AHADI YA NDOTONI - 09
Ilipoishia wiki iliyopita:
“Unayakumbuka maswali ya baba zako wadogo?”
“Ndiyo.”
“Kwa nini ulikasirika?”
“Maswali yao yalikuwa hayana msingi.”
“Sasa mpaka iwe vipi ndiyo ujue kuwa hao siyo watu wema?”
“Mmh!” Lakashina alikosa jibu na kuguna tu.
Endelea sasa....
“Sikiliza mpenzi, mimi kukuonya nimeona mbali sana.”
“Ina maana wewe ndiye unayenipigia simu?”
“Lakashina siku zote nakufundisha kitu kimoja, unapoonywa usitake kuangalia nani anakuonya la muhimu kumuelewa.”
“Sasa kama ni wewe mbona unakuja kwa lugha ya kunitisha?”
“Lakashina mimi si unaniona, kwa nini nije kwa sauti?”
“Sasa yule ni nani?”
“Kwani kipi amekueleza kibaya?”
“Hakuna, ila hunitisha sana.”
“Nakuomba umsikilize, ni mwema kwako acha kumjibu maneno ya kiburi.”
“Sawa nimekuelewa mume wangu.”
“Niambie tatizo nini?”
“Nataka niwe na wewe siku zote.”
“Hata mimi najua jinsi gani ninavyotaka kuwa na wewe karibu, vumilia muda bado.”
“Muda bado mpaka lini?”
“Sijajua, nimekueleza nasafiri.”
“Mbona upo?”
“Lakashina mke wangu, nipo nawe ndotoni lakini si kimwili. Nilikueleza nitakuwa nawe muda wote wa majonzi yako.”
“Kumbuka nateseka, nahitaji kuwa karibu yako muda wote, Lakashina nakupenda mume wangu.”
“Hata mimi nakupenda ndiyo maana kila kukicha nayaimarisha maisha yako.”
“Ni kweli mume wangu, kwa hilo nashukuru.”
“Basi nakuomba umsikilize rafiki yangu.”
“Mume wangu siwezi kupanda farasi wawili.”
“Una maana gani?”
“Ulinieleza nikusikilize wewe tu.”
“Ni kweli lakini kwenye matatizo hata kama sipo msikilize, ni mtu mwema sana kwako.”
“Sawa lakini naomba niwe na mdogo wangu.”
“Kwani yeye alikueleza nini?”
“Eti ni mtu mbaya.”
“Yaweza kuwa kweli.”
“Kwa hiyo nimrudishe?”
“Ikiwezekana.”
“Kwa hili mume wangu sikubaliani nalo, toka amekuwa hapa furaha yangu imeongezeka mara dufu.”
“Mmh! Haya.”
“Umekasirika?”
“Ili iweje.”
“Kwa hiyo umenikubalia?”
“Nimekukubalia.”
“Asante mume wangu,” Lakashina alimkumbatia mume wake kwa furaha, alishtuka usingizini na kujikuta ameukumbatia mto. Lakini chumba chote kilikuwa na manukato ya mumewe Lakashina.
****
Tokea siku ile Lakashina aliamini kuipata haki yake lazima afanye kiburi, kwa kauli ya mumewe japo ilikuwa na mashaka, hakuwa tayari kuitii amri ya sauti ya kiumbe asichokijua na kusimamia uamuzi wake ambao aliuona kila siku upo sawa japo ni mwanamke.
Shughuli zake nazo zilikwenda kama alivyopanga na mapato kila kukicha yaliongezeka. Ilifika hatua hata muda wa kuswali akawa anakosa zaidi ya kushughulika na biashara zake na aliporudi nyumbani alikuwa amechoka sana. Ndotoni alijiwa na mumewe aliyemkumbusha kuswali lakini alipuuza na kuendelea na kazi zake ambazo kila muda ziliongezeka na kupanuka.
