BEYOND LOVE- (ZAIDI YA MAPENZI) SEHEMU YA 11 MPAKA YA 20
Beyond love-11
Wakiendelea
na maongezi, mlango wa chumba cha wagonjwa mahututi ulifunguliwa, muuguzi
akatokeza nje akionyesha wasiwasi mwingi na kumuomba daktari aingie haraka
chumbani kwani mgonjwa tayari alikuwa amekufa! Daktari huyo aliyejulikana kwa
jina la Dk. Mbisse aliingia ndani haraka
akimuacha mama yake Mariam, muda mfupi
baadaye mama huyo alianguka chini na kupoteza fahamu, ikabidi watu waliokuja
naye wambebe juu juu mpaka idara ya
wagonjwa wa nje ambako daktari
alipomuona tu alionyesha wasiwasi na
kuanza kuuliza maswali huku akimuangalia mgonjwa usoni.
Je, nini
kitatokea? Mariam amekufa? Mama yake Je?
Kinaendelea nini kwenye maisha ya Tom huko machimboni? SONGA NAYO.
“Mh!”
Daktari aliguna tena na kuzidi kuwatia wasiwasi watu waliompeleka mama yake Mariam
kwenye chumba chake, hisia kwamba alikuwa amepoteza uhai zilianza kuwaingia
vichwani mwao, wakiwa nje waliendelea kusikiliza kupitia dirishani kila kitu
kilichoendelea.
“Shinikizo
lake liko juu sana, sijawahi kuona presha ya aina hii, ni lazima aanzishiwe
dawa sasa hivi vinginevyo atapasuka mshipa kichwani, inavyoonekana ni mgonjwa
wa presha wa muda mrefu ila alikuwa hajitambui!” Sauti ya daktari iliwafikiwa
majirani waliokuwa wameketi nje kwenye benchi wakisubili kupewa maelezo.
“Dawa
gani tunamuanzishia daktari?”
“Mpeni
Rosartan na Aprinox haraka iwezekanavyo, halafu muendelee kumpima shinikizo
lake kila baada ya nusu saa na nipewe taarifa, kama kuna tatizo lolote niiteni
haraka iwezekanvyo, mmenisikia?” Daktari aliuliza.
“Ndio
daktari!”
“Haya
mpelekeni chumba cha wagonjwa mahututi haraka iwezekanavyo!”
“Sawa
daktari!”
Mama yake Mariam akashushwa kitandani na
kulazwa juu ya machela kisha kusukumwa
kuelekea chumba cha wagonjwa mahututi, majirani na marafiki wakifuata nyuma
kutaka kufamu kilichotokea. Walifurahi baada ya wauguzi kuwaeleza kwamba mama
yake Mariam alikuwa hajafa, bali shinikizo lake la damu lilikuwa limepanda mno,
hivyo lilihitaji kushushwa ili aweze kurejewa na fahamu zake.
Chumba
cha wagonjwa mahututi mama yake Mariam alilazwa kwenye moja ya vitanda
vilivyokuwemo, akawekewa mashine ya hewa ya Oksijeni iliyofunika pua na mdomo wake kisha dawa
zilizoandikwa na daktari zikaanza kutolewa
kwenye njia ya mshipa na vidonge. Kitanda kilichokuwa jirani na mahali alipolazwa mama
huyo, palikuwa na pazia la rangi ya kijani lililozungushwa kwenye kitanda huku madaktari na wauguzi wakionekana
kuhangaika, baadaye Dk. Mbisse alitokeza
nje na kumuona mama yake Mariam.
“Mh!
Huyu mama si nilikuwa naongea naye hapo nje?”
“Ndio!”
”Imekuwaje tena?”
”Imekuwaje tena?”
“Baada
ya kuongea naye tu alianguka chini na
kupoteza fahamu!”
“Farida
makosa yak ohayo!”
“Kwanini
daktari?”
“Ulitoa
ujumbe vibaya, nadhani alifikiri mtoto wake amekufa, siku nyingine ukiwa unatoa taarifa za aina
hiyo lazima uangalie kwanza mazingira, mgonjwa alikuwa amepoteza fahamu tu wewe
ukafikiria amekufa halafu ukaniita kwa kusema “Daktari mgonjwa amekufa!” Hiyo ni kinyume cha taaluma, siku nyingine
usifanyi hivyo, sawa?” Dk Mbisse
aliongea kwa sauti ya chini.
“Sawa
daktari nimesikia, sitarudia tena!”
“Hebu
nimuangalie kidogo!” Dk Mbisse aliongea akikisogelea kitanda cha mama yake
Mariam, alipokifikia alianza kumpima shinikizo la damu, hata yeye alipomaliza
pia aliguna na kumpigia simu daktari aliyemuona kwa mara ya kwanza, wakajadiliana na kukubaliana kuongeza dozi ya
dawa kwani shinikizo lilikuwa juu mno.
*********
Mama
yake Mariam alirejewa na fahamu masaa sabini na mbili baadaye, ikiwa katikati
ya usiku, akaangaza macho yake huku na kule chumbani akijaribu kutaka kuelewa
ni wapi alipokuwa. Fahamu hazikumwijia upesi mpaka alipouona mrija wa dripu
ukiteremka na kuingia kwenye mshipa wa mkono wake, hapo ndipo akaelewa
kwamba alikuwa hospitali. Kikohozi kikamkaba na kujikuta akikohoa, hicho ndicho
kilimfanya mtu aliyekuwa kando yake azinduke usingizini, macho yao yakagongana
na mtu huyo akatoa tabasamu.
“Pole
sana mke wangu, ndio Dunia ilivyo!”
“Baba
Mariam!”
“Naam mke wangu!”
“Nisamehe
kwa yote yaliyotokea, sikumruhusu Mariam atoke, aliiba gari nikiwa usingizini!”
“Usijali
hayo mke wangu yamekwishatokea!”
“Yuko
wapi Mariam?”
*********
Machimboni
Tom aliendelea na maisha yake, kazi yake kubwa ikiwa ni kuosha mabaki ya
mchanga wa dhahabu ulioachwa na matajiri akitumia madini ya Zebaki, kiasi
kidogo cha fedha kilichopatikana alikitumia kwa chakula na kumtumia mama yake
matumizi! Hakuwa na mahali pa kulala, siku zote usiku ulipoingia alilala kando
ya mto karibu kabisa na mahali alipofanyia kazi zake. Haikuwa rahisi kwa mtu
yoyote kuelewa alikuwa kijana mwenye uwezo mkubwa darasani, aliamua kukatisha
masomo sababu ya umasikini, jambo hilo wala hakutaka kuliongelea akiwa na
marafiki zake.
Alikuwa
mkimya kupita kiasi, asiye na maneno mengi wala ugomvi na vijana wenzake jambo
ambalo kwa machimboni lilikuwa ni kawaida,
karibu kila kijana alitembea na kisu na wengi walikuwa wamejaa majeraha
miilini mwao sababu ya kuchomana visu! Hapakuwa na kituo cha polisi wala mahali
pa kutoa malalamiko mtu alipoonewa, wanawake walifanyiwa unyanyasaji wa kutisha
wakibakwa mbele za watu lakini hakuna aliyechukua hatua, hayo ndiyo yalikuwa
maisha ya machimboni ambayo Tom alilazimika kuishi ndani yake sababu alikuwa
akitafuta mafanikio baada ya njia ya
kupitia shule kushindikana.
“Naweza, naweza kufanikiwa pia kwa njia hii, kuna watu
wengi tu Duniani walioacha shule na wakafanikiwa, ni kweli shule ni muhimu
lakini inaposhindikana si mwisho wa kila jambo, bado upo uwezekano wa
kufanikiwa kama binadamu akitumia akili yake!” Hayo ndiyo yalikuwa mawazo yake
kila siku asubuhi kabla ya kwenda kazini,
hakuwa amekata tamaa na aliamini siku moja angepata mafanikio makubwa
sana na kurejea tena Dar es Salaam ambako angemtafuta tena Mariam mpaka ampate
na kumuonyesha kwamba kitendo cha kumkimbia akiwa na shida hakikuwa cha
kiungwana hata kidogo.
