AHADI YA NDOTONI - 03
ILIPOISHIA
Baada ya kutolewa wasiwasi mama Edna na Edna walirudi nyumbani huku wakizidi kumuombea dua ili atoke salama. Njiani Edna tukio la Jeska lilimsukasuka moyoni kiasi cha kumfanya akose raha, maneno ya Jeska kukanusha ujauzito ule siyo wa konda ila ni wa mtu ambaye hakutaka kumtaja ulimsumbua sana.
Aliamua kumueleza mama yake maneno ya Jeska kuhusiana na ujauzito ule, baada ya kukaa kimya alimwita mama yake ambaye naye alikuwa katika dimbwi la mawazo.
“Mama.”
“Unasemaje Edna?”
“Unajua kuna vitu vinanichanganya.”
“Vitu gani?”
“Kuhusiana na ujauzito wa Jeska.”
“Kinakuchanganya nini?”
“Kuhusiana na mtu aliyempa ujauzito.”
“Sasa nini kinakuchanganya?”
“Usiri wa mtu aliyempa ujauzito na inaoneka haikuwa ridhaa yake.”
“Edna mbona mimi kaniambia kila kitu.”
“Si kweli mama alikudanganya.”
“Kanidanganya kipi?”
“Aliyempa mimba si konda?”
“Si konda! Kama si konda ni nani na kwa nini unasema si kwa ridhaa yake?”
“Mama Jeska anasiri nzito moyoni mwake, ameniambia kuwa ameamua kukudanganya kwa vile anakuheshimu sana.”
“Sasa kama ananiheshimu kwa nini anidanganye?”
“Alinieleza kuwa umdhaniaye ndiye kumbe siye.”
“Alikueleza maana ya usemi wake?”
“Alisema atanieleza siku moja kama kuna kitu kitashindikana na kama kikifanikiwa basi siri hiyo atakufa nayo moyoni mwake.”
“Mmh, mbona mnanitisha, unataka kuniambia kuna mtu aliyempa ujauzito hataki tumjue?”
“Ndiyo, inavyoonekana na kitu alichokipanga kukifanya ni kutoa ujauzito kama sikosei, kwa vile umetoka siri itabakia moyoni mwake.”
“Sasa unataka kuniambia ni nani aliyempa ujauzito kwa kukisia?”
“Mama, nimemuuliza maswali mengi ashakumu si matusi ilifikia hata kumuuliza ujauzito huo labda ni wa baba.”
“Alijibu nini?”
”Alikataa.”
‘Sasa mbona anatuchanganya?”
“Lakini mama naomba Jeska akitoka hospitali kaa naye na kumuuliza kwa kituo atakueleza siri iliyomoyoni mwake juu ya ujauzito kuna mengi inaonekana yamejificha.”
“Mmh, haya.”
Walipofika nyumbani walioga na kula chakula cha usiku ambacho hawakuwahi kula kutokana na taarifa ya kushtusha ya Jeska.
***
Jeska alizinduka hospitali majira ya saa saba usiku na kukupepesa macho yake, jicho lake lilitua kwenye chupa ya damu iliyokuwa imebakia robo kumalizika. Alivuta kumbukumbu na kukumbuka alikwenda kutoa mimba lakini tokea hapo hakukumbuka vizuri kama alitokewa na nini.
Alijiuliza pale ndipo hospitali aliyokwenda kutoa mimba au wapi, lakini taratibu alikumbuka kutokwa na damu nyingi wakati wa utoaji wa mimba kiasi cha kuhamishwa chumba kingine. Pia alikumbuka kama alipandishwa kwenye gari kwenda nyumbani lakini zaidi ya hapo hakukumbuka kitu chochote.
Mazingira ya hospitali yalimchanganya yalikuwa masafi tofauti na kule alipolazwa baada ya kutolewa mimba, kilikuwa chumba kama cha kawaida lakini pale palionekana hospitali ya ukweli. Akiwa katika kutafakari macho ametizama juu, daktari aliingia na kukuta Jeska karudiwa na fahamu. Alimsogelea hadi kitandani na kumsemesha.
“Jeska,” alimwita.
“Abee.”
“Pole sana.”
“Asante,” alijibu kwa sauti ya chini.
“Unajisikiaje?”
“Bado.”
“Tatizo bado nini?”
“Kizunguzungu na uchovu wa mwili.”
“Ooh, pole sana, mh, tatizo kubwa ni nini?”
Swali lilikuwa gumu kwa Jeska kusema kilichosababisha kufanya vile, alibakia bubu akikapua macho. Daktari aligundua uzito wa swali lake, alimuuliza kwa kulifumbua zaidi.
“Nini kilichosababisha utoe mimba ikiwa wazazi wako walikuwa tayari kuitunza hiyo?”
“Nimeamua kuitoa kwa vile nataka kusoma.”
“Kwani ungejifungua usingesoma?”
“Nina imani nisingesoma kwa vile nisingeweza kuwatumikia mabwana wawili mtoto na elimu.”
“Ungejua hivyo usingejiingiza katika mapenzi ukiwa mwanafunzi.”
“Najua utasema hivyo, si kila kosa likitokea linamhusu mtendaji.”
“Una maana gani?”