Akiwa katika kazi zake, alikutana na watu wengi akiwemo kijana mmoja ambaye alionesha ushirikiano mkubwa kiasi cha kumteka akili. Lakashina akiwa chumbani kwake kitandani alijikuta akimjaza akilini kijana yule ambaye alionesha ni mstaarabu sana.
Alikumbuka siku moja katika kazi zake Lakashina aliposahau mkoba wake uliokuwa na pesa nyingi lakini kijana yule alimpelekea tofauti na vijana wengine ambao walikuwa wanamuibia hata pesa kidogo. Pia swali la kijana yule liliupasua moyo wake na kumuweka kwenye wakati mgumu pale alipomuuliza:
“Lakashina umeolewa?”
“Mbona umeniuliza hivyo?”
“Katika maisha yangu sikuwahi kuwaza kumuona mwanamke kama wewe.”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Lakashina una kila sifa za mwanamke mwenye kuifahamu thamani yake.”
“Kivipi?”
“Kwanza muumba kakujalia umbile na sura, pili kakujalia heshima busara na ustaarabu pia huruma na mwisho pamoja na utajiri wako bado huridhiki.”
“Ni hayo tu,” Lakashina alimwambia kijana yule kwa sauti ya chini huku akiwa ameangalia chini kwa aibu.
“Ni mengi sana ambayo kama mbingu ingekuwa karatasi na bahari ni wino vingejaa na wino kukauka lakini sifa zako zisingeisha.”
“Unanipamba tu Sadat.”
“Ni kweli, huwezi kujiona bila kuonwa.”
“Kama ndiyo hivyo nashukuru.”
“Basi nijibu, umeolewa?”
“Nitakupa jibu tukionana, naomba uniache kwa leo.”
Lakashina alirudisha mawazo yake na kutabasamu huku akijiuliza ampe Sadat jibu gani ili asimuudhi moyoni mwake.
Akiwa kwenye mawazo mazito juu ya uamuzi wake mzito wa kutoa jibu kwa Sadat, simu yake iliita. Aliichukua simu na kuipokea.
“Haloo.”
“Haloo.” Sauti nzito ya upande wa pili ilipokea.
“Unasemaje?” aliuliza kwa hasira.
“Lakashina nakupa onyo la mwisho.”
“Kuhusu nini?”
“Kwa yote niliyokueleza na hili unalowaza.”
“Nawaza nini?”
“Unalijua lakini ukifanya unachowaza tusilaumiane.”
“Nimeishakueleza maisha yangu hayakutegemei wewe ila Mungu.”
“Hicho ndicho kitakachokuponza.”
“Nimekueleza usinitishe na sitakuogopa.”
“Narudia tena japo masikio yako yamejaa kutu mpaka yatoke damu, zingatia yote ninayokueleza. Nakuonea huruma kwa kuingia kwenye matatizo makubwa.”
“Hata yakinikuta wewe yanakuhusu nini?”
“Eeh, leo unasema hivyo?”
“Ndiyo.”
“Kwa heri.”
Simu ile ilikatika ghafla, Lakashina alitulia kwa muda akiwaza sauti ile ni ya nani na kwa nini kila anapotaka kufanya jambo lake hutokea na kumpa onyo. Lakini aliamini uamuzi aishi maisha gani anao yeye mwenyewe, hata kuwa karibu na ndugu zake sauti ile ilikataa. Kwa uamuzi wake mwenyewe aliweza kuungana na familia yake. Hata vitisho alipopewa kuhusu mdogo wake kila kukicha hakuviona.
Alitupia simu pembeni aliyokuwa bado ameshikilia mkononi, aliamua kujilaza akiwa na hasira ya kusumbuliwa na sauti iliyokuwa ikimnyima raha kila alipokuwa na furaha moyoni mwake. Kuendelea kulala alikuwa akitaka mumewe aje ndotoni ili amueleze ukweli kuchoshwa kuendelea kutishwa na sauti ya mtu asiyeonekana na ikiwezekana waachane kabisa na yupo tayari kurudia maisha yake ya zamani.
