AHADI YA NDOTONI - 04
ILIPOISHIA:
“Kweli mama umekuwa mkali kauli zako hata mimi nilijisikia vibaya, ni kweli Jeska alikuwa amefanya kosa hatukutakiwa kutumia vitisho aseme nani aliyempa ujauzito. Lazima angesema tu kama alivyosema alichanganywa na kitendo cha kubakwa, hata ningefanyiwa mimi ningeumia.”
“Sasa atakuwa wapi?”
“Ni vigumu kujua la muhimu tumsubiri baba arudi atatusaidia akiisoma hii barua.”
Endelea...
“Mmh, mwaka huu mbona Jeska ametuchanganya akili,” mama Edna alisema huku akiirudisha barua kwenye bahasha.
Mara simu ya Edna iliita alipoangalia ilikuwa namba ngeni machoni mwake, aliipokea na kusema.
“Haloo”
“Haloo Edna,” sauti ya upande wa pili ilisema.
“Nani mwenzangu?”
“Mimi Jeska.”
“Jeska! Jamani Jeska upo wapi ndugu yangu?”
“Kabla ya yote barua mmeipata?”
“Ndiyo, upo wapi mbona umeondoka nyumbani bado tunakuhitaji?”
“Edna sipo mbali ila baada ya muda nitarudi nyumbani, kama nilivyosema.”
“Lakini ipo wapi?”
“Nimekwambia sipo mbali, akili yangu ikitulia na nikiwa tayari kuyasema mbele yenu nitarudi nyumbani, msalimie mama.”
“Huyu hapa,” Edna alisema huku akimpa simu mama yake.
“Haloo Jeska.”
“Abee mama, shikamoo.”
“Marahaba, upo wapi mama rudi nyumbani...yote yamekwisha ilikuwa ni hasira tu mwanangu.”
“Najua mama, ila usiwe na wasiwasi nitarudi tu mama nakupenda sana.”
“Najua mwanangu chonde chonde mwanangu rudi walimwengu hawatanielewa, hata nduguyo anasema matatizo yote chanzo ni mimi.”
“Hapana mama, nitarudi.”
Jeska alikata simu na kuizima kila walipompigia hakupatikana.
****
Jeska baada ya kurudi kutoka kwa mzee Ezekiel kupeleka barua kutokana na makubaliano yake na mzee Ezekiel kuwa aandike barua ya kuwatoa wasiwasi ili familia yake itulie isimtafute. Baada ya kurudi hotelini kwake alitulia na kumjulisha mzee Ezekiel kwa simu.
“Tayari baba.”
“Vizuri, umempa nani?”
“Mlinzi.”
“Amekuona?”
“Ndiyo.”
“Amesemaje?”
“Alionesha kunishangaa lakini sikumpa muda wa kuuliza swali zaidi ya kuondoka nikimwacha akinitumbulia macho.”
“Jeska umefanya kitu kizuri sana, nakuhakikishia kuyabadili maisha yako kama shukurani ya kuificha siri ambayo ingenichafua.”
“Nitashukuru”
Mzee Ezekiel muda ule aliamua kurudi nyumbani ili akasikie wamepokeaje barua ya Jeska, alipofika nyumbani alikuta hali ya kawaida na yeye alijifanya hajui lolote. Baada ya mapumziko mafupi mkewe alimfuata alipokuwa amekaa kwenye kochi na kumpatia barua ya Jeska. Kabla ya kuipokea alihoji.
“Ya nini?”
“We, soma.”
Aliichukua ile barua na kuisoma kiuongo na ukweli kisha alishusha pumzi ndefu na kumtupia jicho mkewe aliyekuwa akimfuatilia muda wote aliokuwa alipokuwa akiisoma.
“Umeiona?” Mkewe alimuuliza.
“Nimeiona.”
“Una maoni gani?”
“Nani kaileta?”
“Yeye mwenyewe.”
“Alipoileta alisemaje?”
“Sikuonana naye ila alimpa mlinzi.”
“Nafikiri kuna kitu anakiamini, sidhani kuna umuhimu wa kumtafuta kwa vile amesema atarudi tumpe uhuru anaotaka. Nina imani sasa hivi Jeska ana miaka 19 ana maamuzi ambayo yanayokubalika hata kisheria.”
“Lakini bado ni mtoto aliye chini yetu.”
“Ni kweli, lakini mambo mengi amekuwa akituficha sisi walezi wake ambao tulimlea kama mtoto wetu wa kuzaa. Sidhani kama kuna siku ulimpa upendeleo Edna na kumtenga Jeska?”
