ad

ad

USIKU WA KIGODORO - 12


Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

ILIPOISHIA: Lina akiwa na mumewe, Semi alipata mshtuko mkubwa sana kuona simu ya James, akakumbuka kwamba alimwambia atafika Dar saa nane.
Kwa upande wake James, alishangaa kupiga simu ya Lina mara tatu bila kupokelewa. Mara, akaliona basi la Burudani likiingia, akalifuata. 
SASA ENDELEA…
“Jamani wazima?” aliwasalimia wafanyakazi wa basi hilo.
“Hili gari linatokea Korogwe?” aliuliza mara baada ya salamu yake kujibiwa.
“Ndiyo mkubwa.”
Alipopata jibu hilo, alisimama kando na kusubiri abiria washuke akiamini Lina yuko ndani. Lakini aliendelea kupiga simu yake ambayo haikupokelewa.
Mpaka abiria wa mwisho anashuka na begi, hakuwepo Lina!
“Mh! Hii kali! Anamaanisha nini sasa kutokupokea simu yangu? Angepokea aniambie kuna nini! Basi la Burudani ndiyo hili na hayumo!” alisema mwenyewe akiwa anaelekea kwenye gari lake.
Alipata wazo la kwenda Mlimani City kupumzika akipata kinywaji baridi na moyoni aliamua kwamba Lina akimpigia na yeye hatapokea ili kulipa kisasi.
Aliingia Mlimani City kwa kutumia geti la kaskazini, akaegesha gari sambamba na gari la Semi. Alishuka akaingia kwenye maduka ya ndani kwanza kwa ajili ya kuosha macho.
***
Lina alisimama kwenda chooni, Kindaundau naye alikuwa anaingia Mlimani City kwa teksi huku akimpigia simu Semi kumuuliza alikokaa.
“Nimekaa jirani na meza ya Samakisamaki, we uko wapi?” aliuliza Semi…
“Ndiyo napita getini…hebu ngoja nipokee simu ya shemeji yako kwanza,” alisema Kindaundau.
Simu hiyo iliyopigwa na mke wa Kindaundau ilikuwa ikimjulisha kwamba, mtoto ameumia mguu alikuwa akicheza na wenzake. Kindaundau alimwamuru dereva wa teksi kugeuza gari kuwahi nyumbani kwake, Makumbusho huku akimpigia simu Semi…
“Ee bwana, mtoto wangu kaumia, wife amenipigia sasa hivi, ngoja niwahi nimkimbize hospitali,” alisema Kindaundau…
“Da! Pole sana bwana. Basi utaniambia maendeleo huko.”
“Sawa.”
***
Inaweza kuwa ni ajabu lakini kweli, James alikatiza meza na kwenda kukaa meza moja na Semi maana watu walikuwa wengi siku hiyo hivyo nafasi ya kukaa ilikuwa ya kutafuta sana…
“Habari yako ndugu?” James alimsalimia Semi huku akimuuliza kama kwenye kiti alishokishika kina mtu…
“Njema tu kaka, karibu, hakina mtu. Ila hiki hapa kina mtu,” alisema Semi huku akikishika kiti cha Lina.
Lina alitoka chooni huku akijiwekaweka sawa nywele zake. Macho yake yalikuwa kwa wateja mbalimbali waliokuwepo eneo hilo. Hakuwa na habari ya kuangalia alipokaa mume wake na sasa waume zake.
Alikuwa amebakiza hatua chache kufika kwenye meza, alipotupa macho alipata mshtuko kumwona James amekaa na mume wake, akarudi chooni mbio. Baadhi ya watu waliomuona akirudi walimshangaa.
“Mungu wangu! Kwani wanafahamiana? Loo! Nimekwisha mimi Lina, kiranga chote leo ndiyo mwisho,” alisema peke yake kule chooni huku akijishika kifuani. Mapigo ya moyo yalimwenda kwa kasi ya ajabu.
Alikumbuka kitu, alichukua simu yake, akatuma meseji kwa James…
“Nililala baby, uko wapi? Si ndiyo tunaingia stendi Ubungo sasa. Please usiondoke nina mizigo.”
James alisoma meseji hiyo, akasimama haraka sana…
“Ee bwana, ngoja niwahi stendi kuna mgeni ameingia hapo,” alimwambia Semi huku akitoa noti ya shilingi elfu tano na kumpa Semi…
