ILIPOISHIA
“Manka
karibu.”
“Asante
bosi, kazi iliyokuwa na haraka nayo tayari.”
“Ooh,
vizuri sana sikutegemea ungeifanya kwa muda mfupi hivi.”
“Najitahidi
japo nilikuwa na muda mrefu sijagusa computer,” nilimjibu huku nikimkabidhi
kalatasi, nami nikiachia tabasamu pana ambayo huogopa kuitoa kwa wanaume ili
kuepusha ungongano wa mawazo.
Ilikuwa
ugonjwa wa wanaume kila ninapotabasamu mashavu huweka visima ‘dimples’ wanaume wengi ulikuwa uchawi mkubwa kwao.
Kila mwanaume niliyekutana naye alipenda kunifurahisha ili aone madhari
mantashau ya mashavu yangu.
Lakini
pamoja na yote sikuwa na sifa ya kumteka mwanaume kimapenzi zaidi ya kunionja
na kuniacha. Wasiwasi wangu huenda mwili wangu hauna asali itakayo mfanya
mwanaume yoyote atakaye nionja anirudie mara mbili. Basi baada ya kupokea
aligeuka na kuondoka kurudi ofisini kwangu.
Nilipofika
mlangoni nilikumbuka kitu nilitaka kumuuliza bosi, niligeuka ili nimuulize kitu. Niligeuka
ghafla na kukutanisha macho na bosi ambaye kumbe nyuma yangu alikuwa
akinifuatia. Maskini kaka wa watu alishtuka mpaka akadondoka chini, nilijikuta
namuonea huruma.
Nilirudi
hadi chini alipokuwa amekaa bila kuonesha kujinyanyua, mwili wake haukuwa
mkubwa sana nilimshika mkono ili kumnyanyua.
“Hapana
Manka nitanyanyuka mwenyewe.”
“Hapana
bosi naomba unipe mkono,” nilimwambia kwa sauti ya huruma yenye kubembeleza.
Alinipa mkono na kumnyanyua, baada ya kunyanyuka nilitoa kitambaa changu na
kumfuta sehemu yenye vumbi.
“Tosha
Manka sehemu zingine nitafuta mimi.”
“Hapana
bosi ni wajibu wangu kufanya hili.”
Aliniacha
nimfute kisha nilimtengenezea kiti na kumuomba akae.
“Unaweza
kukaa.”
Bila
kuongeza neno alikaa kwenye kiti chake huku uso wake ukionesha aibu imemtawala.
“Pole
bosi,” nilimwambia kwa sauti ya chini.
“Asante.”
“Hukuumia?”
“Nipo
sawa.”
“Pole
sana.”
“Asante
Manka, nipo sawa kaendelee na kazi.”
Niligeuka
na kuondoka hata nilichotaka kumuuliza nilikiacha na kupanga kumuuliza kupitia
simu yangu ya mezani. Nilitoka hadi ofisini kwangu kuendelea na kazi, kabla ya
kuanza kazi nilijikuta nikijiuliza kilichomdondosha bosi wangu ni nini.
Wasiwasi
ulikuwa uleule bosi kapagawa na mimi, kitu ambacho sikutaka kinitokee kwa muda
ule kwani ilikuwa mapema sana. Niliamini kabisa bosi kwa mtazamo wa nje alikuwa
amepata bonge la mwanamke, lakini ndani sikuwa na sifa zile za kukaa na
mwanaume kwa muda mrefu.
Niliyapuuza
na kuendelea na kazi, nilikumbuka kuna kazi nilitaka kupata maelekezo kwa bosi.
Nilimnyanyua simu kumpigia baada ya kuita kwa muda ilipokelewa.
“Haloo
bosi.”
“Ooh..Aah...Nani
Manka,” maskini bosi wangu alionesha kiwewe bado hakijamtoka.
“Bosi
mbona hivyo?”
“Aah,
kawaida tu, unasemaje?”
“Ok,
bosi nilikuwa nauliza hii kazi ya malipo kuna maandishi ya mkono nayo
niyaandike?”
“Hakuna
tatizo, yaandike kama ilivyoandikwa.”
Nilikata
simu na kuendelea ka kazi yangu kama kawaida, baada ya muda nikiwa bize simu ya
mezani iliita, nilinyanyua na kupokea.
“Haloo
bosi.”
“Ndiyo
Manka jiandae tukapate lunch.”
“Nashukuru
bosi.”
Baada
ya kukata simu, niliangalia saa kubwa ya ukutani iliyokuwa mbele yangu, ilionesha ni saa saba
kasoro kumi mchana. Nilimalizia kazi yangu ili nipate muda wa kwenda kula,
nikiwa bado nimeinama nikirekebisha tatizo la kisarufi nilishtuliwa na sauti ya
bosi.
“Manka
tunaweza kwenda.”
“Hakuna
tatizo bosi, namalizia kurekebisha sarufi.”
“Utamalizia
tukirudi.”
Nilisave
kisha nilizima computer na kunyanyuka, nilijitengeneza vizuri nguo niliyovaa.