Aliamini maisha ya masharti hayana uhuru, pia alijua kama ataachana na Lakashi lazima ataolewa na Sadat kijana mwenye pesa tena mwenye mapenzi ya dhati kwake kuliko kuendelea kuishi na kiumbe wa ajabu kama Lakashi.
Alipojilaza usingizi haukuchelewa kumchukua lakini mpaka anashtuka mumewe Lakashi hakuonekana ndotoni.
Ajabu ilionesha alilala sana na kuamka muda umekwenda sana ilikuwa inakimbilia mchana. Alipoamka alijawa na maswali mengi juu kulala bila kujiwa ndotoni mumewe, alikumbuka njia nyingine ya kumwita kwa kuchoma manukato aliyoelekezwa na mumewe.
Akiwa mtu mwenye hasira aliingia chumbani na kuchoma manukato lakini alisahau kufuata maelekezo ya kuchukua udhu kabla ya kufanya vile. Alichoma manukato yale na kutulia kwa muda lakini mpaka moshi unapotea hakukuwa na dalili zozote za kuonekana Lakashi. Baada ya kumkosa mumewe kwa hasira alisema:
“Na huyu mtu anayenijia kwa sauti akinitokea nitampa vipande vyake na tena anikome.”
Baada ya kusema vile, vilizuka vicheko mfululizo vilivyoonesha kumcheka yeye, aligeuka kumtafuta anayemcheka hakumuona kwa hasira alisema:
“Kama wanaume kweli mbona mnajificha, nakuhakikishieni kufanya mambo ninayoyataka mimi na siyo nyie.”
Alikwenda kuoga kujiandaa kwenda kwenye biashara zake ambazo kila kukicha zilizidi kupanuka, akiwa anajifuta simu yake iliita tena. Hakutaka kuichukua aliiacha iite mpaka ikate. Baada ya kumaliza kujipamba aliichukua simu na kuangalia nani aliyepiga, alishtuka kuona ni Sadat.
Kwa haraka alimpigia simu, baada ya kuita ilipokelewa.
“Haloo.”
“Haloo, Sadat.”
“Lakashina.”
“Ndiyo mimi, Samahani kwa kutopokea simu yako, kuna mjinga mmoja alikuwa akinisumbua.”
“Bila samahani, nilidhani labda ombi langu ndilo lililokuudhi.”
“Hapana Sadat, wewe ni mtu muhimu sana kwangu siwezi kukufanyia hivyo.”
“Nani kakuudhi tena malkia wa moyo wangu?”
“Achana naye tuzungumze yetu.”
“Upo wapi?”
“Nyumbani.”
“Mbona leo umechelewa sana, au huji mjini?”
“Aah, uchovu tu, nakuja sasa hivi.”
“Bado hujatoka nyumbani?”
“Nipo njiani.”
“Basi nakusubiri.”
“Shaka ondoa.”
Lakashina alikwenda kwenye gari lake na kuelekea kwenye biashara zake, njiani alijikuta akimchukua Lakashi na kumpa nafasi Sadat, alijua mapenzi na jini yana masharti makubwa na ukikosea lazima upate matatizo. Lakini Sadat ni mwanadamu ambaye mapenzi na maisha yake hayana masharti yoyote.
Alipanga kumueleza ukweli juu ya uamuzi wake wa kuvunja ndoa yao ya ndotoni na kuolewa na mwanadamu mwenzake. Japo alijua itakuwa si rahisi Lakashi kukubali lakini aliamini penzi la kweli halilazimishwi.
Lakashina alijikuta akihamisha mawazo yake yote kwa Sadat mwanaume ambaye aliugusa moyo wake na kutamani siku moja awe mumewe. Alipofika dukani kwake bila kutulia alimpigia simu Sadat amfuate wakapate chakula cha mchana.
