nini Salima?” aliuliza kwa mshtuko Dedan.
“Baada ya kupitia yote haya unadhani nitaishije? Si ni bora niukatishe uhai wangu kuliko kuishi kwa fedheha? Najua haukunipenda hata kidogo na najua siwezi kuubadilisha moyo wako ukanipenda mimi kama unavyompenda Carolina. Nyote wawili mna maisha mapya mbele yenu na mnapendana kwa dhati je, mimi nitabaki na nani? Niache nijiue,” aliongea Salima na kuangua kilio kikubwa.
Dondoo:
-Kwa msaada wa Carolina, Salima aliweza kupatiwa kazi na nyumba ya kuishi, lakini mbali na yote hayo bado upendo wake kwa Dedan ulikuwa palepale. Kitu cha ajabu ni kwamba Salima alianza kubadilika kitabia. Alianza kukopi kila kitu kutoka kwa Carolina, kuanzia muonekano wake hadi utembeaji. Moyoni akitarajia kuuteka moyo wa Dedan.
-Carolina na Dedan walishtukia tabia ya Salima, ili kuepuka kumuumiza msichana huyo, wakahamisha makazi yao na kuelekea mkoani Arusha ambapo walianza maisha mapya kwa kufunga pingu za maisha na kuishi kwa raha mustarehe kama mume na mke.
-Sonia alifanikiwa kukutana na watoto wake na kuanza maisha mapya. Kutokana na akiba ya fedha aliyoiacha mumewe, Sonia aliweza kuanzisha biashara mbalimbali jijini na kuweza kujikimu.
-Mr. Chakos na Madam Flaviana wote wawili walitupwa jela na kutumikia kifungo cha miaka 40 kila mmoja kwa makosa ya mauaji, utumwa na kukwepa kodi. Polisi nao wakiongozwa na Afande John bado walikuwa wakiendelea kumtafuta Mr. George wakiwa na matumaini ya kumtia nguvuni.
Mwisho.

Akiwa katika mawazo hayo, mara mlango wa wodi aliyolazwa ulifunguliwa. Ndani yake akaingia Dedan aliyeongozana na Carolina. Ikawa kama vile Salima alivyowaza. Kweli Dedan alikuwa mikononi mwa Carolina tena huku wakionekana wenye furaha juu ya maisha yao mapya, japokuwa walijitahidi kuificha hali hiyo mbele ya Salima.
“Salima unaendeleaje?” Carolina alitangulia kuuliza baada ya kumuona Dedan akisitasita kumsalimia Salima ambaye hakujibu chochote zaidi ya kufumba macho yake huku machozi yakimlengalenga.
“Salima, najua uliteseka sana juu yangu kiasi cha kujiingiza katika matatizo makubwa ili unisadie. Kwa moyo wangu wote, naomba radhi kwa hilo. Nipo tayari kurudisha wema wako kwa kukupatia chochote utakacho, tafadhali niambie nikupe nini ili angalau nirudishe nusu ya fadhila zako,” aliongea Dedan akijitahidi kuikaza sauti yake huku akijaribu kutoathiriwa na machozi ya Salima.
“Naomba unipe kitanzi, kisu au bastola!” alijibu Salima kwa hasira.
“Una maanisha nini Salima?” aliuliza kwa mshtuko Dedan.
“Baada ya kupitia yote haya unadhani nitaishije? Si ni bora niukatishe uhai wangu kuliko kuishi kwa fedheha? Najua haukunipenda hata kidogo na najua siwezi kuubadilisha moyo wako ukanipenda mimi kama unavyompenda Carolina. Nyote wawili mna maisha mapya mbele yenu na mnapendana kwa dhati je, mimi nitabaki na nani? Niache nijiue,” aliongea Salima na kuangua kilio kikubwa.
Dondoo:
-Kwa msaada wa Carolina, Salima aliweza kupatiwa kazi na nyumba ya kuishi, lakini mbali na yote hayo bado upendo wake kwa Dedan ulikuwa palepale. Kitu cha ajabu ni kwamba Salima alianza kubadilika kitabia. Alianza kukopi kila kitu kutoka kwa Carolina, kuanzia muonekano wake hadi utembeaji. Moyoni akitarajia kuuteka moyo wa Dedan.
-Carolina na Dedan walishtukia tabia ya Salima, ili kuepuka kumuumiza msichana huyo, wakahamisha makazi yao na kuelekea mkoani Arusha ambapo walianza maisha mapya kwa kufunga pingu za maisha na kuishi kwa raha mustarehe kama mume na mke.
-Sonia alifanikiwa kukutana na watoto wake na kuanza maisha mapya. Kutokana na akiba ya fedha aliyoiacha mumewe, Sonia aliweza kuanzisha biashara mbalimbali jijini na kuweza kujikimu.
-Mr. Chakos na Madam Flaviana wote wawili walitupwa jela na kutumikia kifungo cha miaka 40 kila mmoja kwa makosa ya mauaji, utumwa na kukwepa kodi. Polisi nao wakiongozwa na Afande John bado walikuwa wakiendelea kumtafuta Mr. George wakiwa na matumaini ya kumtia nguvuni.
Mwisho.
Post a Comment