“Ipo
tu siku changudoa yule atanitambua!
Nitamuonyesha mie ni nani, yeye si anajidai na utajiri wa baba yake, mimi
nitakuwa nazo zangu mwenyewe, hivi sasa naamini Duniani hakuna mapenzi ya
kweli, watu wanadanganyana tu, kwa jinsi Mariam alivyokuwa akiniambia maneno
mazuri vile, kumbe yote yalikuwa kamba? Siamini, sitampenda mwanamke tena,
naapa!” Tom alisema moyoni mwake akiosha mchanga kando ya mto, bado chuki
dhidi ya Mariam iliula moyo
wake, alimchukia msichana huyo kuliko
kitu kingine chochote chini ya jua la
Mungu.
Je,
nini kitaendelea
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
Beyond Love -12
Tom alifanya kazi kwa nguvu akiwa na usongo wa kupata utajiri ili siku
moja arejee Dar es Salaam na kumwonyesha
Mariam kwamba maisha na mafanikio yalikuwa ni kwa kila mtu, si kwa watoto wa matajiri peke yao. Ndio maana
alikuwa na nidhamu katika kila fedha aliyoipata, hakujishirikisha katika mambo mabaya kama
ulevi na uvutaji wa bangi, ambayo
yalifanywa karibu na vijana wote wa machimboni.
Je, nini kitaendelea? Tom
atafanikiwa? Mariam yu hai au amekufa? SONGA NAYO…
“Yeke mura! Mang’ana?” (Vipi mshkaji mambo?) Tom
alimsalimia Mwita kulipokucha asubuhi wakijaanda kuondoka kwenye kibanda chao
kidogo kwenye mto kuendelea na kazi yao
ya kuosha Marudio.
“Maia!” (Safi tu)
Ilikuwa ni saa kumi na mbili asubuhi, wote watatu
wakaamshana na kuanza kuondoka kuelekea mtoni, kila mmoja wao akiwa na
uchungu moyoni mwake, wote walikuwa ni
watoto wa masikini waliotamani sana kufanikiwa katika maisha yao, wakiwa
njiani Tom aliwaeleza mambo mbalimbali
aliyoyasoma kwenye vitabu vya watu waliofanikiwa kama Donald Trump, Robert
Kiyosaki na Bill Gates, alieleza kwa
lugha rahisi ili wapate kumwelewa na
pia wasigundue kwamba alikuwa na elimu
kuwazidi, jambo ambalo hakutaka kabisa ligundulike, siku zote alitaka kufanana
na watu waliomzunguka ili iwe rahisi kufanya nao kazi.
“Ili ufanikiwe ni lazima uwe na ndoto, ninaposema
ndoto simaanishi kulala na kuota, uwe unatamani kuwa kama mtu fulani na ufanye
kazi kwa nguvu kufikia kiwango hicho cha maisha, uwe tayari kupitia kwenye
dhiki zote alizozipitia mtu huyo, tatizo letu tunatamani kuwa kama Yesu Kristo lakini hatupo tayari kusulubishwa
msalabani, tunataka kwenda Mbinguni
lakini hatuko tayari kufa… wewe Mwita unataka uwe kama nani maishani mwako?”
“Gachuma!”
Mwita alitamka kwa ujasiri, Gachuma alikuwa mfanyabiashara maarufu sana
miongoni mwa kabila la Wakurya, wengi walimchukulia kama mfano wa kuigwa.
“Uko tayari kupitia matatizo yote aliyoyapitia
Gachuma?”
“Sana tu”
“Wewe Gimonge unataka kuwa kama nani?”
“Kuna rijamaa rimoja ra Mwanza rinaitwa
Rikishimba” Gimonge alisema kwa Kiswahili chenye lafudhi ya Kikurya akimtaja
mfanyabiashara mmoja wa Mwanza
Wote walikuwa na ndoto za
kufikia hatua fulani maishani mwake,
kila siku asubuhi mpaka jioni waliongea mafanikio, magari mazuri,
wanawake wazuri, nyumba nzuri, nguo nzuri pamoja na heshima ambayo wangepewa
kama wangefanya vizuri maishani mwao. Walijiona wadogo ambao kesho yake
wangekuwa wakubwa, hawakufanya mchezo hasa Tom ambaye kila alipomfikiria mama
yake nyumbani machozi yalimtoka,
alitamani sana kubadilisha maisha ya mama yake ili naye apate
kuheshimiwa na majirani waliombeza na kumdharau kwamba yeye na mume wake
walikimbilia mjini ambako maisha yaliwashinda.
Kidogo alichopata Tom alikitumia na mama yake,
sehemu nyingine akatunza kama akiba akiwa na lengo la kufungua biashara
ndogo machimboni lakini hakufanikiwa, kwani
fedha ilipoongezeka na kufikia
mtaji wa kufungua duka, alipata taarifa
kwamba mama yake ni mgonjwa, akaondoka machimboni kwenda kumwona. Hali
aliyomkuta nayo ilikuwa ya kusikitisha, alikuwa amepungua kupita kiasi na miguu
imevimba, uso wake ukiwa mweupe na mashavu yametuna na macho yakiwa na rangi ya
njano.
“Pole mama”
“Ahsante mwanangu,
hali yangu si nzuri, ni bora umekuja ili unipeleke hospitali”
“Hakuna shida mama, nina fedha kidogo hapa ambayo
nimepata, bila shaka itakusaidia!”
“Ahsante sana mwanangu”
Walikubali na siku iliyofuata Tom alikodisha
baiskeli na kumbeba mama yake mpaka Tarime
Mjini ambako alimpeleka hospitali ya Wilaya, uchunguzi ukafanyika na
kugundua kwamba mama huyo alikuwa na tatizo
kwenye Wengu lake, lilikuwa limepanuka na kuongezeka ukubwa, jambo
lililofanya liwe na uwezo usio wa kawaida wa kuvunjavunja chembechembe za damu.
“Kwa kitaalam hali hii inaitwa Splenomegally!” daktari alimwambia Tom
mbele ya mama yake.
“Atapona?”
“Atapona lakini itachukua muda mrefu, kwa hivi
sasa itabidi alazwe wodini kuongezewa damu na pia tufanye uchunguzi zaidi
kutafuta sababu ni kwanini Wengu limevimba!” Dk. Richard Mitiro alimwambia Tom ambaye uso wake ulionyesha kukata tamaa.
“Itagharimu shilingi ngapi matibabu yake?”
“Si fedha nyingi, lakini atahitahi mtu wa
kumwongezea damu”
“Nina shilingi elfu hamsini tu, ila damu ninayo nyingi”
“Zinatosha, ngoja niandike kwenye fomu uende maabara kupima damu tuone kama inafaa
kumwongezea mama yako”
“Sawa daktari”
Mama alichukuliwa na kwenda kulazwa wodini, Tom akapelekwa maabara ambako damu yake ilichukuliwa na kuchunguzwa
ikilinganishwa na ya mama yake ambayo pia ilichukuliwa baadaye na kuonyesha
alikuwa na uwezo wa kumtolea chupa tatu, mchana wa siku hiyo hiyo akatoa damu
na mama yake akaanza kuongezewa mpaka siku iliyofuata jioni ndio zoezi hilo
likakamilika. Tom alishindwa kuondoka,
ikabidi abaki na mama yake hospitali kwa muda wa wiki
nzima majibu yalipotoka na kuonyesha
kuvimba kwake kwa Wengu kulisababishwa na tatizo kubwa kwenye damu yake.
“Itabidi umpeleke Mwanza!”
“Mwanza? Daktari, Mwanza?” aliuliza kwa mshangao
mkubwa.
“Ndio kijana”
“Hauwezi kunisaidia tu hapa hapa? Sina uwezo wa
kumpeleka mama Mwanza kwa matibabu”
“Kauze hata ng’ombe!”