Sadat alifika dukani baada ya muda mfupi, waliongozana wote hadi kwenye hoteli iliyokuwa karibu kupata chakula cha mchana. Baada ya mhudumu kuchukua mahitaji yao aliondoka na kuwaacha wakizungumza.
“Mh, Lakashina lete habari.”
“Aah, kawaida tu.”
“Mbona leo umechelewa?”
“Si muhimu kuyajua tuzungumze yetu.”
“Basi jana usiku nilipokupigia simu nilikuwa nimeshtuka usingizini baada ya kuota tupo ufukweni tukipunga upepo na niliposhtuka nikajikuta nipo kitandani peke yangu.”
“Ooh, po...,” Lakashina alishtuka kumuona mtu kama mumewe Lakashi akipita mbele ya meza yao, harufu ya manukato apendayo kujipaka ilikatisha kwenye pua zake.
“Vipi?” Sadat alishtuka baada ya kumuona Lakashina akishangaa.
“Hebu ngoja,” Lakashina alinyanyuka kumfuata mtu aliyemfananisha na mumewe aliyekuwa amesimama amempa mgongo akizungumza na mtu ili kupata uhakika.
Alikwenda mpaka sehemu ile na kumpita, alipomuangalia usoni hakuwa yeye, alishusha pumzi na kurudi kwenye meza yake. Alipoketi Sadat alimuuliza.
“Vipi Lakashina?”
“Hapana.”
“Kuna kitu gani, naona umenyamaza ghafla na kunyanyuka, umeona nini?”
“Achana nayo tuendelee na yetu.”
“Mh, umefikia wapi?”
“Kuhusu nini?”
“Jibu langu.”
“Sadat lazima nikwambie ukweli toka moyoni mwangu hata mimi nakupenda.”
“Sasa basi nipe jibu langu.”
“Naomba unipe muda.”
“Kuna kipingamizi gani cha kuchelewesha jibu?”
“Hakuna kipingamizi si unajua jambo zuri halihitaji haraka.”
“Lakashina, kumbuka moyo wangu wote nimekuachia wewe, kwa nini usiniruhusu kuwa sehemu ya pili ya mwili wako?”
“Unajua Sadat mi...,” Lakashina alinyamaza tena kimya baada ya kumuona mumewe Lakashi akiwa amekaa meza ya jirani akiwa amemkazia macho, kitu kile kilimshtua tena Sadat.
“Lakashina vipi tena?”
Hakumjibu kitu, aliendelea kumkazia macho mtu aliye mbele yake ambaye aliamini kabisa ni mumewe Lakashi.
Mtu yule aliendelea kutulia akiwa amemuangalia huku machozi yakimtoka, ilikuwa ajabu ya mumewe Lakashi kunywa pombe, kitu kilichokuwa haramu kwake na kumzuia hata yeye mwenyewe asinywe pombe.
“Lakashina vipi?” Sadat aliuliza huku akigeuka kumuangalia mtu aliyekuwa meza ya mbele yao.
Lakashina ambaye moyo ulikuwa umemlipuka na kwenda mbio, bado aliendelea kukaza macho yake kama kaona kitu cha ajabu ambacho hajawahi kukiona maishani mwake.
Sadat baada ya kuchanganywa na hali ile alinyanyuka na kuwafuata meza ya pili kutaka kujua wamemfanya nini Lakashina.
“Samahani ndugu.”
“Bila samahani.”
“Eti mmemfanya nini huyu mwanamke?”
“Sisi?”
“Ndiyo.”
”Kwani amekwambia tumemfanya nini?”
“Hata mimi nashangaa, tulikuwa tunazungumza mara aliwatazama na kushindwa kuendelea kuzungumza.”
“Muulize vizuri, sisi hapa tuna mazungumzo yetu wala hatuna habari na meza yenu.”
“Eti wamekufanya nini?” Sadat alimuuliza Lakashina.
Swali la Sadat kwa Lakashina lilikuwa kama kumzindua
Like: www.facebook.com/2jiachie
Web: www.2jiachie.com
ITAENDELEA SIKU YA KESHOOOOOOOO
“Unayakumbuka maswali ya baba zako wadogo?”