Saa kumi na mbili asubuhi Edna na mama yake walifika hospitali kumjulia hali Jeska, walipofika walikwenda wodini na kumkuta Jeska akiwa anaongezwa chupa ya damu nyingine.
Wakati wanaingia alikuwa amejipumzisha, bahati nzuri walikutana na daktari wa zamu.
“Vipi baba?”
“Aah, salama tu mama mgonjwa anaendelea vizuri, hata usiku alipozinduka nimezungumza naye mengi”
“Kuna mwanga wowote ulioupata?”
“Mmh, kwa kweli binti ni msiri sana, nimembembeleza na kunieleza atanieleza baadaye.”
“Mmh, mtoto huyu msiri sana.”
“Ni kweli inaonesha ana vitu vingi moyoni mwake vinavyomuumiza.”
“Sawa baba wacha na sisi tukajaribu labda tutaambulia.”
Waliagana na daktari aliyekuwa akielekea ofisini kwake kujiandaa kurudi nyumbani. Walipofika pembeni ya kitanda cha Jeska, kabla ya kumuamsha alifumbua macho mwenyewe.
“Jeska.”
“Abee mama, shikamoo.”
“Marahaba mwanangu unaendeleaje?”
“Mmh, sijambo kidogo.”
“Pole Jeska,” Edna alimsalimia.
“Asante Edna.”
“Mmh, mwanangu kwa nini siku hizi unanificha?” Mama Edna alimuuliza Jeska.
“Kukuficha lipi mama?”
“Eti mimba si ya konda wa daladala?”
Jeska hakujibu alinyamaza kimya kwa kuamini akikataa ataulizwa ni nani, lakini aliamua kujibu.
“Ndiyo mama.”
“Ya nani?”
“Japo najua nitaonekana sina adabu naomba kwa hili mzazi wangu niachie mwenyewe maadamu ujauzito umetoka.”
“Jeska mbona unatuzunguka, kwa nini usimseme ikiwezekana tumfungulie mashtaka.”
“Nakuombeni tuacheni na hilo.”
“Au baba yako?”
Kauli ile ilimshtua Jeska ambaye alikuwa bubu mara moja,
“Haiwezekani litokee tatizo zito kama hili ukae kimya kama ni baba yako sema na akirudi atanitambua.”
“Mama mbona hivyo umeambiwa ni baba?” Edna alimtetea baba yake.
“Mama mbona umekwenda mbali hivyo, baba afanye hivyo ili iwe nini?”
“Kwani si mwanaume, Jeska basi naomba umtaje la sivyo nitajua ni baba yako,” mama Edna alikuja juu.
“Nitamtaja ngoja nimalize matibabu utamjua tu.”
“Sawa, lakini lazima nimjue na pia nataka kumjua aliyekutoa ujauzito wako, tukiachia hali hii hata mwenzako Edna akipata atakimbilia huko. Hata wewe usingekutwa na balaa hili tusingejua.”
“Mama hebu niacheni nimalize matibabu nitawaeleza kila kitu bila kuwaficha.”
“Sawa.”
Baada ya makubaliano Jeska alipewa chai na kunywa kisha walimuacha na kurudi nyumbani. Siku ile ndiyo siku aliyokuwa akirudi Mzee Ezekiel baba yake Edna, baada ya kufika alielezewa yote kuhusiana na kilichomkuta Jeska.
“Mnasema ametoa mimba?”
“Ndiyo, na kazua mapya kuwa mwenye ujauzito ule si konda,” mama Edna alimwambia mumewe.
“Etii! Kamtaja nani?” aliuliza kwa mshtuko.”
“Amesema akimaliza matibabu ataweka kila kitu hadharani.”
“Mmh, sawa tutamsikiliza.”
Mzee Ezekiel baba Edna alipumua baada ya kusikia hakutajwa, lakini alipanga kabla familia yake haijakwenda hospitali mchana awahi kumuomba Jeska asimwambie mtu hata kwa kumuhamisha hospitali ili tu ibakie siri yao wawili.
Itaendelea wiki ijayo....
“Na ndugu zako wote?”
“Ni mimi peke yangu ndiye niliyebakia.”
“Ina maana wazazi wako hawana ndugu?”
“Heri ningekaa kwenye dimbwi la mamba wenye njaa kuliko hao ndugu wa baba, nina wasiwasi hata kifo cha wazazi wangu huenda wao wakahusika. Baada ya kifo cha wazazi wangu walinichukua lakini mwishoni walinifukuza kama mbwa na matokeo yake ni haya, kuna umuhimu wa kukatisha maisha yangu tabu hizi mpaka lini?”
Jeska alizungumza kwa uchungu mkubwa na kumfanya daktari amuonee huruma, lakini bado aliamini kuna kitu cha kumsaidia kutokana na matatizo yake.
“Jeska nina cha kukusaidia kwa matatizo yako yote?”
“Kivipi?”
“Kwanza kumtafuta aliyekubaka na pili kumjua aliyetaka kukutoa roho kwa kukutoa ujauzito ili sheria ichukue mkondo wake.”
Jeska hakujibu haraka kutafakari aliyosema daktari, kabla ya kumjibu swali lake alimuuliza:
“Samahani dokta.”