“Hii utanilipia hii juisi na mayai.”
“Poapoa mkubwa,” alijibu Semi bila kujua mchezo wote unachezwa na mke wake.
James alikimbilia kwenye gari huku akipiga simu kwa Lina…
“Haloo, sasa umekuja na basi gani?”
“Burudani, si nilikwambia.”
“Mbona basi la Burudani limefika, wewe sijakuona?”
“Burudani la pili..”
“Poapoa, nakuja.”
Lina alihema kwa kuhisi unafuu. Lakini alijua ana kibarua kimoja bado, James atakapomkosa Ubungo itakuwaje? Si atahisi amechukua usafiri kwenda nyumbani? Je, akifika nyumbani na kukuta hajafika?
James alipoingia Ubungo tu, meseji ya Lina ikaingia…
“Baby simu inazima chaji, sijui itakuwaje?”
Lina alipotuma meseji hiyo, akazima simu na kurudi kukaa kwa mume wake, Semi…
“Sweet, tuondoke, tumbo haliko vizuri ghafla,” alimwambia mume wake…
“Mimi mwenyewe nilitaka kukwambia hivyo.”
Waliondoka eneo hilo, wakiwa njiani, Semi alipokea simu…
“Ee Masua, niambie bosi wangu…eee….wapi? Lini? Aaa, sasa….da! Oke, ngoja nifike nyumbani, nakuja tuondoke.”
Alipokata simu alimgeukia mkewe…
“Baby kuna safari ya Zanzibar saa kumi, inabidi nikuache nyumbani mimi niondoke kwenda uwanja wa ndege.”
“Jamani baby, hizo safari zako bwana,” Lina alijidai hajapenda lakini moyoni alishangilia ile mbaya.
“Si ndiyo kutafuta hela mke wangu.”
“Poa, kurudi lini?”
“Nadhani baada ya siku mbili.”
***
Baada ya mumewe kuondoka, Lina alichukua begi lake aliloondoka nalo kwa James, akaenda kukodi Bajaj hadi sokoni. Alinunua viazi, mkungu wa ndizi, nazi na machungwa. Vitu vyote hivyo akavitia kwenye mfuko wa salfeti na kufungwa kamba.
Safari ikaanza ya kwenda nyumbani kwa James. Ile anafika tu, James naye akaingia na gari...
Je, unajua nini kilitokea hapo? Usikose kusoma kwenye Gazeti la Risasi Jumamosi, Jumamosi ijayo.
Naomba ushauri wako
“Oo! Baby, pole na safari, nilijua utakuwa umeshakuja kivyako maana si uliniambia simu ipo karibu na kuzima chaja!”
“Ndiyo hivyo baby, pole na hapa baba angu?”
“Nimepoa sana mpenzi.”
Walikumbatiana, wakabusiana, wakashikana mkono kuingia ndani maana tayari mlinzi alishafika kumpokea Lina kwenye Bajaj na ule mfuko wake mkubwa.
James alibadili zile hisia kwamba Lina ana mume mwingine zaidi ya yeye, aliamini ni maneno ya Kindaundau tu…
“Mtu awe na mwanaume mwingine wa ndoa kabla yangu halafu afikie kwangu toka safari ya mbali kama Korogwe, haiwezekani, kutakuwa na kitu, tena amekuja na mzigo mkubwa tu,” alisema moyoni James huku picha ya Kindaundau kumdanganya ikimjia kwa mbele walivyokuwa wamekaa siku ile kwenye ule mgahawa kule mjini.
***
Lina, ili ajifanye alikuwa safarini kweli na alimmisi sana mume wake huyo, aliamua usiku huo kumtendea vitu adimu na kumwonesha mapenzi motomoto.
Walipomaliza kula tu aliomba wakaoge, walikwenda chumbani kuoga, Lina ndiye aliyemtaka James waende wakalale kwa kisingizio kuwahi kuamka kesho yake lakini ukweli ni kwamba alitaka wacheze kandanda kitandani.
Walipopanda kitandani tu, Lina alitia hisani, maana alipokumbuka jinsi alivyomwona James pale Mlimani City amekaa na mume wake alisikia huruma sana. Aliamini walikaa jirani kwa sababu viti havikuwa vingi na hakuna aliyekuwa tayari kumjua mwenzake kwa undani.
“Baby, nakupenda sana,” ndivyo alivyoanza kusema Lina akimuweka James kifuani pake…