“Sijawahi na wala sikuwahi kuwaza jambo hilo zaidi ya kufikiria siku moja Jeska ayazungumze mafanikio yake kupitia mikono yetu. Inaonesha jinsi gani Jeska kaumizwa na kubakwa kitendo ambacho kimechubua kovu la kufiwa na wazazi wake.”
“Sasa sisi tutafanya nini ikiwa yeye mwenyewe hataki kusema ukweli ili tumchukulie hatua aliyembaka. Lakini kwa vile amesema ipo siku atarudi na kuyasema yote tumpe muda.”
Baada ya makubaliano mzee Ezekiel aliaga na kuondoka, safari yake ilikuwa kwenda hotelini kwa Jeska akapange mikakati mingine baada ya kufanikiwa mpango wake wa awali wa kumtorosha Jeska. Alipofika hotelini alimkuta Jeska amejilaza akiwa hajui nini hatima ya maisha yake baada ya kukubali kuusaliti moyo wake kwa kuuficha ukweli.
Mzee Ezekiel alikumta amejilaza kitandani akiwa amejifunga taulo lililovuka magoti kidogo. Jicho lake lilitua kwenye maumbile ya mvuto ya Jeska. Alimeza funda la mate na kuingia ndani wakati huo Jeska alikuwa akijiweka vizuri.
“Karibu baba.”
“Asante.”
“Za huko?”
“Mmh nzuri, akili tuliyotumia itakufanya uishi bila wasiwasi.”
“Nitaishi vipi ina maana maisha yangu yote yatakuwa ya hotelini?”
“Hapana, kuna nyumba nimekutafutia nitakupangia nyumba nzima ambayo utaishi huko nitakutafutia mfanyakazi wa ndani. Nitakutoa siku moja moja sehemu za starehe zilizokuwa nje ya mji ili kuhakikisha unafurahia maisha.”
“Kama hivyo nitashukuru.”
“Nia yangu ni kurudisha furaha yako na kuondoa maumivu yote ya kubakwa, ichukulie kama ajali. Si hayo tu nina mpango wa kukujengea nyumba na kukufungulia miradi ili usiwe tegemezi. Leo nipo kesho sipo sitaki upate tabu.”
Huo ndiyo ukawa mwanzo wa Jeska kuishi mbali na familia iliyomlea huku mzee Ezekiel akiongeza mapenzi kwa Jeska ambaye bila kujielewa alikuwa amenaswa na mtego wa mzee Ezekiel na kumgeuza kuwa mpenzi wake.
Penzi lake na mzee Ezekiel lililipuka kama moto wa volkano, safari zote za ndani na nje ya nchi walikuwa pamoja, Jeska alizidi kupendeza toka umbile la kitoto na kuhamia katika umbile la mtu mzima lisilo tilia mashaka ukaribu wake na mzee Ezekiel watu waliwaona wapo sawa.
Jeska kwa muda mfupi alisahau maumivu yote ya kubakwa na mzee Ezekiel na kujikuta akifurahia penzi la mzee huyo na kutamani awe mke mdogo mwenye haki zote.
Mzee Ezekiel alimhakikishia kumuoa ndoa ya Bomani na kumpatia sehemu ya mirathi ya mali yake. Hatua ile ilimfurahisha sana Jeska na kuamini mwanzo wa maisha mapya ya kuweza kumiliki mali yake kutokana na uwezo mkubwa wa mzee Ezekiel.
Ukaribu wa mzee Ezekiel na Jeska ulianza kuyumbisha nyumba ya mzee Ezekiel kwa mapenzi yote kuhamishia kwa Jeska aliyefahamika kama mke wa pili wa mzee Ezekiel. Kutokana na tabia ya mke wa mzee Ezekiel mama Edna kutotembea mambo mengi ya nje hakuyajua.
Wakati mipango imekaribia na hatua zote muhumu za kufunga ndoa ya Bomani, siku moja baada ya kutoka kwa Jeska majira ya saa tano usiku mzee Ezekiel akiwa katika gari lake alipata ajali ya gari lake kugongwa sehemu ya mlango na kumsababishia maumivu makali sehemu za kifua na mbavu.
“Asante, lakini ndivyo hivyo mwisho wa mwaka siwezi kukaa hapa tena.”
“Unaishi na nani?”