“Ndiyo.”
“Kwa nini ulikasirika?”
“Maswali yao yalikuwa hayana msingi.”
“Sasa mpaka iwe vipi ndiyo ujue kuwa hao siyo watu wema?”
“Mmh!” Lakashina alikosa jibu na kuguna tu.
Endelea sasa....
“Sikiliza mpenzi, mimi kukuonya nimeona mbali sana.”
“Ina maana wewe ndiye unayenipigia simu?”
“Lakashina siku zote nakufundisha kitu kimoja, unapoonywa usitake kuangalia nani anakuonya la muhimu kumuelewa.”
“Sasa kama ni wewe mbona unakuja kwa lugha ya kunitisha?”
“Lakashina mimi si unaniona, kwa nini nije kwa sauti?”
“Sasa yule ni nani?”
“Kwani kipi amekueleza kibaya?”
“Hakuna, ila hunitisha sana.”
“Nakuomba umsikilize, ni mwema kwako acha kumjibu maneno ya kiburi.”
“Sawa nimekuelewa mume wangu.”
“Niambie tatizo nini?”
“Nataka niwe na wewe siku zote.”
“Hata mimi najua jinsi gani ninavyotaka kuwa na wewe karibu, vumilia muda bado.”
“Muda bado mpaka lini?”
“Sijajua, nimekueleza nasafiri.”
“Mbona upo?”
“Lakashina mke wangu, nipo nawe ndotoni lakini si kimwili. Nilikueleza nitakuwa nawe muda wote wa majonzi yako.”
“Kumbuka nateseka, nahitaji kuwa karibu yako muda wote, Lakashina nakupenda mume wangu.”
“Hata mimi nakupenda ndiyo maana kila kukicha nayaimarisha maisha yako.”
“Ni kweli mume wangu, kwa hilo nashukuru.”
“Basi nakuomba umsikilize rafiki yangu.”
“Mume wangu siwezi kupanda farasi wawili.”
“Una maana gani?”
“Ulinieleza nikusikilize wewe tu.”
“Ni kweli lakini kwenye matatizo hata kama sipo msikilize, ni mtu mwema sana kwako.”
“Sawa lakini naomba niwe na mdogo wangu.”
“Kwani yeye alikueleza nini?”
“Eti ni mtu mbaya.”
“Yaweza kuwa kweli.”
“Kwa hiyo nimrudishe?”
“Ikiwezekana.”
“Kwa hili mume wangu sikubaliani nalo, toka amekuwa hapa furaha yangu imeongezeka mara dufu.”
“Mmh! Haya.”
“Umekasirika?”
“Ili iweje.”
“Kwa hiyo umenikubalia?”
“Nimekukubalia.”
“Asante mume wangu,” Lakashina alimkumbatia mume wake kwa furaha, alishtuka usingizini na kujikuta ameukumbatia mto. Lakini chumba chote kilikuwa na manukato ya mumewe Lakashina.
****
Tokea siku ile Lakashina aliamini kuipata haki yake lazima afanye kiburi, kwa kauli ya mumewe japo ilikuwa na mashaka, hakuwa tayari kuitii amri ya sauti ya kiumbe asichokijua na kusimamia uamuzi wake ambao aliuona kila siku upo sawa japo ni mwanamke.
Shughuli zake nazo zilikwenda kama alivyopanga na mapato kila kukicha yaliongezeka. Ilifika hatua hata muda wa kuswali akawa anakosa zaidi ya kushughulika na biashara zake na aliporudi nyumbani alikuwa amechoka sana. Ndotoni alijiwa na mumewe aliyemkumbusha kuswali lakini alipuuza na kuendelea na kazi zake ambazo kila muda ziliongezeka na kupanuka.