“Bila samahani.”
“Eti mama anajua kama nilikuwa natoa mimba?”
“Ndiyo.”
“Alisemaje?”
“Alilalamika kwa uamuzi wako wakati waliisha kueleza usiitoe.”
“Mh!” Jeska aliguna na kuendelea kutafakari swali la daktari kumtaja aliyempa ujauzito.
Aliamini siri yake ni nguzo ya ndoa ya wazazi wa Edna na kuhusu kumtaja aliyemtoa ujauzito vile vile angekuwa amewaharibia wenzake ambao walitumia hospitali ile kutoa ujauzito kama yeye angeitaja na kukamatwa kwa muhusika lazima shoga zake watamuona hana maana hata kumtenga.
Aliamini bado siri yake ni muhimu kwa jambo lile la kutoitaja hospitali aliyotumia kutoa ujauzito. Baada ya ukimya wa muda Jeska alisema:
“Dakta najua unania nzuri na matatizo yangu, lakini mwenye utatuzi wa yaliyo mbele yangu ni yule aliye sababisha yote haya.”
“Hapana Jeska, najua pengine una hofu kuwataja watu hao lakini nakuahidi kukulinda kwa kila kitu ambacho kitajitokeza hata kukuwekea wakili katika matatizo yako ikiwemo ya kudhulumiwa mali uliyoachiwa na wazazi wako.”
“Nashukuru, nipe muda nitakueleza kila kitu.”
“Leo huwezi?”
“Nimekueleza nitakueleza kila kitu naomba unielewe.”
“Vizuri, basi kuna chakula unatakiwa kula.”
“Siwezi niache nilale sijisikii labda asubuhi.”
“Ngoja nikudunge sindano ili upunguze maumivu.”
Daktari alimdunga sindano kisha alimwacha Jeska apumzike kwa vile usiku ulikuwa mkubwa. Baada ya daktari kuondoka hakuchukua muda mrefu naye usingizi ulimpitia.
Daktari alijifanya kushangaa na kuwaita wauguzi kuwaulizia mgonjwa.
“Eti jamani, mgonjwa mmemuona wapi?”
“Mmh, si asubuhi alikuwemo ndani?” Muuguzi mmoja alisema.
“Kwani hamkumkuta?”Mwingine aliuliza.
“Sasa tungemkuta tungemuuliza?” Mama Edna alimjibu kwa hasira.
“Mmh, kwa kweli hatujui.”
“Au amerudi nyumbani mwenyewe.”
Wakati wakishauriana kupotea kwa Jeska, mara aliingia mzee Ezekiel baba yake Edna, wote waligeuka kumtazama.
“Karibu mzee,” daktari alimkaribisha mzee Ezekiel kama hamfahamu.
“Asante.”
“Nikusaidie nini?”
“Hapana huyu ni mume wangu,” mama Edna aliingilia kati.
“Ooh, mzee karibu sana.”
“Asante, vipi naona kuna nyuso sizifahamu, kuna usalama?”
“Usalama upo, ila kuna tatizo moja mgonjwa haonekani kwenye wodi yake.”
“Mmemtafuta nje ya wodi?”
“Bado.”
“Sasa unangoja nini, mtafuteni nje ya wodi mkimkosa ndipo mjadiliane.”
Walikubaliana kumtafuta nje wa wodi kwa kutumwa wauguzi kuranda kila kona ya hospitali kumtafuta mgonjwa lakini hakuna aliyemuona. Mzee Ezekiel alishauri warudi nyumbani huenda amerudi mwewnyewe. Wote walirudi nyumbani kumuangalia Jeska kama kweli amerudi nyumbani, huku siri kubwa ikibaki moyoni kwa mzee Ezekiel.
Walipofika nyumbani hawakumkuta mtu, walikubaliana wasubiri atakuwa amekwenda wapi na kama mpaka siku ya pili hajaonekana walikubaliana wapeleke taarifa polisi. Mzee Ezekiel alimweleza mkewe mambo yote kuhusu Jeska atayashughulikia yeye.
Edna aliamini kabisa chanzo cha Jeska kutoroka ni mama yake, hakuacha kumlaumu mama yake.
“Mama unaona ukali wako ndiyo kila siku unamchanganya da Jeska, sasa unaona kaamua kutoroka?” Edina alimwambia mama yake.
“Sasa atakuwa mtoto wa jicho asiyekanywa akikosea.”
“Lazima mama uangalie yule yupo vipi, hana wazazi lolote utakalo mkalipia atajua humpendi.”
“Ningekuwa simpendi ningemlea muda wote huu.”
“Lakini kataa kubali kutoroka kwa Jeska ni kutokana na kauli zako kali za vitisho.”
“Aah, Mungu ndiye anajua kama nilikuwa simpendi, kipi alichotaka nisimpe nilimfanya kama mwanangu wa kuzaa ndiyo maana hata kumkanya nimemkanya kama ambavyo ningekukanya wewe.”
“Sasa atakuwa amekwenda wapi?”
“Tutajuaje mimi na wewe hatujui.”
“Asiwe ameamua kujiua!”
“Mungu apishe mbali, siamini kama uamuzi kama huo ndiyo suluhu ya maisha yake.”