“Nipo peke yangu na mfanyakazi wa ndani, kwa sasa nina pesa kidogo za matumizi zikiisha nitamlipa nini.
Na mwaka ukiisha nitalipa nini na nikifukuzwa nitakwenda wapi kama sio kuadhirika mtoto wa kike,” Jeska alijikuta akitoa siri yake yote bila kujua mtu aliye mbele yake ni wa aina gani kutokana na kupagawa kutokana na kifo cha mzee Ezekiel na maisha atakayoishi.
“Hapa mjini huna ndugu?”
“Wapo lakini ni wabaya wangu.”
“Kivipi?”
“Japo sikujui hunijui lakini msaada wako mkubwa unanifanya niwe muwazi kwako.”
“Ni kweli mimi ni mtu mwema pia naweza kuwa msaada mkubwa katika maisha yako.”
Jeska alijikuta akiitoa siri yake yote toka kifo cha familia yake mpaka alivyochukuliwa na familia ya mzee Ezekiel baba yake shogae kipenzi Edna. Lakini la mzee Ezekiel kumbaka alilificha, lakini kwa ajabu yule mgeni alimwambia.
“Mbona unaficha lingine.”
“Lipi hilo?”
“La kukubaka mzee Ezekiel na kukutorosha hospitali.”
“Mmh, umejuaje?” Jeska alishtuka.
“Namejua tu kwani lilikuwa siri.”
“Mbona unanitisha, hakuna anayejua zaidi yangu na dokta.”
“Sasa hapo siri ipo wapi, tuachane na hilo, mmhu”
“Hapana, inaonekana basi unajua mengi kuhusu mimi.”
“Sijui lolote, hebu endelea kunihadithia ili niweze kukusaidia.”
“Kama hivyo baada ya kubakwa na kufichwa huku lakini mkosi bado ulikuwa ukiniandama na kujikuta niliyemtegemea ndiyo hivyo amefariki.”
“Lakini si mlikuwa na mpango wa kuoana?”
“Eti?” Jeska alizidi kushtuka maneno ya mgeni wake kuonekana kujua mambo mengi ambayo yeye aliamini ni siri.
“Jamani kaka wewe ni nani unayejua mambo yangu mengi?”
“Sijui mengi ila hutaki kuwa mkweli na muwazi kwangu.”
“Kaka yangu mengine nayasahau kutokana na kuchanganyikiwa.”
“Basi nitakuwa nakusaidia, upo tayari nikusaidie?”
“Nipo tayari, japo maneno yako yananitia wasiwasi.”
“Sikiliza Jeska.”
“Ha! Kaka umejuaje jina langu?”
“Jeska hayo si muhimu zaidi la lililo mbele yako.”
“Sasa utanisaidia vipi?”
“Nataka mali zote zilizochukuliwa na wazazi wako zirudi kwako.”
“Kwangu! Wewe ni mwana sheria?”
“Ni mtu wa kawaida ila ninajua jinsi ya kukurudishia mali zako.”
“Utafanya nini?”
“Jeska, wewe shida yako mali zako au kujua zitarudi vipi?”
”Mmh, siamini naona sawa na kunipa matumaini lakini jambo hili siamini kama litawezekana ni muda mrefu sana hata hati zote wanazo wao.”
“Kazi hiyo niachie mimi, sawa.”
Baada ya kusema vile mgeni aliingiza mkono mfukoni na kumpatia noti mpya nne za elfu tano tano na kumueleza.
“Naomba hizi hela usizitumie leo kaziweke chini ya mto mpaka kesho kisha ruksa kuzitumia.”
“Asante,” Jeska alishukuru huku akipokea.
“Nilitaka kusahau na ukiamka asubuhi chukua zote usiache hata moja chini ya mto.”
“Hakuna tatizo.”
“Wacha nikuache niwahi kwenye shughuli zangu nikipata muda nitarudi usiku.”
“Kuja kulala?”
“Utakavyotaka wewe, au nisirudi?”
”Hapana njoo tu.”
“Basi wacha nikukimbie.”
“Ngoja nikaweke pesa zangu ndani,” Jeska alisema huku akinyanyuka kuelekea chumbani kwake.
Jeska alikwenda hadi chumbani na kuziweka pesa zake chini ya mto kisha alitoka sebuleni alipomuacha mgeni. Lakini sebule ilikuwa nyeupe mgeni hakuwepo, alipotoka nje pia hakumkuta pamoja na gari lake.
Itaendelea siku ya Jumanne hapa hapa.

Post a Comment