Akiwa katika kazi zake, alikutana na watu wengi akiwemo kijana mmoja ambaye alionesha ushirikiano mkubwa kiasi cha kumteka akili. Lakashina akiwa chumbani kwake kitandani alijikuta akimjaza akilini kijana yule ambaye alionesha ni mstaarabu sana.
Alikumbuka siku moja katika kazi zake Lakashina aliposahau mkoba wake uliokuwa na pesa nyingi lakini kijana yule alimpelekea tofauti na vijana wengine ambao walikuwa wanamuibia hata pesa kidogo. Pia swali la kijana yule liliupasua moyo wake na kumuweka kwenye wakati mgumu pale alipomuuliza:
“Lakashina umeolewa?”
“Mbona umeniuliza hivyo?”
“Katika maisha yangu sikuwahi kuwaza kumuona mwanamke kama wewe.”
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Lakashina una kila sifa za mwanamke mwenye kuifahamu thamani yake.”
“Kivipi?”
“Kwanza muumba kakujalia umbile na sura, pili kakujalia heshima busara na ustaarabu pia huruma na mwisho pamoja na utajiri wako bado huridhiki.”
“Ni hayo tu,” Lakashina alimwambia kijana yule kwa sauti ya chini huku akiwa ameangalia chini kwa aibu.
“Ni mengi sana ambayo kama mbingu ingekuwa karatasi na bahari ni wino vingejaa na wino kukauka lakini sifa zako zisingeisha.”
“Unanipamba tu Sadat.”
“Ni kweli, huwezi kujiona bila kuonwa.”
“Kama ndiyo hivyo nashukuru.”
“Basi nijibu, umeolewa?”
“Nitakupa jibu tukionana, naomba uniache kwa leo.”
Lakashina alirudisha mawazo yake na kutabasamu huku akijiuliza ampe Sadat jibu gani ili asimuudhi moyoni mwake.
Akiwa kwenye mawazo mazito juu ya uamuzi wake mzito wa kutoa jibu kwa Sadat, simu yake iliita. Aliichukua simu na kuipokea.
“Haloo.”
“Haloo.” Sauti nzito ya upande wa pili ilipokea.
“Unasemaje?” aliuliza kwa hasira.
“Lakashina nakupa onyo la mwisho.”
“Kuhusu nini?”
“Kwa yote niliyokueleza na hili unalowaza.”
“Nawaza nini?”
“Unalijua lakini ukifanya unachowaza tusilaumiane.”
“Nimeishakueleza maisha yangu hayakutegemei wewe ila Mungu.”
“Hicho ndicho kitakachokuponza.”
“Nimekueleza usinitishe na sitakuogopa.”
“Narudia tena japo masikio yako yamejaa kutu mpaka yatoke damu, zingatia yote ninayokueleza. Nakuonea huruma kwa kuingia kwenye matatizo makubwa.”
“Hata yakinikuta wewe yanakuhusu nini?”
“Eeh, leo unasema hivyo?”
“Ndiyo.”
“Kwa heri.”
Simu ile ilikatika ghafla, Lakashina alitulia kwa muda akiwaza sauti ile ni ya nani na kwa nini kila anapotaka kufanya jambo lake hutokea na kumpa onyo. Lakini aliamini uamuzi aishi maisha gani anao yeye mwenyewe, hata kuwa karibu na ndugu zake sauti ile ilikataa. Kwa uamuzi wake mwenyewe aliweza kuungana na familia yake. Hata vitisho alipopewa kuhusu mdogo wake kila kukicha hakuviona.
Alitupia simu pembeni aliyokuwa bado ameshikilia mkononi, aliamua kujilaza akiwa na hasira ya kusumbuliwa na sauti iliyokuwa ikimnyima raha kila alipokuwa na furaha moyoni mwake. Kuendelea kulala alikuwa akitaka mumewe aje ndotoni ili amueleze ukweli kuchoshwa kuendelea kutishwa na sauti ya mtu asiyeonekana na ikiwezekana waachane kabisa na yupo tayari kurudia maisha yake ya zamani.