“Mama Jeska huamini kabisa ni kiumbe kilichoumbwa kwa mikosi toka kifo cha familia yake, tuliweza kumpunguzia maumivu ya msiba ule mzito na kumfanya asahau. Lakini hili la mimba limemuumiza sana, kuna siri nzito moyoni mwake ambayo sijui kwa nini hakutaka kuitoa.”
Wakiwa katikati ya mazungumzo mlinzi wa getini aliingia na barua mkononi.
“Karibu Musa naona una barua.”
“Ndiyo mama.”
“Nani amekupa?”
“Kanipa Jeska.”
“Jeska! Jeska yupi?”
“Si dada Jeska.”
“Huyu Jeska wa kwetu?”
“Ndiyo.”
“Wa humu ndani?”
“Ndiyo mama.”
“Yupo wapi?”
“Alikuja na teksi hadi getini dereva alipiga honi kuashiria ananiita, nilikwenda hadi kwenye gari na kumkuta dada Jeska ambaye alinisabahi kisha alinipa barua hii nikuleteeni kisha gari liliondoka.”
“Alikuambia anakwenda wapi?”
“Hakuniambia”
“Afya yake?”
“Ipo sawa.”
Unaikumbuka namba ya ile teksi?”
“Kwa kweli sikuitilia maanani.”
“Mmh, sawa kaendelee na kazi.”
Waliipokea ile barua na kuifungua kuangalia ndani kuna kitu gani, baada ya kuifungua walikutana na ujumbe ambao ulionesha kweli umeandikwa na Jeska kutokana na kuufahamu vyema mwandiko wake. Barua ilikuwa imeandikwa hivi:
Kwenu wazazi wangu, shikamooni.
Napenda kuandika waraka huu kuwatoeni wasiwasi kwa kutoweka kwangu ghafla, lakini napenda kuwatoa wasiwasi wazazi wangu pamoja na dada yangu kipenzi Edna. Najua kitendo nilichokitenda kitaonekana ni utovu wa nidhamu lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kufanya niliyoyafanya.
Kupewa ujauzito kwa kubakwa kwa kweli kuliniumiza sana kiasi cha kujikuta kiumbe nisiyetakiwa duniani. Lakini ninyi wazazi wangu pamoja na ndugu yangu kipenzi Jeska umeweza kunipa moyo na kufuta dhana mbaya moyoni mwangu ya kukatisha maisha yangu.
Nina mengi ya kuzungumza na ninyi wazazi wangu baba mama na Edna juu ya nini kilinikuta, sikutaka kulitamka hili mapema kwa vile lingeniongezea maumivu moyoni mwangu. Naamini kabisa hakuna hata mmoja angekubali kusubiri kuwaeleza kitu ambacho alikuwa na shauku kukijua.
Nimeamua kuondoka hapo nyumbani ili nipate muda wa kupumzisha maumivu makali ya moyo wangu, baada ya kuupumzisha moyo wangu nitarudi nyumbani, nakuombeni mnipokee japo mimi ni mwana mkosefu pengine kuonekana asiye na shukurani.
Ila siku ilifika kila kitu kitakuwa wazi na mtanielewa zaidi pengine kunionea huruma zaidi kama milivyonionea huruma na kunitunza mpaka leo hii. Sitaki kuwachosha kwa maneno mengi, nilitaka kuwatoa hofu tu msinitafute nipo katika mikono salama na baada ya muda nitarudi nyumbani ni mimi mwanenu Jeska.
Baada ya kuisoma alimpa Edna naye aisome kutokana na kuwa na shauku kutaka kujua kwenye karatasi ile kumeandikwa nini. Edna naye alisoma kimya kimya ile barua kisha alinyanyua macho kumtazama mama yake aliyekuwa akimfuatilia alipokuwa akisoma.
“Mama hii barua umeielewa?”
“Kilichoandikwa si umekisoma?”
“Ndiyo.”
“Basi lazima tuielewe.”
“Sina maana hiyo”
“Una maana gani?”
“Mama kuna fumbo zito ambalo Jeska kalificha, mmh kubakwa...na nani?”
“Tutajuaje naye amefanya siri.”
“Lakini mama ulitakiwa kumuelewa Jeska kuliko kumkaripia.”
“Edna usitake kuniudhi, kwani angenieleza haya aliyoandika kwenye barua nisingemuelewa?”
“Asingeweza kutokana na kauli yako ya ukali, Jeska anaamini toka apatwe na tatizo umemtenga.”
“Nimemtenga kivipi Edna? Mbona unanitia lawama zisizo na msingi.”
“Kweli mama umekuwa mkali kauli zako hata mimi nilijisikia vibaya, ni kweli Jeska alikuwa amefanya kosa hatukutakiwa kutumia vitisho aseme nani aliyempa ujauzito. Lazima angesema tu kama alivyosema alichanganywa na kitendo cha kubakwa, hata ningefanyiwa mimi ningeumia.”
“Sasa atakuwa wapi?”
“Ni vigumu kujua la muhimu tumsubiri baba arudi atatusaidia akiisoma hii barua.”
Itaendelea wiki ijayo Jumatatu.