“Hatuna ng’ombe hata mmoja daktari”
“Inabidi ujitahidi, hali ya mama si nzuri,
anahitaji uchunguzi wa kina zaidi ya uwezo tulionao hapa Tarime, hospitali ya
Bugando itafaa zaidi maana wao wana vifaa vikubwa kuliko tulivyonavyo sisi”
“Ninaelewa daktari, tatizo fedha”
“Kawaone ndugu nyumbani”
“Sina ndugu”
“Sijawahi kuona Mkurya asiye na ndugu”
“Wazazi wangu walitengwa”
“Na nani?”
“Na ndugu zao”
“Sababu?”
“Walikimbilia mjini wakaacha kuwasiliana nao, baba
alipougua na kufariki ndio tukarudi huku na mimi ndiye mtoto pekee kwa wazazi
wangu”
“Nakushauri ukafanye mpango,” daktari alizidi
kusisitiza.
Alichokifanya Tom ni kuondoka ofisini kwa daktari
na kwenda moja kwa moja kitandani kwa mama yake, hakutaka kulia wala kuonyesha
udhaifu lakini mama yake aligundua na
kumuuliza ni kwa sababu gani alikuwa kwenye hali hiyo ya masikitiko, akashindwa
kumficha na kulazimika kuuweka ukweli wote wazi kwamba walitakiwa kwenda Mwanza
kwa uchunguzi zaidi! Mama yake alibubujikwa na machozi ya uchungu, hakuwa
ametarajia kabisa taarifa kama hizo kwani alifahamu hawakuwa na uwezo wa
kufanya jambo hilo.
“Tutatoa wapi fedha?”
“Sijui mama, lakini nashauri tuondoke kwenda
nyumbani, nikakuache ili mimi nikimbie machimboni Nyamongo kujaribu kuhangaika,
labda naweza kufanikisha kwa msaada wa Mungu” aliongea Tom, safari hii
alishindwa kuyazuia machozi, mashavu yake yakalowa na mama yake kuanza
kuyafuta.
“Usijali mwanangu,
Mungu yupo!”
“Sitaki ufe mama, sitaki kubaki peke yangu”
“Mungu atasaidia”
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
Jioni ya siku hiyo hiyo kwa baiskeli ya kukodi Tom
alimbeba mama yake na kumrejesha
nyumbani ingawa hali yake ilikuwa bado dhaifu, huko hawakulala usiku mzima wakiwa wameangaliana,
Tom akiwa na wasiwasi sana na maisha ya mama yake! Hakutaka afe na aliamini
ilikuwepo njia ya kulifanya jambo hilo. Kulipokucha, ingawa kwa shingo upande,
Tom aliaga na kumwacha mama yake akiwa amelala hoi kitandani, hakuwa na uhakika
kama wakati wa kurudi angemkuta akiwa hai lakini ilibidi afanye hivyo kwani
kuendelea kumwangalia peke yake kitandani isingesaidia.
“Mama acha tu niende, utajitahidi kidogo kidogo
kuwa unanyanyuka na kupika, lazima nikatafute fedha, nitakuwa nakuja mara kwa
mara kukuona, nikipata kiasi cha kutosha tu nitakuja nikupeleke hospitali!” Tom
alisema maneno hayo akibubujikwa na machozi, kwake kilichokuwa kikitokea
kilikuwa ni sawa na kumuaga mama yake kwa mara ya mwisho, ndani ya moyo wake alifahamu siku atakaporejea
angekuta maiti imelala kitandani ikiwa
imeharibika! Mawazo hayo yalimfanya afumbe macho kwa kuogopa.
“Nenda tu mwanangu, lililopangwa na Mungu hatuwezi
kulibadilisha”
“Ahsante mama,
buriani”
“Buriani mwanangu”
Tom akatoka na kufunga mlango nyuma yake kisha
kuanza kutembea kwa unyonge akipita porini mpaka akafika machimboni
Nyamongo, hakuwakuta Mwita na Gimonge
kambini kwao, akaelewa tayari walikuwa kazini mtoni wakiosha marudio! Akazidi
kutembea mikono akiwa ameshika nyuma,
machozi yakimbubujika mpaka mtoni ambako hakuwakuta Mwita na Gimonge
jambo ambalo halikuwa la kawaida na kulikuwa na watu wachache sana mtoni siku
hiyo, akazidi kushangaa. Muda mfupi baadaye akapita mtu mmoja na kulazimika
kumsimamisha.
“Wako kwenye shimo namba tatu!”
“Kuna nini?”
“Limetema vibaya mno, watu wote hivi sasa wana
fedha!”
“Mungu wangu!” Tom alitamka neno hilo na kuanza
kukimbia kuelekea kwenye shimo aliloambiwa, hakuna kitu alichohitaji katika maisha yake wakati huo kama kupata
fedha ili aweze kumpeleka mama yake hospitali,
alijisikia mwenye bahati mbaya kutokuwepo wakati shimo hilo likitema
dhahabu.
Alikuta kundi kubwa la watu likiwa zimezunguka shimo hilo, hali ilikuwa tofauti kabisa na alivyotarajia kwani mahali ambako watu wengi walikuwa wamepata fedha alitegemea kuwa na vicheko na furaha lakini wengi wa watu walikuwa wakitokwa na machozi! Moyo wake ukashtuka, hata hivyo akapenya katikati ya watu kwenda mbele ambako alikuta miili kumi ikiwa imelazwa chini, muda huo huo akaguswa begani, alipogeuza kichwa chake alikutana na Mwita, mashavu yake yakiwa yamelowa na machozi.
“Vipi tena?”
“Mwenzetu kafa!”
“Nani?”
“Gimonge”
“Kimetokea nini?”
“Shimo limetitia na kuwabana watu ndani yake, bahati mbaya yeye
na vijana wengine ndio walikuwemo!”
“Ha! Dhahabu zimo?”
“Nyingi mno lakini watu wameogopa kuingia kwa
sababu linaendelea kutitia taratibu!”
“Wee! Kwa hiyo hata nikiingia sasa hivi dhahabu
zimo?”
“Ndio”
“Hebu nipe hiyo RPG yako pamoja na tochi!” Tom alimwomba Mwita vifaa vya
kuchimbia, kichwani mwake taswira ya mama yake mzazi akiwa kitandani akiteseka
kwa maumivu huku akisubiri kifo kwa sababu hapakuwa na fedha ilimwijia.
“Za nini?”
“Wewe nipe tu”
Mwita bila kujiuliza mara mbili alimkabidhi Tom
vifaa vyake, katikati hali ambayo hakuitarajia alishangaa kumwona rafiki yake
akikimbia mbio katikati ya watu na kwenda moja kwa moja kuzama ndani ya shimo
lililokuwa likititia, watu wakashika mikono kichwani mwao katika hali ya
mshangao, mtu mwenye akili timamu asingeweza kufanya jambo la aina hiyo wakati
maiti kumi zilikuwa zimelala chini. Muda huo huo shimo likaanza kutitia, watu wote wakakimbia kwenda pembeni kuepusha
maisha yao.
Je, nini kitatokea? Tom atanusurika au ndio mwisho wake?
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
Beyond love -13
Kumuacha mama yake afe kwasababu ya fedha wakati aliambiwa kwamba dhahabu
ilikuwa inatoka ingawa shimo lilikuwa likititia, halikumuingilia akilini mwake
kabisa. Aliona ni bora afe akijaribu kuliko kumpoteza mama yake ambaye
alitakiwa kuwa na fedha za kumtibu.
Huku watu wakishangaa ujasiri aliokuwa nao, Mwita alichukua tochi pamoja na
RPG yake, kisha akaingia shimoni! Muda huo huo likaanza kutitia! Watu wakaanza
kukimbia ili kukoa maisha yao! Je, nini kitatokea? Tom atapona? SONGA NAYO...
