KALA JEREMIAH AENDELEA KUWA BALOZI WA PEPSI NCHINI
Washindi watatu walioshinda shilingi laki tano kila mmoja baada ya kunywa Pepsi.
MSANII, Kala Jeremiah ameendelea kuwa balozi wa
kinywaji cha Pepsi nchini kwa msimu mwingine, Hayo yamezungumza na
Meneja Mafunzi wa SBC , Rashid Chenje , hii leo katika Ukumbi wa Maelezo
uliopo Posta, jijini Dar e s Salaam, wakati akizindua shindano jipya
la ‘’Jishindie mamilioni kila siku na Pepsi’’Aidha Pepsi wametoa zawadi za Papo kwa Papo baada ya waandishi kunywa soda za Pepsi na waandishi watatu kuibuka washindi wa shilingi laki tano kwa kila mshindi.
Shindano hilo limeanza rasmi leo na litamalizika 21/12/2014 huku mwisho wa kutoa zawadi, ni tarehe 30 January 2015, ambapo kila siku mshindi mmoja wa shilingi milioni moja taslimu atajishindia kwa kunywa soda za kampuni hiyo.
(Na Gabriel Ng’osha/GPL)

Post a Comment