Kwa chati nilimuona bosi wangu koo likimcheza kama mtu mwenye kiu kikali. Baada
ya kuhakikisha nipo sawa tulitoka hadi kwenye gari lake kisha tulikwenda kwenye
moja ya hoteli ya kifahari ambayo ilinikumbusha mbali enzi nipo kwenye ndoa
yangu.
Tulipofika
Mateja alionesha kutojiamini sana kwangu kitu ambacho sikuamini mwanaume kama
yeye kuwa katika hali ile. Sikuwa na sifa kubwa zaidi ya mwanamke aliyepoteza
matumaini ya kupata hadhi mbele ya mwanaume. Niliamini kaniona kwa nje
hanijui ndani nilivyo ndio maana
ananipapatikia.
Nilijua
akikipata anachokitafuta kwangu pengine ndiyo siku ya kunifukuza kazi, lakini
sikuwa na jinsi kila mwanaume mwenye pesa aliamini mwanamke sahihi wa kukaa
naye ni mimi. Baada ya kuketi kwenye viti vyetu muhudumu alifika na kutaka oda
zetu.
“Manka
agiza chochote ukitakacho kwa bei yoyote.”
“Asante,
nataka kula unachokipenda wewe,” utanishangaa kwa nini nimesema vile, nilifanya
vile ili kumtoa wasiwasi na kumfanya awe huru kwangu japo si katika suala la
mapenzi.
“Hapana
Manka nataka wewe leo ndio uchague chakula tutakacho kula.”
“Sawa,”
nilichagua chakula ambacho wote tulikuwa.
Baada
ya chakula wakati wa kunywa vinywaji Shaka aliniuliza.
“Samahani.”
“Bila
samahani.”
“Manka,
umeolewa?”
“Sijaolewa.”
“Una
mchumba sina?”
“Sina.”
“Rafiki
wa kiume?”
“Sina.”
“Manka
mbona unanidanganya.”
“Kweli
bosi.”
“Hivi
Manka kwa umbile alilokujali muumba usiwe na mwanaume?”
“Si
kwamba sijawahi mwanaume ila kwa sasa sina.”
“Kweli?”
“Kweli
kwa nini nikufiche ili iwe nini?”
“Mara
nyingi watu wamekuwa si wakweli.”
“Huo
ndio ukweli wangu.”
“Kwa
nini mrembo kama wewe huna rafiki wa kiume?”
“Sina
bahati nimeamua kuishi peke yangu.”
“Ina
maana hata ombi langu litagonga ukuta?”
“Ombi
gani?”
“Kwa
vile huna mtu nilifikili unafaa kuwa mke wangu.”
“Aaah,
bosi,” kauli ile ilinishtua sikupenda kuisikia masikioni mwangu.
Sikuwa
na jibu la moja kwa moja, moyo mapigo ya
moyo walinienda mbio na machozi yalinitoka. Mateja alishtuka kuniona nikitoka
machozi badala kumpa jibu lake.
“Manka
vipi?”
“Hataa,”
nilitikisa kichwa.
“Mbona
machozi yanakutoka.”
“Kauli
yako imenishtua.”
“Kivipi?”
“Sikutegemea
kuniambia neno hilo mapema kiasi hiki.”
“Manka,
penzi limuingiapo mtu huwa kama kichaa aliyekatikiwa na mishipa ya fahamu.
Niyasemayo si mimi ni moyo wangu naomba unihurumie.”
“Ni
kweli, lakini sina bahati kila siku mapenzi limekuwa likinitesa.”
“Kivipi?”
“Mpaka
leo sijajua sababu ya kuachwa na wanaume.”
“Ni
wazi wote waliopita walikuwa na tamaa ya kukujua ulivyo na si mapenzi ya dhati.
Lakini nakuamini mimi ndiye mwanaume sahihi kwako.”
“Hiyo
kauli kwangu nimeizoea, lakini mwisho wa siku mambo huwa kinyume.”
“Niamini
Manka, nitakuwa mume mwema.”
“Mmh
nitashukuru, lakini usinitende utaniumiza.”
“Siwezi.”
Baada
ya chakula tulirudi ofisini, hatukufanya sana kazi Mateja alikuwa na uchu wa
fisi. Aliniomba tufunge ofisi twende tukastarehe, sikuwa na pingamizi nilifunga
kazi na kuongozana naye kwenye gari lake. Mateja alinipeleka kwenye hoteli ya
kifahari ya nyota tano.
Kwa
vile shida yake niliijua sikushtuka kumsikia akiuliza chumba cha VIP, baada ya
kulipia tulikwenda kwenye chumba kilichokuwa ghorofa la pili. Chumba
kilichokuwa cha kifahari, ambacho kilikuwa kipo katika hadhi ya juu. Katika
maisha yangu sikuwahi kuingia kwenye chumba kizuri kama kile.
Chumba
nilikiona kilikuwa kinapendeza lakini wasiwasi wangu bosi wangu atakipata
alichokifikilia kukipata mwilini mwangu. Sikutaka nami kijiweka nyuma kwani
nilikumbuka kauli za Bi Shuu mama mlezi wangu shangingi mstaafu, kuwa niwapo
mbele ya mwanaume nijionesha nipo tayari kumpa kile anachokitaka.
