ad

ad

MONO NDIYE ATAIONGOZA ATLETICO KESHOKUTWA DHIDI YA MADRID NDANI YA BERNABEU


Baada ya Diego Simeone kusimamishwa kwenye mechi ya watani wa Hispania, Real Madrid na Atletico Madrid, sasa jukumu hilo amekabidhiwa Germán Burgos ‘Mono’.

Inaaminika Mono ndiye mtu wa Atletico Madrid asiyeipenda Madrid kuliko wote.
Madrid ilimsumbua sana wakati akiwa kipa wa A Atlético na sasa ataiongoza pale Santiago Bernabéu, keshokutwa Jumamosi.
Siku zote Mono amekuwa akiizungumzia mechi aliyokuwa langoni na Madrid ikashinda mabao 2-1 yote yakifungwa na Luis Figo.
Hata hivyo alijitahidi kuokoa mkwaju wa penalti ambao ulimuumiza pua na damu kuvuja kwa wingi.
Hakuwa kushinda dhidi ya Madrid hadi alipokuwa kocha msaidizi.
Wakati fulani aliwahi kumuambia Kocha Jose Mourinho akiwa Madrid: “Mimi siyo Villanova, ntakuvunja shingo yako.”

Hata hivyo katika mechi iliyofuata, Atletico ikanagukia pua kwa Madrid. Swali je, kesho akiwa bosi kwa muda atalipa kisasi?

No comments

Powered by Blogger.