Kwa masaa kadhaa shimo liliendelea kutitia hali iliyowatia hofu sana
wachimbaji waliokuwa jirani na mashimo hayo, hawakuhitaji akili nyingi sana
kufahamu kwamba Tom alikuwa ameshafariki na hataonekana tena!
Watu walihuzunika sana, walishindwa kuelewa ni kwanini Tom alikuwa kujitoa
kafara kiasi kile, kila alikuwa akizungumza lake. Walishindwa kuelewa ni akili
ya aina gani aliyoitumia kuingia shimoni wakati alikuwa akiona maiti zimelala
juu ya mashimo hayo baada ya kutitia.
“Lakini kwanini hamkumzuia?” Mmmoja wa vijana waliokuwa wakijadiliana
alisema.
“Huu ni uzembe wa hali ya juu,” mwingine akadakia.
“Au mlimdanganya?”
“Hapana, aliingia mwenyewe!”
“Kwanini mlimuachia?”
“Hakuna aliyekuwa akijua nia yake, aliomba tochi na RPG kisha ghafla
tukashangaa anakimbilia shimoni, akaingia!”
“Mh! Lakini huyu jamaa mjinga sana!”
“Sana, ni kama alikuwa akitaka kufa!”
Mazungumzo yale yaliwaumiza sana mwita na Gimonge, hawakuona kama walikuwa
na sababu ya kuendelea kuyasikiliza. Walichokifanya ni kuchepuka pembeni kama
wanajadilina jambo fulani kisha baadaye wakaondoka na kwenda nyumbani.
“Vipi kaka, unadhani jamaa atapona kweli?” Mwita alikuwa wa kwanza
kumuuliza rafiki yake Gimonge.
“Sidhani, kwa hali ilivyo?”
“Eh...!”
“Siyo rahisi kutoka akiwa hai!”
“Sasa?”
“Nafikiri cha kufanya hapo ni kwenda kujaribu kama tutaweza kumtoa, lakini
ikishindikana hadi kesho, ni wazi kwamba atakuwa amekufa!”
“Akifa itakuwaje ndugu yangu?”
“Hakuna kitu kingine zaidi ya kwenda kumweleza mama yake hali halisi!”
“Sawa!”
“Turudi machimboni!”
“Twende!”
Waliporudi machimboni hali ilizidi kuwa mbaya kwani shimo lilizidi kutitia,
hapakuwa na matumani ya Tom kutoka akiwa mzima. Kila mtu aliamini Tom alikuwa
amekufa.
******
Asubuhi ya siku iliyofuata Gimonge na Tom walikuwa safarini kwenda kwa mama
yake na Tom kumpa taarifa za msiba wa mwanaye. Kila mmoja alikuwa hafahamu
jinsi gani mama yake Tom angezipokea taarifa hizo kwa majonzi.
Hadi kufikia saa nane walikuwa wameshafika nyumbani kwa mama yake na Tom
ambaye walimkuta akiwa hoi kitandani.
“Shikamoo mama!”
“Marhaba wanangu, hamjambo?”
“Hatujambo, pole sana kwa kuumwa!” Mwita akamwambia.
“Ahsante, hata hivyo nimeshazoea, hapa nasubiri siku yangu ya kufa tu,
najua sitapona!”
“Usiseme hivyo mama, Mungu yupo na wewe, amini kwamba kwake kila kitu
kinawezekana!”
“Vipi mbona mpo hivyo?” Mama Tom aliwauliza baada ya kuona wana majonzi
ingawa walikuwa wakijaribu kuyaficha.
“Hakuna kitu!”
“Semeni tu wanangu, hamuweza kunificha!” Mama Toma akasema kwa uchungu,
tayari alishahisi kwamba kulikuwa na tatizo!
“Mwambie...” Mwita akamwambia Gimonge.
“Mwambie wewe!”
“Hapana mwambie wewe!” Waliendelea kubishana kwa muda mrefu sana, kiasi
mama Tom akazidisha wasiwasi.
“Ni nini lakini wanangu, ni vyema mkaniambia kuliko kubishana, maana hata
kama mtachelewa kuniambia lakini lazima mwishoni mtaniambia tu!”
“Mama...Tom amefariki!”
“Unasema?”
“Tom amefariki mama, hatuna haja ya kukuficha!”
“Ilikuwaje?”
“Alisikia shimo linatoa madini, yeye akaingia ingawa lilikuwa linatitia,
tangu jana hajatoka na tumeshatoa maiti nyingi lakini yake hatujaiona!”
“Tom mwanangu unaondoka na kuniacha mama yako nakufa! Unakufa kabla
hujaiona maiti yangu....Eeeh Mungu naomba umpokee mwanangu, najua na mimi
nitamfuata muda siyo mrefu!” Mama Tom alilia sana lakini baadaye akawaomba wale
vijana aongozane nao Nyamongo.
“Kufanya nini tena?” Mwita akamwuliza.
“Nataka kuona mahali mwanangu alipolala!”
“Lakini unaumwa mama!”
“Najua lakini nitajikaza, lazima nione mahali mwanangu alipolala kabla na
mimi sijafa!”
“Mama kwa hali yako hutaweza kutembea!”
“Mtatumia machela kunibeba!” Hawakuwa na sababu ya kubishana naye tena,
wakakubaliana naye.
Machela ikatengezezwa jioni ile ile na siku iliyofuata walimbeba na kuanza
safari ya kwenda Nyamongo. Walifika jioni majira ya saa 10:15.
“Nipekeni machimboni!”
“Kwanini tusiende asubuhi?”
“Siwezi kulala kabla ya kuona mahali alipolala mwanangu, lazima nione leo
hii hii!” Hakuna aliyepingana naye, walijua ni kiasi gani alikuwa na uchungu.
Wakambeba na kuongoza moja kwa moja machimboni. Walipofika, mama Tom
aliangalia shimo alilofia mwanaye huku machozi yakimtoka. Alionekana akiwa
kimya kwa sekunde chache kisha akafuta machozi yake na kugeuza shingo na
kuwatizama watu waliokuwa wamezunguka eneo lile.
“MWANANGU HAJAFA! TOM YUPO HAI?” Mama Tom akasema kwa sauti kubwa.
“Mama hivi unaona hapo kuna mtu atakayeweza kutoka akiwa hai?”
“Nasema Tom hajafa!” Yalikuwa maneno ambayo yaliyowachanganya wengi, hakuna
aliyeweza kujua sababu za mama huyo kukazania kwamba mwanaye hakufa.
Kitu akabaki ameduwaa.
****
Pamoja na kukandamizwa na mchanga akiwa ardhini, Tom alikuwa akijitahidi
kuchimba kidogo kidogo kwenye mwamba ili aweze kutoka. Pamoja na mateso yote
aliyokuwa akiyapata ya kukosa pumzi, hata mara moja hakuachia mfuko wake wa
salufeti uliokuwa na dhahabu.
Alijitahidi sana kujiokoa lakini pumzi ilikuwa ikimuishia, akilini mwake
alikuwa akihuzunika sana kufa na kumuacha mama yake akiwa katika hali ngumu.
“Najua mama yangu utateseka sana, lakini hakuna jinsi naamini ni mipango ya
Mungu, siwezi kuzuia kifo changu ikiwa Mungu mwenyewe wa mbinguni atakuwa
amenipangia, sina ujanja tena, naelekea kifo changu sasa!” Tom akajisemea
moyoni mwake.
Hakuwa na kitu cha kubadilisha ukweli kwamba alikuwa anakufa! Kitu pekee
kilichokuja akini mwake ilikuwa ni kutafuta toba kwa Mungu wake. Kwanza aliamua
kumsamehe Mariamu, hakutaka kufa akiwa na kinyongo na watu. Baada ya hapo
akakumbuka sala ya Baba Yetu, akaanza kusali ili akifa aende Mbinguni.