Like: www.facebook.com/2jiachie
Web: www.2jiachie.com
Baada ya kutolewa wasiwasi mama Edna na Edna walirudi nyumbani huku wakizidi kumuombea dua ili atoke salama. Njiani Edna tukio la Jeska lilimsukasuka moyoni kiasi cha kumfanya akose raha, maneno ya Jeska kukanusha ujauzito ule siyo wa konda ila ni wa mtu ambaye hakutaka kumtaja ulimsumbua sana.
Aliamua kumueleza mama yake maneno ya Jeska kuhusiana na ujauzito ule, baada ya kukaa kimya alimwita mama yake ambaye naye alikuwa katika dimbwi la mawazo.
“Mama.”
“Unasemaje Edna?”
“Unajua kuna vitu vinanichanganya.”
“Vitu gani?”
“Kuhusiana na ujauzito wa Jeska.”
“Kinakuchanganya nini?”
“Kuhusiana na mtu aliyempa ujauzito.”
“Sasa nini kinakuchanganya?”
“Usiri wa mtu aliyempa ujauzito na inaoneka haikuwa ridhaa yake.”
“Edna mbona mimi kaniambia kila kitu.”
“Si kweli mama alikudanganya.”
“Kanidanganya kipi?”
“Aliyempa mimba si konda?”
“Si konda! Kama si konda ni nani na kwa nini unasema si kwa ridhaa yake?”
“Mama Jeska anasiri nzito moyoni mwake, ameniambia kuwa ameamua kukudanganya kwa vile anakuheshimu sana.”
“Sasa kama ananiheshimu kwa nini anidanganye?”
“Alinieleza kuwa umdhaniaye ndiye kumbe siye.”
“Alikueleza maana ya usemi wake?”
“Alisema atanieleza siku moja kama kuna kitu kitashindikana na kama kikifanikiwa basi siri hiyo atakufa nayo moyoni mwake.”
“Mmh, mbona mnanitisha, unataka kuniambia kuna mtu aliyempa ujauzito hataki tumjue?”
“Ndiyo, inavyoonekana na kitu alichokipanga kukifanya ni kutoa ujauzito kama sikosei, kwa vile umetoka siri itabakia moyoni mwake.”
“Sasa unataka kuniambia ni nani aliyempa ujauzito kwa kukisia?”
“Mama, nimemuuliza maswali mengi ashakumu si matusi ilifikia hata kumuuliza ujauzito huo labda ni wa baba.”
“Alijibu nini?”
”Alikataa.”
‘Sasa mbona anatuchanganya?”
“Lakini mama naomba Jeska akitoka hospitali kaa naye na kumuuliza kwa kituo atakueleza siri iliyomoyoni mwake juu ya ujauzito kuna mengi inaonekana yamejificha.”
“Mmh, haya.”
Walipofika nyumbani walioga na kula chakula cha usiku ambacho hawakuwahi kula kutokana na taarifa ya kushtusha ya Jeska.
***
Jeska alizinduka hospitali majira ya saa saba usiku na kukupepesa macho yake, jicho lake lilitua kwenye chupa ya damu iliyokuwa imebakia robo kumalizika. Alivuta kumbukumbu na kukumbuka alikwenda kutoa mimba lakini tokea hapo hakukumbuka vizuri kama alitokewa na nini.
Alijiuliza pale ndipo hospitali aliyokwenda kutoa mimba au wapi, lakini taratibu alikumbuka kutokwa na damu nyingi wakati wa utoaji wa mimba kiasi cha kuhamishwa chumba kingine. Pia alikumbuka kama alipandishwa kwenye gari kwenda nyumbani lakini zaidi ya hapo hakukumbuka kitu chochote.
Mazingira ya hospitali yalimchanganya yalikuwa masafi tofauti na kule alipolazwa baada ya kutolewa mimba, kilikuwa chumba kama cha kawaida lakini pale palionekana hospitali ya ukweli. Akiwa katika kutafakari macho ametizama juu, daktari aliingia na kukuta Jeska karudiwa na fahamu. Alimsogelea hadi kitandani na kumsemesha.
“Jeska,” alimwita.
“Abee.”
“Pole sana.”
“Asante,” alijibu kwa sauti ya chini.
“Unajisikiaje?”
“Bado.”
“Tatizo bado nini?”
“Kizunguzungu na uchovu wa mwili.”
“Ooh, pole sana, mh, tatizo kubwa ni nini?”
Swali lilikuwa gumu kwa Jeska kusema kilichosababisha kufanya vile, alibakia bubu akikapua macho. Daktari aligundua uzito wa swali lake, alimuuliza kwa kulifumbua zaidi.
“Nini kilichosababisha utoe mimba ikiwa wazazi wako walikuwa tayari kuitunza hiyo?”
“Nimeamua kuitoa kwa vile nataka kusoma.”
“Kwani ungejifungua usingesoma?”
“Nina imani nisingesoma kwa vile nisingeweza kuwatumikia mabwana wawili mtoto na elimu.”
“Ungejua hivyo usingejiingiza katika mapenzi ukiwa mwanafunzi.”
“Najua utasema hivyo, si kila kosa likitokea linamhusu mtendaji.”
“Una maana gani?”