Aliamini maisha ya masharti hayana uhuru, pia alijua kama ataachana na Lakashi lazima ataolewa na Sadat kijana mwenye pesa tena mwenye mapenzi ya dhati kwake kuliko kuendelea kuishi na kiumbe wa ajabu kama Lakashi.
Alipojilaza usingizi haukuchelewa kumchukua lakini mpaka anashtuka mumewe Lakashi hakuonekana ndotoni.
Ajabu ilionesha alilala sana na kuamka muda umekwenda sana ilikuwa inakimbilia mchana. Alipoamka alijawa na maswali mengi juu kulala bila kujiwa ndotoni mumewe, alikumbuka njia nyingine ya kumwita kwa kuchoma manukato aliyoelekezwa na mumewe.
Akiwa mtu mwenye hasira aliingia chumbani na kuchoma manukato lakini alisahau kufuata maelekezo ya kuchukua udhu kabla ya kufanya vile. Alichoma manukato yale na kutulia kwa muda lakini mpaka moshi unapotea hakukuwa na dalili zozote za kuonekana Lakashi. Baada ya kumkosa mumewe kwa hasira alisema:
“Na huyu mtu anayenijia kwa sauti akinitokea nitampa vipande vyake na tena anikome.”
Baada ya kusema vile, vilizuka vicheko mfululizo vilivyoonesha kumcheka yeye, aligeuka kumtafuta anayemcheka hakumuona kwa hasira alisema:
“Kama wanaume kweli mbona mnajificha, nakuhakikishieni kufanya mambo ninayoyataka mimi na siyo nyie.”
Alikwenda kuoga kujiandaa kwenda kwenye biashara zake ambazo kila kukicha zilizidi kupanuka, akiwa anajifuta simu yake iliita tena. Hakutaka kuichukua aliiacha iite mpaka ikate. Baada ya kumaliza kujipamba aliichukua simu na kuangalia nani aliyepiga, alishtuka kuona ni Sadat.
Kwa haraka alimpigia simu, baada ya kuita ilipokelewa.
“Haloo.”
“Haloo, Sadat.”
“Lakashina.”
“Ndiyo mimi, Samahani kwa kutopokea simu yako, kuna mjinga mmoja alikuwa akinisumbua.”
“Bila samahani, nilidhani labda ombi langu ndilo lililokuudhi.”
“Hapana Sadat, wewe ni mtu muhimu sana kwangu siwezi kukufanyia hivyo.”
“Nani kakuudhi tena malkia wa moyo wangu?”
“Achana naye tuzungumze yetu.”
“Upo wapi?”
“Nyumbani.”
“Mbona leo umechelewa sana, au huji mjini?”
“Aah, uchovu tu, nakuja sasa hivi.”
“Bado hujatoka nyumbani?”
“Nipo njiani.”
“Basi nakusubiri.”
“Shaka ondoa.”
Lakashina alikwenda kwenye gari lake na kuelekea kwenye biashara zake, njiani alijikuta akimchukua Lakashi na kumpa nafasi Sadat, alijua mapenzi na jini yana masharti makubwa na ukikosea lazima upate matatizo. Lakini Sadat ni mwanadamu ambaye mapenzi na maisha yake hayana masharti yoyote.
Alipanga kumueleza ukweli juu ya uamuzi wake wa kuvunja ndoa yao ya ndotoni na kuolewa na mwanadamu mwenzake. Japo alijua itakuwa si rahisi Lakashi kukubali lakini aliamini penzi la kweli halilazimishwi.
Lakashina alijikuta akihamisha mawazo yake yote kwa Sadat mwanaume ambaye aliugusa moyo wake na kutamani siku moja awe mumewe. Alipofika dukani kwake bila kutulia alimpigia simu Sadat amfuate wakapate chakula cha mchana.
Sadat alifika dukani baada ya muda mfupi, waliongozana wote hadi kwenye hoteli iliyokuwa karibu kupata chakula cha mchana. Baada ya mhudumu kuchukua mahitaji yao aliondoka na kuwaacha wakizungumza.
