ad

ad

ASHA BARAKA, ALI CHOKI SASA 'NO BEEF'


 
Ali Choki na Asha Baraka wakikumbatiana kumaliza bifu lao la muda mrefu.
 
Asha na Choki wakishow love ndani ya studio za Global TV Online baada ya upatanisho.
 
Choki na Asha wakiwa katika pozi na Mhariri Mtendaji wa Global Publishers Richard Manyota (wa pili kulia) aliyefanikisha kumalizika kwa bifu hilo. Kushoto ni Mhariri wa Gazeti la Ijumaa Wikienda Sifael Paul.
 

...Wakipeana mikono baada ya kumaliza bifu lao la muda mrefu.
 
Choki na Asha wakipata picha ya pamoja na Mhariri wa Gazeti la Risasi Jumamosi Erick Evarist.
 
Ali Choki na Asha Baraka wakiwa ndani ya studio za Global TV Online leo wakati wa kumaliza bifu lao.
 
Choki na Asha wakiwa katika picha ya pamoja na Manyota (wa pili kulia). Kushoto ni Mhariri Kiongozi wa Magazeti ya Championi Saleh Ally.
Choki akiteta jambo na Manyota (kulia) na Saleh kabla ya upatanisho.
BIFU lililodumu kwa muda mrefu kati ya Mkurugenzi wa Bendi ya Twanga Pepeta, Asha Baraka na Mkurugenzi wa Bendi ya Extra Bongo, Ali Choki leo limemalizika rasmi katika ofisi za Global Publishers Ltd zilizopo Mwenge, Bamaga jijini Dar.
Juhudi za kuwapatanisha wakongwe hao katika muziki wa dansi zimefanywa na baadhi ya viongozi wa Global Publishers ambap wanakiri kuwa halikuwa jambo rahisi kuwapatanisha viongozi hao.
Wakongwe hao katika muziki wa dansi wameamua kumaliza tofauti zao na kuwa kitu kimoja huku wakiahidi kushirikiana katika muziki na mambo mengine.
Mbali na mengi yaliyoongea pia wamekubaliana kufanya onyesho la pamoja huko mbeleni kuwadhihirishia mashabiki kuwa kwa sasa hawana bifu lolote na wamekuwa kama ilivyokuwa awali.
Mtandao huu unawapongeza na kuwatakia kila la kheri viongozi hao kwa uamuzi sahii waliouchukua ili kuzidi kusukuma gurudumu la muziki wa dansi.
(PICHA NA GPL)

No comments

Powered by Blogger.