‘Baba yetu uliye Mbinguni,
Jina lako litukuzwe,
Ufalme wako uje,
Mapenzi yako yatimizwe hapa duniani,
Kama yatimizwavyo huko mbinguni,
Utupe leo riziki zetu,
Utusamehe makosa yetu,
Kama tunavyowasamehe waliotukosea,
Usitutie majaribuni,
Bali utuokoe na yule muovu,
Kwakuwa ufalme ni wako,
Na nguvu,
Na utukufu,
Hata milele,
Amen.’
Alipomaliza sala hiyo akavuta pumzi ndefu sana kisha akazishusha taratibu
akihisi kifua kumbana. Akayafumbua macho yake kisha akaufungua ule mfuko wa
salufeti, akasikia mapigo ya mopyo wake yakipiga paaa!
“HAPANA, LAZIMA JAMBO FULANI LIFANYIKE NIWEZE KUTOKA HUMU SHIMONI! NIKITOKA
LAZIMA NITAKUWA TAJIRI MKUBWA NA HATA MAMA YANGU ATAPONA! MUNGU ALIYENIUMBA
AMBAYE NILIKUWA NAMUOMBA MUDA MFUPI ULIOPITA NDIYE ATAKAYENITOA HUMU SHIMONI
NIKIWA HAI!” Tom akawaza akilia kwa uchungu.
Je, Tom atafanikiwa kutoka au atafia shimoni?
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
Beyond Love -14
Tom yupo shimoni akiwa hana uwezo wa kupumua vizuri,
anaomba sala ya ‘baba Yetu’, akiamini ingemsaidia kabla ya kifo chake. Lakini
alipomaliza sala hiyo na kuangalia dhahabu iliyokuwa kwenye mfuko wake, aliumia
sana moyo wake.
Alijipa matumaini ya kutoka, akiamini kufanikiwa kwake
kutoka kungekuwa mwisho wa maisha ya kifukara na mateso. Akamuomba Mungu kwa
mara nyingine amsaidie kutoka akiwa hai. Je, atafanikiwa? SONGA NAYO...
Maneno ya mama yake Tom
yaliwashangaza sana watu wengi waliokuwa machimboni, wengi walimpuuza!
Isingewezekana mtu kuwa shimoni kwa siku tatu halafu akawa mzima. Maneno ya
mama Tom yalikuwa sawa na usiku wa giza.
“Mh!” Mmoja aliguna.
“Vipi?”
“Huyu mama anazeeka vibaya!”
“Kweli!”
“Lakini damu nzito kuliko
maji ndugu zangu, huwezi kujua kwanini huyu mama anaamini mwanaye hajafa, maana
kama angekuwa amekufa, angeona ishara yoyote moyoni mwake,” kijana mmoja
alisema kwa sauti kubwa, mama Tom akamsikia.
“Nisikilizeni jamani, Tom
hajafa! Nina uhakika huo, moyo wangu hauniambii kabisa kwamba mwanangu
amekufa!” Mama Tom akasema huku machozi yakimtoka kwa uchungu.
“Jamani sasa tufanyeje?”
Mmoja wa vijana waliokuwa pale machimboni alisema.
“Nafikiri ni vyema kama
tukiendelea kuchimba, huenda tukampata!”
“Sawa!” Vijana wakaitikia na
kazi ya kuanza kuchimba ikaanza.
Gimonge na Mwita walikuwa
wakiongoza wenzao kuchimba pembeni ya shimo ambalo Tom alikuwepo! Walichimba
kwa muda mrefu sana bila mafanikio. Kila walipotaka kuacha, mama Tom alipiga
kelele akisema kwamba wanamuacha mwanaye afie ndani ya shimo.
“Lakini juhudi zetu mama
umeziona, Tom hawezi kuwa hai katika hili shimo! Ni maiti ngapi tumezitoa?
Shimo lenyewe linazidi kutitia, siyo rahisi Tom akawa mzima mama, amini
ninachokuambia!” Gimonge akamwambia mama Tom.
“Hapana...hapana...mimi ni
mtu mzima wanangu, ninachowaambia ni kwamba Tom hajafa na ni vyema kama
mkiendelea na juhudi za kuchimba, mwananu yupo hai ingawa atakuwa na hali mbaya
sana!”
“Kwahiyo?”
“Endeleeni kuchimba!”
“Sawa mama, hatuna budi
kukuridhisha!” Kazi ya kuendelea kuchimba ikaendelea.
Wengi wa vijana waliokuwa
wakichimba walikuwa wakifanya hivyo kwa ajili ya kumridhisha mama Tom tu,
lakini hawakuwa na matumaini ya kumtoa Tom akiwa mzima.
*******
Hewa ilizidi kumuishia Tom.
Njaa, kiu na joto vilizidi kumsumbua lakini kila alipochungulia kwenye mfuko
wake uliokuwa na dhahabu zinazong’aa alijiona ana kila sababu ya kujitahidi
sana ili aweze kutoka akiwa salama akafurahie utajiri.
Tom aliendelea kupagua
majbali pamoja na mchanga kwa mikono akielekea kutoka juu kupitia upande wa
pili wa shimo. Alijitahidi sana kutoka eneno ambalo lilikuwa likititia,
aliendelea kufanya hivyo kwa muda mrefu hadi aliposikia ardhi ikitingishika!
Alihisi kama kulikuwa na mtu
akilima au akichimba kitu chini ya ardhi aliyokuwemo. Hapo alijua huenda shimo
lilitaka kutitia tena! Akajisogeza pembeni zaidi kupisha mtetemeko na kishindo
alichokuwa akikisikia. Ghafla akashangaa kuona sululu ikitita na kutoa pembeni
ya sehemu aliyokuwemo, tobo likaonekana!
Tom hakuamini!
Alikuwa ni Gimonge, Mwita na
vijana wengine wakichimba. Tom akapata furaha ya ajabu sana. Akaaza kupumua kwa
kasi ya ajabu sana.
“...Huyu hapa!” Mwita akapaza
sauti yake.
“Nani?”
“Tom!”
Mama yake Tom aliposikia hivyo
alitamani kuamka kumfuata lakini alishindwa, aliishia kulia kwa sauti kubwa.
Tom akabebwa na kutolewa hadi juu ambapo alianza kupepewa! Wakati yote hayo
yakifanyika, hakuwa tayari kuuachia mfuko wake wa dhahabu uliokuwa mkononi
mwake. Mwita alipotaka kumsaidia, alishangaa Tom akikataa.
“Wewe umechoka sana, acha
nikusaidie!”
“Hapana, nitabeba mwenyewe!”
“Mamamaaaaaaa......” Tom
alipaza sauti baada ya kumuona mama yake akiwa amelala kwenye machela, huku
macho yake yakiwa yamejaa machozi.
“Tom mwananguuuuuuuu.....”
mama Tom naye akapaza sauti yake.
“Pole sana mwanangu!” Ilikuwa
ni mapema sana wewe kufa, napaswa mimi nitangulie kwanza, nikuache ukihangaikia
maisha yako.
“Mama Mungu amesikia kilio
chetu mama, utaishi maisha ya furaha katika kipindi chote ulichobakisha
duniani! Mama tumeuaga umasikini...” Tom akasema huku akimfungulia mama yake
ule mfuko wa slufeti uliokuwa na dhahabu!
Mama yake Tom hakuamini macho
yake, akamkumbatia mwanaye wakilia kwa furaha. Katika vitu ambavyo Tom
hakujaribu kabisa kuvifanya ni pamoja na kuuachia ule mfuko aliokuwa ameushika!
Isingekuwa rahisi kufanya jambo la hatari kiasi hicho, alikumbatiana na mama
yake, lakini mfuko wake ukiwa mkononi mwake.
Kilichofanyika baada ya hapo
ilikuwa ni Tom kuandaliwa uji mwepesi kisha akapewa akanywa na kupata nguvu,
baada ya hapo akapewa maji ya kunywa.