Saa kumi na mbili asubuhi Edna na mama yake walifika hospitali kumjulia hali Jeska, walipofika walikwenda wodini na kumkuta Jeska akiwa anaongezwa chupa ya damu nyingine.
Wakati wanaingia alikuwa amejipumzisha, bahati nzuri walikutana na daktari wa zamu.
“Vipi baba?”
“Aah, salama tu mama mgonjwa anaendelea vizuri, hata usiku alipozinduka nimezungumza naye mengi”
“Kuna mwanga wowote ulioupata?”
“Mmh, kwa kweli binti ni msiri sana, nimembembeleza na kunieleza atanieleza baadaye.”
“Mmh, mtoto huyu msiri sana.”
“Ni kweli inaonesha ana vitu vingi moyoni mwake vinavyomuumiza.”
“Sawa baba wacha na sisi tukajaribu labda tutaambulia.”
Waliagana na daktari aliyekuwa akielekea ofisini kwake kujiandaa kurudi nyumbani. Walipofika pembeni ya kitanda cha Jeska, kabla ya kumuamsha alifumbua macho mwenyewe.
“Jeska.”
“Abee mama, shikamoo.”
“Marahaba mwanangu unaendeleaje?”
“Mmh, sijambo kidogo.”
“Pole Jeska,” Edna alimsalimia.
“Asante Edna.”
“Mmh, mwanangu kwa nini siku hizi unanificha?” Mama Edna alimuuliza Jeska.
“Kukuficha lipi mama?”
“Eti mimba si ya konda wa daladala?”
Jeska hakujibu alinyamaza kimya kwa kuamini akikataa ataulizwa ni nani, lakini aliamua kujibu.
“Ndiyo mama.”
“Ya nani?”
“Japo najua nitaonekana sina adabu naomba kwa hili mzazi wangu niachie mwenyewe maadamu ujauzito umetoka.”
“Jeska mbona unatuzunguka, kwa nini usimseme ikiwezekana tumfungulie mashtaka.”
“Nakuombeni tuacheni na hilo.”
“Au baba yako?”
Kauli ile ilimshtua Jeska ambaye alikuwa bubu mara moja,
“Haiwezekani litokee tatizo zito kama hili ukae kimya kama ni baba yako sema na akirudi atanitambua.”
“Mama mbona hivyo umeambiwa ni baba?” Edna alimtetea baba yake.
“Mama mbona umekwenda mbali hivyo, baba afanye hivyo ili iwe nini?”
“Kwani si mwanaume, Jeska basi naomba umtaje la sivyo nitajua ni baba yako,” mama Edna alikuja juu.
“Nitamtaja ngoja nimalize matibabu utamjua tu.”
“Sawa, lakini lazima nimjue na pia nataka kumjua aliyekutoa ujauzito wako, tukiachia hali hii hata mwenzako Edna akipata atakimbilia huko. Hata wewe usingekutwa na balaa hili tusingejua.”
“Mama hebu niacheni nimalize matibabu nitawaeleza kila kitu bila kuwaficha.”
“Sawa.”
Baada ya makubaliano Jeska alipewa chai na kunywa kisha walimuacha na kurudi nyumbani. Siku ile ndiyo siku aliyokuwa akirudi Mzee Ezekiel baba yake Edna, baada ya kufika alielezewa yote kuhusiana na kilichomkuta Jeska.
“Mnasema ametoa mimba?”
“Ndiyo, na kazua mapya kuwa mwenye ujauzito ule si konda,” mama Edna alimwambia mumewe.
“Etii! Kamtaja nani?” aliuliza kwa mshtuko.”
“Amesema akimaliza matibabu ataweka kila kitu hadharani.”
“Mmh, sawa tutamsikiliza.”
Mzee Ezekiel baba Edna alipumua baada ya kusikia hakutajwa, lakini alipanga kabla familia yake haijakwenda hospitali mchana awahi kumuomba Jeska asimwambie mtu hata kwa kumuhamisha hospitali ili tu ibakie siri yao wawili.
Itaendelea wiki ijayo....
“Na ndugu zako wote?”
“Ni mimi peke yangu ndiye niliyebakia.”
“Ina maana wazazi wako hawana ndugu?”
“Heri ningekaa kwenye dimbwi la mamba wenye njaa kuliko hao ndugu wa baba, nina wasiwasi hata kifo cha wazazi wangu huenda wao wakahusika. Baada ya kifo cha wazazi wangu walinichukua lakini mwishoni walinifukuza kama mbwa na matokeo yake ni haya, kuna umuhimu wa kukatisha maisha yangu tabu hizi mpaka lini?”
Jeska alizungumza kwa uchungu mkubwa na kumfanya daktari amuonee huruma, lakini bado aliamini kuna kitu cha kumsaidia kutokana na matatizo yake.
“Jeska nina cha kukusaidia kwa matatizo yako yote?”
“Kivipi?”
“Kwanza kumtafuta aliyekubaka na pili kumjua aliyetaka kukutoa roho kwa kukutoa ujauzito ili sheria ichukue mkondo wake.”
Jeska hakujibu haraka kutafakari aliyosema daktari, kabla ya kumjibu swali lake alimuuliza:
“Samahani dokta.”
“Bila samahani.”