“Mh, Lakashina lete habari.”
“Aah, kawaida tu.”
“Mbona leo umechelewa?”
“Si muhimu kuyajua tuzungumze yetu.”
“Basi jana usiku nilipokupigia simu nilikuwa nimeshtuka usingizini baada ya kuota tupo ufukweni tukipunga upepo na niliposhtuka nikajikuta nipo kitandani peke yangu.”
“Ooh, po...,” Lakashina alishtuka kumuona mtu kama mumewe Lakashi akipita mbele ya meza yao, harufu ya manukato apendayo kujipaka ilikatisha kwenye pua zake.
“Vipi?” Sadat alishtuka baada ya kumuona Lakashina akishangaa.
“Hebu ngoja,” Lakashina alinyanyuka kumfuata mtu aliyemfananisha na mumewe aliyekuwa amesimama amempa mgongo akizungumza na mtu ili kupata uhakika.
Alikwenda mpaka sehemu ile na kumpita, alipomuangalia usoni hakuwa yeye, alishusha pumzi na kurudi kwenye meza yake. Alipoketi Sadat alimuuliza.
“Vipi Lakashina?”
“Hapana.”
“Kuna kitu gani, naona umenyamaza ghafla na kunyanyuka, umeona nini?”
“Achana nayo tuendelee na yetu.”
“Mh, umefikia wapi?”
“Kuhusu nini?”
“Jibu langu.”
“Sadat lazima nikwambie ukweli toka moyoni mwangu hata mimi nakupenda.”
“Sasa basi nipe jibu langu.”
“Naomba unipe muda.”
“Kuna kipingamizi gani cha kuchelewesha jibu?”
“Hakuna kipingamizi si unajua jambo zuri halihitaji haraka.”
“Lakashina, kumbuka moyo wangu wote nimekuachia wewe, kwa nini usiniruhusu kuwa sehemu ya pili ya mwili wako?”
“Unajua Sadat mi...,” Lakashina alinyamaza tena kimya baada ya kumuona mumewe Lakashi akiwa amekaa meza ya jirani akiwa amemkazia macho, kitu kile kilimshtua tena Sadat.
“Lakashina vipi tena?”
Hakumjibu kitu, aliendelea kumkazia macho mtu aliye mbele yake ambaye aliamini kabisa ni mumewe Lakashi.
Mtu yule aliendelea kutulia akiwa amemuangalia huku machozi yakimtoka, ilikuwa ajabu ya mumewe Lakashi kunywa pombe, kitu kilichokuwa haramu kwake na kumzuia hata yeye mwenyewe asinywe pombe.
“Lakashina vipi?” Sadat aliuliza huku akigeuka kumuangalia mtu aliyekuwa meza ya mbele yao.
Lakashina ambaye moyo ulikuwa umemlipuka na kwenda mbio, bado aliendelea kukaza macho yake kama kaona kitu cha ajabu ambacho hajawahi kukiona maishani mwake.
Sadat baada ya kuchanganywa na hali ile alinyanyuka na kuwafuata meza ya pili kutaka kujua wamemfanya nini Lakashina.
“Samahani ndugu.”
“Bila samahani.”
“Eti mmemfanya nini huyu mwanamke?”
“Sisi?”
“Ndiyo.”
”Kwani amekwambia tumemfanya nini?”
“Hata mimi nashangaa, tulikuwa tunazungumza mara aliwatazama na kushindwa kuendelea kuzungumza.”
“Muulize vizuri, sisi hapa tuna mazungumzo yetu wala hatuna habari na meza yenu.”
“Eti wamekufanya nini?” Sadat alimuuliza Lakashina.
Swali la Sadat kwa Lakashina lilikuwa kama kumzindua
Like: www.facebook.com/2jiachie
Web: www.2jiachie.com
ITAENDELEA SIKU YA KESHOOOOOOOO

Post a Comment