Hakutaka kulala kijijini
Nyamongo, baada ya kupata nguvu wakakodisha Landrover iliyowapeleka hadi mjini
ambapo Tom aliuza dhahabu kidogo, fedha aliyopata aliwagawia Mwita na Gimonge
kisha kiasi kilichobaki alikitumia kama nauli ya kwenda Nairobi kuuza madini
yake.
Alipofika Nairobi alikwenda
moja kwa moja kwa Sonara wa Kimataifa kuuza madini yake. Hakuamini macho yake
pale alipokabidhiwa kiasi cha shilingi bilioni 7 za Tanzania, Tom akashika kiasi
hicho kikubwa cha fedha akiwa na umri wa miaka 20. Kitu kilichokuwa akilini
mwake kilikuwa ni afya ya mama yake.
Mara moja akakodi ndege na
kwenda nayo hadi nyumbani kwao ambapo alimchukua mama yake na kumpeleka Nairobi
kupata matibabu. Alimpeleka katika hospitali kubwa iliyosifika Afrika Mashariki
nzima kwa kutoa tiba za uhakika ingawa walikuwa gharama za hospitali hiyo
zilikuwa kubwa sana.
Baada ya vipimo kufanyika na
mama Tom kupewa kulazwa, Tom aliitwa ofisini kwa daktari na kupewa majibu ya
vipimo vya mama yake ikiwa ni pamoja na gharama za matibabu.
“Huyu mgonjwa ni nani wako?”
“Mama yangu!”
“Mama yako?”
“Ndiyo!”
“Pole sana mwanangu!”
“Nashukuru, hivi anasumbuliwa
na nini?”
“Anasumbuliwa na uboho wa
kweye mifupa!”
“Ni nini hiyo na inakuwaje?”
“Hiyo kitalaamu tunaita Bone
Marrow, ambayo huathiri ute wa kwenye mifupa hivyo kusababisha upungufu wa
nguvu za kuzalisha chembe hai nyeupe za damu na hapo ndio chanzo cha tatizo
hilo kutokea!”
“Sasa?”
“Ni matibabu tu!”
“Atapona?”
“Ni matumaini yetu, lakini anatakiwa
kufanyiwa ukarabati katika mifupa yake, kitaalamu tunaita Bone Marrow
Transplant!”
“Naomba afanyiwe mapema
tafadhali!”
“Tatizo ni gharama yake,
sijui kama utaweza kumudu!”
“Ni kiasi gani?”
“Milioni 40 za Kenya!”
“Zitakuwa kiasi gani kwa
fedha za Tanzania?”
“Milioni 400!”
“Hakuna shida, nipo tayari
kutoa kiasi chochote kwa ajili ya mama yangu! Fedha haina thamani aliyonayo
mama yangu!” Tom alisema akionyesha huzuni sana.
“Hakuna tabu, acha tukaanze
hiyo kazi leo hii!”
“Nitashukuru sana dokta, kazi
njema!”
Matibabu ya mama Tom yalianza
mara moja, wiki mbili baadaye aliruhusiwa baada ya hali yake kutengemaa.
Alipewa dawa kwa ajili ya kutumia nyumbani. Safari hii hawakurudi kijijini
walipokuwa, badala yake walikwenda Dar es Salaam.
Tom akafungua akaunti katika
Benki ya CRDB Tawi la Lumumba na kuhifadhi fedha zake. Akaanza mipango ya
maisha yake mapya. Alinunua nyumba nyingi sana jijini Dar es Salaam na Kibaha.
Akateua nyumba moja iliyopo Mbezi Beach kwa ajili ya kuishi na mama yake.
Katika nyumba hiyo kubwa ya
kifahari, waliishi yeye, mama yake na msichana wa kazi tu! Tom akawa maarufu
Dar es Salaam nzima, akaanza kutoa misaada katika Vituo vya Watoto Yatima.
Akawa anadhamini michezo mbalimbali, jina lake likawa kubwa Dar es Salaam
nzima, jina lake likabadilika, hakuitwa Tom tena, sasa alijulikana kwa jina
jipya.
Alikuwa akiitwa Papaa Bill,
likiwa ni kifupisho cha jina Bill Gates,
bilionea wa Marekani. Jina lake likawa maarufu katika nyimbo za Dansi na Bongo
Fleva. Tom (Papaa Bill) akaanza kufanya biashara mbalimbali jijini Dar es
Salaam na Afrika Mashariki, safari za kwenda nje ya nchi zikawa haziishi. Jina
lake likazidi kuwa kubwa sana, akawa Mjasiriamali aliyealikwa kufundisha katika
vyuo, shule, makanisa na Jumuiya mbalimbali juu ya elimu ya Ujasiriamali na
jinsi alivyoweza kupata utajiri na kudumu nao. Tom akaawa Papaa Bill
kwelikweli! Utajiri wake ukaongezeka maradufu.
Jioni moja akiwa mezani
wanapata chakula cha usiku na mama yake, alimweleza juu ya mkutano aliotakiwa
kuufanya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam siku iliyofuata. Mama yake alimtia moyo
sana.
“Itakuwa saa ngapi?”
“Ni semina ya siku nzima,
nashindwa kuelewa itakuwaje, maana chuo kizima watakuwa wakinisikiliza!”
“Tatizo lipo wapi mwanangu,
mbona mara nyingi umekuwa ukienda kutoa semina kwa watu?”
“Siyo Chuo Kikuu mama, kwanza
ni wengi halafu pili ni wasomi, natakiwa kuandaa pointi za msingi sana kuweza
kuwateka watu wenye elimu kunizidi mimi!”
“Usiwe na wasiwasi mwanangu,
Mungu atakutangulia!”
“Ahsante sana mama! Nakupenda
sana!”
“Nakupenda pia Tom!”
“Siamini kama umepona mama,
lakini moyo wangu unaumi sana kula mafanikio haya bila baba. Ingekuwa furaha
sana baba naye angekuwa nasi, sijui kwanini Mungu alimchukua mapema kiasi
kile?!” Tom alisema machozi yakimlengalenga.
“...Mwanangu...Mungu hufanya
kila jambo kwa makusudi yake, amini kwamba ana sababu za kumchukua baba
yako...usijiumize mwanangu, Mungu atatutia nguvu! Hata hivyo ukianza kumlaumu
kwa kumuita utakuwa unamkufuru! Kaka ni yeye ndiye aliyemuumba, kwanini asiamue
kumchukua kwa wakati wake? Mwanangu umesahau kwamba sote tunaelekea huko huko
na siku moja tutakutana naye? Tulia mwanangu, usijali tutakutana naye siku
moja!” Mama Tom alisema kwa uchungu sana akimwangalia mwanaye.
“Sawa mama!” Tom akaitika kwa
upole, hakuweza kukaa zaidi, Tom akaingia chumbani kwake kulala na mama yake
pia.
******
Ukumbi wa Nkurumah ulikuwa umejaa wanafunzi wengi sana pamoja na
Wahadhiri wakimsikiliza kwa makini Papaa Bill (Tom) alivyoweza kupata utajiri.
Historia ya maisha yake iliwahunisha wengi.
Haikuwa rahisi watu kuamini
kwamba Papaa Bill na fedha zake aliwahi kupitia maisha ya taabu kiasi kile.
Baadhi yao hasa wanawake walishindwa kuzuia machozi yao, wakajikuta wakilia kwa
huzuni wakati wakimsikiliza Papaa Bill.
“Hata jina la Papaa Bill,
nilipewa hapa mjini baada ya kuwa maarufu na utajiri nilionao. Jina langu
halisi ni Tom!” Papaa Bill alisema watu walimsikiliza makini.
Hakuna hata mmoja aliyekuwa
akikohoa, kila alitaka kusikia kila neno lililotoka kichwani mwa Papaa Bill.
******
“Tom?!” Msichana mmoja aliyekuwa
katikati ya wanafunzi alisema kwa sauti huku akioonyesha kushtuka sana.
“Vipi?”
“Namfahamu huyu Tom!”
“Acha kujipendekeza, mara hii
unasema unamfahamu? Au kwasababu umeona ni tajiri?”
