SUAREZ AOMBA RADHI KWA KUMNG'ATA CHIELLINI,
MSHAMBULIAJI
Luis Suarez amepoza shutuma dhidi yake baada ya Jumatatu usiku
kuomba radihi kwa kumng'ata Giorgio Chiellini na ameahidi kutorudia
kufanya kosa kama hilo - huku Barcelona ikipiga hatua zaidi katika
kuwania saini yake.
Siku
nne baadea ya kufungiwa miezi minne na ameambia FIFA kwamba tukio hilo
lilitokea katika mechi ya Kombe la Dunia kati ya Uruguay na Italua mjini
Natal lilitokana na kushindwa kujizuia.
Mshambuliaji
huyo wa Liverpool ameibuka kikamilifu na kujutia kosa lake. Lakini
kuomba kwake radihi kunakuja katika wiki ambayo habari zimevuma mchezaji
huyo mwenye umri wa miaka 27 anatakiwa kwa dau la Pauni Milioni 80 Nou
Camp.
Gary
Lineker, mshambuliaji wa zamani wa Barcelona, amesema klabu hiyo ya
Katalunya imemuambia Suarez bombe msamaha kama wanataka waendelee na
jitihada za kumnunua.


Post a Comment