“Hata mimi nakupenda sweet, nilikumisi sana mke wangu.”
“Kweli, kuliko nilivyokumisi mimi?”
“Hunishindi bwana.”
Mara kulipita ukimya kwani walijikuta wamezama kwenye penzi la upande wa pili, walikuwa ndani ya denda. Miguno tu ndiyo iliashiria kwamba wapo pembeni ya uwanja wakisubiri kuingia kati ili kuanza kusakata soka.
Lina kwa mara ya kwanza alimshika James na kumshusha chini, akamuwekea kiti akae. Halafu akashusha godoro, akalitandika vizuri sana, wakalala hapo…
“Baby leo utanipata kwa staili ya usiku wa kigodoro,” alisema Lina.
Alimvuta James na kumkaribisha kwake huku akimsisitizia kwamba anahitaji mtoto kutoka kwake.
Akili za Lina hapo zilikuwa siyo zenyewe, kwani zilibadilika ghafla na kujikuta eti yuko tayari aachane na Semi kuliko kuachana na James.
Alitumia staili mbalimbali ambazo James hakuwahi kujua kama anazitambua na kila pozi alisisitiza kupewa mimba ndiyo ilikuwa kilio chake kikubwa katika mahaba ya usiku huo.
Kwa sababu walitandika godoro chini, kwa hiyo hata pale mmoja wao alipocheza rafu, hakuna mlio uliotoka. Ilikuwa kimyakimya, sanasana kuhema sana kwa Lina na maneno yenye kubembeleza ndiyo yalisikika kwa mbali lakini.
Lina alimaliza pozi zake zote, sasa akataka kupewa mapozi na James. Naye alikuwa mtaalam, alimuonyesha mapozi ya nguvu, mara wakae wote, mara mmoja asimame mwingine achunge mbuzi, mara mwingine kulia mwingine kushoto lakini bila kuachana.
Lina alianza kupiga kelele na kutangaza ushindi wake alipokalishwa kwenye baskeli kiti cha nyuma halafu dereva akamwangalia lakini wakiwa wanaenda mbele.
Kilio chake kilitoa picha kwamba kweli walikuwa kwenye usiku wa kigodoro…
“Na…na…na mimba nakuhakikishia utapata sweet,” alisema kwa kigugumizi James.
“Mtoto tutamuita Jali dear, yaani mimi na wewe.”
Lina alipomaliza kusema hivyo tu akanyoosha miguu na kusalimu amri akifuatiwa kwa karibu sana na James naye, wakawa wanahema wote!
***
Siku iliyofuata, Lina aliondoka kwenda kazini akimwongopea James anapitia saluni kuosha nywele kwanza maana alipokwenda Korogwe zilichafuka hivyo hakutaka lifti lakini walikubaliana kwamba, jioni waende wakapate dina Mlimani City.
***
Ilikuwa saa kumi na mbili na nusu jioni, Semi alirejea kutoka Zanzibar, akafika nyumbani kwake hakumkuta Lina…
“Uko wapi wewe?” Semi alimtumia meseji mkewe.
“Nipo saluni baby wangu. Vipi hali yako sweet?”
“Sawa, hali yangu mi mzima sana,” alijibu Semi bila kusema amerudi.
Alioga, akavaa akatoka. Safari yake ilikuwa kwenda Mlimani City kwenye ahadi moja ambapo ilimlazimu arejee Dar halafu kesho yake aende tena Zanzibar.
Alikanyaga mafuta hadi Mlimani City. Kwa folenifoleni alijikuta amefika Mlimani City saa moja na dakika kumi giza likiwa limeingia tayari.
Aliegesha gari na kwenda kukaa. Ile anaweka kikao kwenye kiti tu, anasikia sauti ikimsalimia…
“Bro za tangu jana, kama nakukumbuka,” alisema James ambaye kiti alichokaa aliweza kuonana na Semi moja kwa moja wakati kiti alichokaa Lina alimpa mgongo kwa hiyo Semi alimwona kwa nyuma.
Kabla hajaitika salamu ya James, Semi alikaza macho kwa Lina, akashangaa, akasimama na kumfuata…
“Lina,” aliita huku akimwangalia usoni na kumshika begani…

Endelea kulike: www.facebook.com/2jiachie
Tembelea: www.2jiachie.com

No comments

Powered by Blogger.