“Niache bwana, namfahamu
naamini akiniona atanikumbuka!” Msichana huyo alisema maneno hayo huku
akikazana kwenda mbele aliposimama Bill akihutubia.
Hakujali kama maneno yale
yalisikika au lah, shida yake ilikuwa kuonana na Bill. Akajipenyeza katikati ya
watu hadi akafika mbele kabisa aliposimama Bill, alishtuka sana kumuona
msichana huyo.
”Mariam?!”
“Tom?!”
“Ni wewe?”
“Ndiyo!”
“Wewe ni mtu mbaya sana!”
Je, nini kitatokea?
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
Beyond love -15
Anamwangalia kwa jicho la hasira huku kumbukumbu mbaya
zikimjia akilini mwake. Tom anamwambia Mariam ni mtu mbaya sana. Ni maneno
makali yaliyomwingia sana Mariam. Je, nini kitatokea? SONGA NAYO...
Yalikuwa maneno makali sana
yaliyomchoma moyo Mariam, hakuelewa sababu iliyomfanya Tom amwambie yeye ni mtu
mbaya! Aliamini alikuwa mtu mwema sana katika maisha ya Tom, hasa kutokana na
ukweli kwamba alishapata matatizo makubwa sana kutokana na kumsadia Tom.
Mariam akamwangalia Tom kwa
macho ya mshangao, watu wakiwa kimya kuangalia kilichotokea, kuna waliochukizwa
na kitendo cha Mariam kwenda mbele kwani kiliharibu mtiririko mzima wa semina.
“Tom, mimi ni mtu mbaya?”
“Yeah! Wewe ni mtu mbaya sana
katika maisha yangu! Naona sasa umeona thamani yangu baada ya kusikia nimekuwa
tajiri! Unajua baadhi ya watu wenye uwezo huwa mnajisahau sana, mnaona kama
utajiri ni kwa ajili yenu na maisha ya shida ni ya watu wa chini siku zote!
“Mungu huyo huyo aliyewapa
ninyi utajiri, ambao ulininyanyasa na kutoa thamani ya utu wangu, ndiye
aliyenibariki na hivi sasa nina fedha!” Tom alisema kwa uchungu sana.
“Usiseme hivyo Tom!”
“Kumbe nisemeje?”
“Hujui yaliyotokea, nina
habari mbaya sana!”
“Sawa...niache kwanza
nimalize semina, hayo mambo mengine yafuate baadaye!”
“Sawa!” Mariam akaitika kwa
shingo upande, huku machozi yakimtoka machoni mwake.
Akaondoka na kwenda kukaa
mahali alipokuwa mwanzoni. Furaha yake ikatoweka kabisa, hakuwa na amani tena,
shida yake ilikuwa kuhakikishiwa kuwa na mwanaume aliyempenda, Tom!
Hakuna aliyekuwa akifahamu
kilichokuwa kikiendelea, ilikuwa ni siri ya Tom na Mariam peke yao, wao ndiyo
waliojua kilichokuwa kikiendelea. Semina ikaendelea ambapo Tom alieleza siri ya
mafanikio ya utajiri wake na jinsi anavyoweza kutunza fedha na kuendelea kuwa
tajiri.
“Tatizo siyo kupata fedha,
kikubwa ni jinsi gani ambavyo unatumia fedha zako! Labda niwaeleze jambo moja,
baada ya kupata kiasi kikubwa cha fedha ni rahisi sana fedha hizo kupuputika
kwa matumizi ambayo siyo ya lazima.
“Hata ukiwa na fedha nyingi
kiasi gani? Kama hutatulia na kupanga mikakati, basi lazima mwisho wa siku
utalia. Jambo la kwanza kabisa katika safari ya kuelekea kwenye mafanikio ni
nidhamu ya fedha!
“Lazima fedha iheshimiwe,
usiamini una fedha nyingi sana kiasi cha kuanza matumizi ambayo siyo ya lazima.
Nidhamu ya fedha inaanzia unapokuwa na kiasi kidogo kwanza, matumizi yako
yapoje?
“Hupaswi kuidharau shilingi
mia, maana ni mwanzo wa kuelekea kwenye elfu moja. Anza sasa kuwa na nidhamu ya
fedha, utaona faida yake. Jambo lingine ni kuweka mikakati ya nini ufanye huku
utafiti ukiwa silaha ya kila jambo linalohitaji fedha kabla ya kulifanya.
“Fanya utafiti wako kwanza,
ni kweli ukitoa fedha zako hazitapotea? Ni kweli ni biashara nzuri inayolipa?
Unaweza kufanya utafiti kwa wengine ambao wamewahi au wanafanya biashara ambayo
inafanana na hiyo unayotarajia kuifanya kabla ya kuingia kwenye biashara
husika.
“Tunza fedha, nenda kwa
mahesabu, kila kitu kifanyike kwa rekodi, utaona mafanikio yake. Ndugu zangu,
kama nilivyotangulia kusema awali kwamba, kupata fedha au utajiri siyo jambo
gumu sana, lakini kinachowashinda wengi ni jinsi gani ya kuweza kudumu na huo
utajiri bila kutetereka. Kwangu mimi naamini tunaweza na si imani yangu kwamba
kuna mmoja kati yenu atashindwa kuwa na nidhamu ya fedha ili mwisho wa siku
aweze kupata utajiri!” Tom alisema akishangiliwa.
Watu walikuwa makini sana
kumsikiliza kwa kila alichokuwa akiongea, kwa wanafunzi pamoja na Wahadhiri wa
Chuo Kikuu, ilikuwa faraja kubwa sana kwao kupata semina elekezi juu ya kufikia
mafanikio.
Tom alikuwa na fedha nyingi
sana, alikuwa tajiri mwenye uwezo mkubwa wa fedha na mwenye mali zinazoendelea
kuzaliana. Ukiachana na maduka mbalimbali aliyokuwa amefungua jijini Dar es
Salaam, Arusha, Mbeya, Tanga, Moshi, Mwanza na Dodoma alikuwa akimiliki kampuni
ya kuuza na kununua madini mbalimbali iliyoitwa Tom Minerals Ltd iliyokuwa eneo
la Posta jijini Dar es Salaam.
Alimjengea mama yake nyumba
ya kifahari Musoma ambapo alimwekea mifugo na maduka ambayo aliyasimamia. Maisha
ya kubahatisha yakawa yamefutika kabisa, mama yake Tom akaishi maisha ya
kitajiri yaliyojaa furaha na amani.
Tom alikuwa akilipwa kiasi
cha shilingi milioni 10 kwa saa kila anaposimama kutoa semina na ushuhuda wa
maisha yake. Kila siku alikuwa akiendelea kukua na kukua!
Baada ya kumaliza semina, Tom
akiongozwa na wapambe wake, walitoka wakiliendea gari lake. Mariam alikuwa
akimfuata na kumuita jina lake lakini Tom hakugeuka. Alipolifikia gari lake,
akafunguliwa mlango na kuingia.
Mariam akaendelea kulia
akiomba asikilizwe, hata hivyo maneno yale Tom hakuyasikia kwakuwa alifunga
vioo vyote. Mariam alipozidi kulia, Tom akafungua dirisha moja na kumwangalia
kwa jicho la huruma.
“Hebu mwacheni, mruhusuni
aje!” Tom akasema, wapambe wake hawakuwa na kipingamizi tena, wakamruhusu Mariam ambaye alisogelea gari la Tom akizidi
kulia.
“Mfungulieni mlango!” Tom
akaagiza.
Mlango ukafunguliwa, Mariam
akaingia ndani ya gari, mlango ukafungwa na vioo vikapandishwa. Tom akawasha
kiyoyozi kisha akafungulia redio yake kwa sauti ya chini sana.
“Nini kipya unataka kunieleza
Mariam? Nimeshakuambia wewe ni mtu mbaya
sana katika maisha yangu, sioni kama kuna sababu ya kuendelea kusumbuana.