“Eti mama anajua kama nilikuwa natoa mimba?”
“Ndiyo.”
“Alisemaje?”
“Alilalamika kwa uamuzi wako wakati waliisha kueleza usiitoe.”
“Mh!” Jeska aliguna na kuendelea kutafakari swali la daktari kumtaja aliyempa ujauzito.
Aliamini siri yake ni nguzo ya ndoa ya wazazi wa Edna na kuhusu kumtaja aliyemtoa ujauzito vile vile angekuwa amewaharibia wenzake ambao walitumia hospitali ile kutoa ujauzito kama yeye angeitaja na kukamatwa kwa muhusika lazima shoga zake watamuona hana maana hata kumtenga.
Aliamini bado siri yake ni muhimu kwa jambo lile la kutoitaja hospitali aliyotumia kutoa ujauzito. Baada ya ukimya wa muda Jeska alisema:
“Dakta najua unania nzuri na matatizo yangu, lakini mwenye utatuzi wa yaliyo mbele yangu ni yule aliye sababisha yote haya.”
“Hapana Jeska, najua pengine una hofu kuwataja watu hao lakini nakuahidi kukulinda kwa kila kitu ambacho kitajitokeza hata kukuwekea wakili katika matatizo yako ikiwemo ya kudhulumiwa mali uliyoachiwa na wazazi wako.”
“Nashukuru, nipe muda nitakueleza kila kitu.”
“Leo huwezi?”
“Nimekueleza nitakueleza kila kitu naomba unielewe.”
“Vizuri, basi kuna chakula unatakiwa kula.”
“Siwezi niache nilale sijisikii labda asubuhi.”
“Ngoja nikudunge sindano ili upunguze maumivu.”
Daktari alimdunga sindano kisha alimwacha Jeska apumzike kwa vile usiku ulikuwa mkubwa. Baada ya daktari kuondoka hakuchukua muda mrefu naye usingizi ulimpitia.
Daktari alijifanya kushangaa na kuwaita wauguzi kuwaulizia mgonjwa.
“Eti jamani, mgonjwa mmemuona wapi?”
“Mmh, si asubuhi alikuwemo ndani?” Muuguzi mmoja alisema.
“Kwani hamkumkuta?”Mwingine aliuliza.
“Sasa tungemkuta tungemuuliza?” Mama Edna alimjibu kwa hasira.
“Mmh, kwa kweli hatujui.”
“Au amerudi nyumbani mwenyewe.”
Wakati wakishauriana kupotea kwa Jeska, mara aliingia mzee Ezekiel baba yake Edna, wote waligeuka kumtazama.
“Karibu mzee,” daktari alimkaribisha mzee Ezekiel kama hamfahamu.
“Asante.”
“Nikusaidie nini?”
“Hapana huyu ni mume wangu,” mama Edna aliingilia kati.
“Ooh, mzee karibu sana.”
“Asante, vipi naona kuna nyuso sizifahamu, kuna usalama?”
“Usalama upo, ila kuna tatizo moja mgonjwa haonekani kwenye wodi yake.”
“Mmemtafuta nje ya wodi?”
“Bado.”
“Sasa unangoja nini, mtafuteni nje ya wodi mkimkosa ndipo mjadiliane.”
Walikubaliana kumtafuta nje wa wodi kwa kutumwa wauguzi kuranda kila kona ya hospitali kumtafuta mgonjwa lakini hakuna aliyemuona. Mzee Ezekiel alishauri warudi nyumbani huenda amerudi mwewnyewe. Wote walirudi nyumbani kumuangalia Jeska kama kweli amerudi nyumbani, huku siri kubwa ikibaki moyoni kwa mzee Ezekiel.
Walipofika nyumbani hawakumkuta mtu, walikubaliana wasubiri atakuwa amekwenda wapi na kama mpaka siku ya pili hajaonekana walikubaliana wapeleke taarifa polisi. Mzee Ezekiel alimweleza mkewe mambo yote kuhusu Jeska atayashughulikia yeye.
Edna aliamini kabisa chanzo cha Jeska kutoroka ni mama yake, hakuacha kumlaumu mama yake.
“Mama unaona ukali wako ndiyo kila siku unamchanganya da Jeska, sasa unaona kaamua kutoroka?” Edina alimwambia mama yake.
“Sasa atakuwa mtoto wa jicho asiyekanywa akikosea.”
“Lazima mama uangalie yule yupo vipi, hana wazazi lolote utakalo mkalipia atajua humpendi.”
“Ningekuwa simpendi ningemlea muda wote huu.”
“Lakini kataa kubali kutoroka kwa Jeska ni kutokana na kauli zako kali za vitisho.”
“Aah, Mungu ndiye anajua kama nilikuwa simpendi, kipi alichotaka nisimpe nilimfanya kama mwanangu wa kuzaa ndiyo maana hata kumkanya nimemkanya kama ambavyo ningekukanya wewe.”
“Sasa atakuwa amekwenda wapi?”
“Tutajuaje mimi na wewe hatujui.”
“Asiwe ameamua kujiua!”
“Mungu apishe mbali, siamini kama uamuzi kama huo ndiyo suluhu ya maisha yake.”