Siku
zote aliniambia nijiamini ili kumfanya mwanaume naye ajiliuze mara mbili mbili
ataniingiaje. Sikupoteza wakati baada ya kuingia tu chumbani nilivua nguo zote
na kubakia kama kuku aliyenyonyolewa. Sikuchelewa kumsaula na yeye tukawa sale
sale maua.
Nilitembea kama miss kuelekea kwenye kabati
kuchukua taulo kwa makusudi nimuoneshe umbile langu ambalo mwanzo huwa utata
kwa wanaume.
Lakini
wakiisha nipata nakuwa kama Big G iliyotafunwa na kuisha utamu mwisho wake
hutemwa. Kwa kweli sikupenda kutongozwa siku moja na siku hiyo hiyo kumvulia
mwanaume nguo ya ndani.
Niliamini kabisa kujilahisi vile lazima
thamani yangu ingepungua lakini kama ningemzungusha, kidogo thamani yangu kwake
ingepanda. Nilijua lazima ataniona maharage ya Msanga maji nusu kijiko. Lakini
sikuwa na jinsi kutokana na njia aliyotumia kwa kweli nilijikuta siwezi kuuruka
mtego wake mwepesi. Sikuwa ndege mjanja lakini nilinaswa kijinga sana, japo
sikujua tatizo langu lakini nilipokuwa natembea na kumuachia umbile la nyuma
lililokuwa linawatesa wanaume wengi. Niliinama makusudi kama najikuna mguu ili
tu nizidi kumpagawisha.
Kitu
kilichofanya Mateja azidi kuwa katika wakati mgumu, wakati nafungua kabati
nitoe taulo Mateja alikuwa tayari yupo nyuma yangu na kunikumbatia kwa nyuma.
Nilijua uzalendo ulikuwa umemshinda, mambo yalianzia pale.
Tulianza
kubadilishana mate palepale kwenye kabati, baada ya muda aliona anachelewa,
mwanaume alinibeba juujuu mpaka kitandani. Kwa vile mchicha ulikuwa
umeishakolea nazi tuliumwaga juu ya ubwabwa na kuanza kujimegea tataribu.
Mateja alionekana ana pupa kama mamba mwenye njaa, hakuchelewa kukifikisha
chombo ukingoni mwa bahari.
Baada
ya mapumziko mafupi tulirudi ndani ya ngarawa kuendelea na safari, katika vitu
ambavyo katika maisha yangu nilikuwa sivipendi ni usumbufu ndani safari. Ooh
geuka hivi, lala hivi, inama hivi, nyanyuka hivi, kwa upande wangu niliona
usumbufu lakini nilivumilia kwa vile ndiyo ilikuwa siku yetu ya kwanza
kukutana.
Kama
ningekuwa nimemzoea ningempasha, kwani hakuna starehe ya mapenzi mpaka
kusumbuana kumgeuza mwenzako kituko,ile kwangu sikuona mapenzi zaidi ya adhabu.
Siku zote niliamini baada ya safari ndefu mtu humwaga mzigo na kutelemka. Siku
ile tulikaa kaa mpaka saa tatu usiku baada ya kuoga na kula alinirudisha
nyumbani.
Kabla
ya kuondoka Mateja aliniahidi vitu vingi ikiwemo kunijengea nyumba kuninunulia
gari na kuyabadili maisha yangu kwa ujumla. Siku ile moja tu alinipatia laki
tano taslimu, sikuamini niliona miujiza kupata raha na kiasi kikubwa cha pesa
kama kile.
Nilipofika
nyumbani nilimkuta Bi Shuu yupo chumbani kwake, Nilifungua mlango wa chumba
changu na kuingia ndani. Nilipowasha taa nilishtuka kumuona Bi Shuu kanisimamia
nyuma, akuzungumza chochote ila alinikata jicho kali.
“Shikamoo
Bi Shuu”
“Hainisaidii
kitu”
“Mbona
hivyo mama yangu”
“Kazi
gani ya kutoka saa moja asubuhi kurudi saa tano za usiku?”
Mmh,
makubwa nimekuwa mtoto mdogo wa kuwa chini yake kwa kila kitu. Nilijua uchawi
wa Bi Shuu ni nini, niliinama na kuchukua mkoba wangu na kufungua. Nilihesa
nyekundu tano na kumpa.
“Za
nini?”
“Katumie
tu”
“Za
kodi?”
“Walaa,
nimekutunuku tu mama yangu.”
“Kweli!?”
“Kweli
unafili uliyonifikiza madogo”
Bi
Shuu alifurahi na kunikumbatia na kusahau aliyobwatuka muda mfupi, baada ya
kunipandisha na kunishusha alisema.
“Weee
mwana kulikoni”
“Kaa
chini nikupashe kazi imekuwa kaziiiii”
“Usiniambie”
ITAENDELEA SIKU YA KESHOOOOOOOOO
Post a Comment