AUNT: NILIONANA NA NYALANDU UKUMBINI
STAA wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel, amesema hakuna
ukweli wowote wa yeye kutanua na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro
Nyalandu nchini Marekani, kwani alikutana naye ukumbini, akiwa amealikwa
na blog iitwayo Vijimambo ambayo hutangaza utalii wa Tanzania nchini
humo kila mwaka.
Alisema wakati wa safari yake hakuelewa lolote kuhusu Waziri Nyalandu na anashangazwa na yanayozungumzwa hivi sasa kwani baada ya kumsalimia walipokutana, hawakuwahi kuonana tena hadi aliporejea, kwani yeye alikuwa amepangiwa kwenye hoteli ambayo pia ndiyo ukumbi wa shughuli hiyo ulipokuwa.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akizungumza jambo.
“Watu wanataka kunijengea uadui na mke wake Faraja Kota ambaye
tunaheshimiana sana, mimi nilialikwa kule nikiwa na wasanii wengine,
wanamuziki Kassim Mganga na IT na hata malipo ya kazi yangu nililipwa na
wao, wanaosema nilitumia hela za wizara sijui wanataka nini, kama
wizara iliwapa fedha hao waliotualika mimi sijui,” alisema muigizaji
huyo.
Post a Comment