ad

ad

EXCLUSIVE: MKUDE AMWAGA WINO SIMBA, MIAKA MIWILI, WALIOMTAKA WOTE KIMYAAA

MKUDE AKISAINI MKATABA LEO MBELE YA RAIS WA SIMBA, EVANS AVEVA
Hatimaye kiungo Jonas Mkude amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Simba.

Mkude amesaini mkataba huo leo mbele ya Rais wa Simba, Evans Aveva.
Pamoja na Aveva na viongozi wengine wa Simba akiwemo Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, Mkude alisaini mkataba huo mbele ya waandishi wa habari.
Awali kulikuwa na taarifa kwamba Mkude ameishaongeza mkataba Simba.

Lakini akaieleza blogu hii hakuwa tayari amefanya hivyo. Lakini hatimaye Simba imemaliza kazi leo na kuwakata maini wapinzani wao Yanga na Azam FC waliokuwa wameanza kumtolea jicho.

No comments

Powered by Blogger.