“Mama Jeska huamini kabisa ni kiumbe kilichoumbwa kwa mikosi toka kifo cha familia yake, tuliweza kumpunguzia maumivu ya msiba ule mzito na kumfanya asahau. Lakini hili la mimba limemuumiza sana, kuna siri nzito moyoni mwake ambayo sijui kwa nini hakutaka kuitoa.”
Wakiwa katikati ya mazungumzo mlinzi wa getini aliingia na barua mkononi.
“Karibu Musa naona una barua.”
“Ndiyo mama.”
“Nani amekupa?”
“Kanipa Jeska.”
“Jeska! Jeska yupi?”
“Si dada Jeska.”
“Huyu Jeska wa kwetu?”
“Ndiyo.”
“Wa humu ndani?”
“Ndiyo mama.”
“Yupo wapi?”
“Alikuja na teksi hadi getini dereva alipiga honi kuashiria ananiita, nilikwenda hadi kwenye gari na kumkuta dada Jeska ambaye alinisabahi kisha alinipa barua hii nikuleteeni kisha gari liliondoka.”
“Alikuambia anakwenda wapi?”
“Hakuniambia”
“Afya yake?”
“Ipo sawa.”
Unaikumbuka namba ya ile teksi?”
“Kwa kweli sikuitilia maanani.”
“Mmh, sawa kaendelee na kazi.”
Waliipokea ile barua na kuifungua kuangalia ndani kuna kitu gani, baada ya kuifungua walikutana na ujumbe ambao ulionesha kweli umeandikwa na Jeska kutokana na kuufahamu vyema mwandiko wake. Barua ilikuwa imeandikwa hivi:
Kwenu wazazi wangu, shikamooni.
Napenda kuandika waraka huu kuwatoeni wasiwasi kwa kutoweka kwangu ghafla, lakini napenda kuwatoa wasiwasi wazazi wangu pamoja na dada yangu kipenzi Edna. Najua kitendo nilichokitenda kitaonekana ni utovu wa nidhamu lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kufanya niliyoyafanya.
Kupewa ujauzito kwa kubakwa kwa kweli kuliniumiza sana kiasi cha kujikuta kiumbe nisiyetakiwa duniani. Lakini ninyi wazazi wangu pamoja na ndugu yangu kipenzi Jeska umeweza kunipa moyo na kufuta dhana mbaya moyoni mwangu ya kukatisha maisha yangu.
Nina mengi ya kuzungumza na ninyi wazazi wangu baba mama na Edna juu ya nini kilinikuta, sikutaka kulitamka hili mapema kwa vile lingeniongezea maumivu moyoni mwangu. Naamini kabisa hakuna hata mmoja angekubali kusubiri kuwaeleza kitu ambacho alikuwa na shauku kukijua.
Nimeamua kuondoka hapo nyumbani ili nipate muda wa kupumzisha maumivu makali ya moyo wangu, baada ya kuupumzisha moyo wangu nitarudi nyumbani, nakuombeni mnipokee japo mimi ni mwana mkosefu pengine kuonekana asiye na shukurani.
Ila siku ilifika kila kitu kitakuwa wazi na mtanielewa zaidi pengine kunionea huruma zaidi kama milivyonionea huruma na kunitunza mpaka leo hii. Sitaki kuwachosha kwa maneno mengi, nilitaka kuwatoa hofu tu msinitafute nipo katika mikono salama na baada ya muda nitarudi nyumbani ni mimi mwanenu Jeska.
Baada ya kuisoma alimpa Edna naye aisome kutokana na kuwa na shauku kutaka kujua kwenye karatasi ile kumeandikwa nini. Edna naye alisoma kimya kimya ile barua kisha alinyanyua macho kumtazama mama yake aliyekuwa akimfuatilia alipokuwa akisoma.
“Mama hii barua umeielewa?”
“Kilichoandikwa si umekisoma?”
“Ndiyo.”
“Basi lazima tuielewe.”
“Sina maana hiyo”
“Una maana gani?”
“Mama kuna fumbo zito ambalo Jeska kalificha, mmh kubakwa...na nani?”
“Tutajuaje naye amefanya siri.”
“Lakini mama ulitakiwa kumuelewa Jeska kuliko kumkaripia.”
“Edna usitake kuniudhi, kwani angenieleza haya aliyoandika kwenye barua nisingemuelewa?”
“Asingeweza kutokana na kauli yako ya ukali, Jeska anaamini toka apatwe na tatizo umemtenga.”
“Nimemtenga kivipi Edna? Mbona unanitia lawama zisizo na msingi.”
“Kweli mama umekuwa mkali kauli zako hata mimi nilijisikia vibaya, ni kweli Jeska alikuwa amefanya kosa hatukutakiwa kutumia vitisho aseme nani aliyempa ujauzito. Lazima angesema tu kama alivyosema alichanganywa na kitendo cha kubakwa, hata ningefanyiwa mimi ningeumia.”
“Sasa atakuwa wapi?”
“Ni vigumu kujua la muhimu tumsubiri baba arudi atatusaidia akiisoma hii barua.”
Itaendelea wiki ijayo Jumatatu.
Like: www.facebook.com/2jiachie
Web: www.2jiachie.com

Post a Comment