Haiwezekani kipindi nikiwa na matatizo unikatae halafu sasa hivi nina mafanikio
ndiyo unajifanya unanililia. Huo naufananisha na unafiki! Acha unafiki Mariam!”
Tom akasema kwa hasira ya wazi akimtizama Mariam machoni.
“Hapana Tom, nakupenda sana
Tom wangu, Mungu ndiye shahidi wa ninac hokiongea. Nilitaka kupoteza maisha
yangu kwasababu yako! Hujui kilichotokea!”
“Kwani ulipatwa na nini?”
“Siku ile wakati narudi
kutoka hospitalini, nilipata ajali mbaya ya gari, nikakimbizwa hospitalini na
kulazwa. Nilikuwa na hali mbaya sana maana nilipoteza kabisa fahamu kwa miaka
mitano!
“Nililala kitandani kwa muda
wote huo nikiwa sijui kinachoendelea, ni kama nilikuwa nimekufa! Nilipata
majereha makubwa sana katika ubongo wangu hivyo kushindwa kupata fahamu katika
kipindi chote hicho. Niliteseka sana, lakini nilipopata fahamu na hali yangu
kurejea kawaida ndipo nikarudi tena hapa chuo, ndiyo maana unaniona nina umri
mkubwa zaidi kuliko wanafunzi wengine!” Mariam alisema huku machozi
yakitiririka machoni mwake kwa kasi sana.
“Pole sana Mariam, nakupenda
sana Mariam!”
“Hata mimi Tom, sijaona
mwanaume mwingine zaidi yako, sikuambii haya kwasababu ya utajiri ulionao sasa,
kumbuka hata kipindi ulipokuwa huna kitu nilikuwa nakupenda kwa mapenzi haya
haya ninayokupenda leo!
“Nirudishe moyoni mwako
tafadhali, nipe nafasi nyingine Tom, naamini kwa kuwa na wewe maisha yangu yatakuwa ya furaha tena baada ya
kuishi bila kuwa na furaha kwa miaka mingi sasa!” Mariam akamwambia Tom.
“Lakini umeshachelewa!”
“Kivipi?”
“Subiri!”
Tom akatoa simu yake mfukoni
kisha akabonyeza namba fulani, akaanza kuzungumza na mtu. Dakika moja baadaye,
msichana mrembo sana mwenye sifa zote za kuitwa mrembo akaingia kwenye gari ya
Tom. Alikuwa mrefu, mwenye hips pana, makalio makubwa yaliyobebwa na kiuno
chembamba sana.
Msichana huyo alikuwa amevaa
suruali nyepesi nyeusi, blauzi ya pink pamoja na viatu vya wazi vyenye rangi ya
pinki. Macho yake yalifunikwa kwa miwani kubwa ya giza! Alikuwa na midomo
minene, iliyopambwa na mafuta maalum ya kupambia midomo, nyusi zilizochongwa
kwa ustadi wa hali ya juu zilizochorwa kwa wanja mweusi zilizidisha uzuri wake.
Alikuwa msichana mrembo
kwelikweli, manukato yake yalikaribia kupasua pua za Mariam! Yalikuwa manukato
ya bei mbaya yenye harufu nzuri kuliko kawaida. Alipofika aliketi na kumtizama
Mariam kwa dharau.
“Unasemaje Tom?” Msichana
huyo akasema akionekana kuchukizwa na Mariam kuingia kwenye gari la Tom.
“Nataka kukutambulisha!”
“Sawa...”
“Mariam huyu ni mchumba wangu
mpenzi ninayempenda sana, anaitwa Juliana. Ndiye mwanamke niliyenaye kwasasa
ambaye kwakweli nampenda sana. Tupo mbioni kufunga ndoa ili tuishi kama mke na
mume!” Tom akamwambia Mariam. Alipomaliza akamgeukia Juliana.
“Juliana, huyu anaitwa
Mariam, alikuwa mpenzi wangu wa zamani kabla sijakutana na wewe!”
“Mh! Kumbe ulikuwa na
mwanamke mbaya hivi? Ulifikiria nini lakini kuwa na uhusiano naye? Huyu ni kama
alikuwa anakusababishia nuksi tu, katika maisha yako? Huyu ni takataka tu,
hastahili kabisa kuwa na wewe!” Juliana akasema huku akifungua mlango tayari
kwa kurudi kwenye gari lake.
“Tom mimi mbaya, takataka?
Ndiyo umeamua kumuita mwanamke wako ili anitukane? Sawa bwana, Mungu yupo!”
Mariam akasema akilia sana.
Muda huo huo akashuka kwenye
gari na kukimbia akielekea mtoni. Hakuna aliyejua alichokifuata.
Je, nini kitatokea? Mariam
amefuata nini mtoni?
Beyond Love -16
Huyu alikuwa msichana mzuri aliyefikia kilele cha urembo
lakini tatizo alikuwa mwenye dharau sana. Alimtizama Mariam kuanzia juu hadi
chini kisha akamgeukia Tom na kumwambia; “Mh! Kumbe ulikuwa na mwanamke mbaya hivi? Ulifikiria
nini lakini kuwa na uhusiano naye? Huyu ni kama alikuwa anakusababishia nuksi
tu, katika maisha yako? Huyu ni takataka tu, hastahili kabisa kuwa na wewe!”
Mariam aliumizwa sana na maneno yale.
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO....
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
Maneno yale kutoka kwa
Juliana yalikuwa sumu kali kwa Mariam, kwanza alijiangalia kuanzia chini hadi
juu, kisha akamwangalia na Juliana baadaye akayarudisha macho yake kwa Tom,
hakuamini alichosikia, aliona kama alikuwa katikati ya ndoto kali na huenda
muda wowote angezinduka.
Alishuka haraka sana
kwenye gari kisha akapiga hatua za haraka akielekea katika mto uliokuwa chini
ya Jengo la Utawala. Kila mtu alimshangaa, alionekana kama mwendawazimu.
Kilichokuwa kikimuuma
zaidi ni kitendo cha kumsaidia Tom kwa moyo wake, tena wakati akirudi kutoka
kumpeleka baba yake na Tom hospitalini akapata ajali ambayo ilimlaza kitandani
kwa miaka kadhaa.
Hakuona thamani yake
tena, kila kitu alikiona kichungu, hakuwa na hamu ya kuendelea kuishi duniani.
Alipofika mtoni alikaa chini akiwaza jinsi gani atakavyoweza kumaliza hasira
zake, haikuwa rahisi kupata jibu la haraka. Tom alikuwa amempa kovu ambalo
lisingepona kabisa.
“Nimemkosea nini mimi
jamani, kosa langu ni nini? Kwanini ananinyanyasa kiasi hiki? Kwanini
ananikosesha amani kiasi hiki? Amenionaje kwanza, yaani napoteza kabisa
mwelekeo wa maisha yangu!” Mariam akawaza.
Aliendelea kulia akiwa
hajui la kufanya, maisha yake sasa yalishakuwa machungu. Lakini baada ya kuwaza
muda mrefu, akapata jibu; jibu lenyewe lilikuwa baya sana. Aliwaza kujiua!
“Ndiyo lazima
nife...sioni sababu ya kuendelea kuishi katika dunia yenye tabu kiasi hiki,
dunia yenye watu wenye roho mbaya ambao hawataki kuangalia thamani ya maisha ya
wenzao, bora nife!” Mariam aliwaza akifikiria njia nzuri ya kujitoa uhai bila
maumivu.
“Watu wanaojinyonga
mara nyingi hutamani kukata kamba, lazima nifikirie njia nzuri ambayo
haitaniumiza, lazima niondoke duniani kimya kimya, tena bila maumivu makali.
Nataka kufa taratibu...ndiyo bora nife, hakuna sababu ya kuendelea kuishi
nikiteseka!” Aliwaza Mariam.
Alidhamiria kufa,
lakini hakutaka kusikia maumivu wakati roho yake ikitengana na mwili, lakini
alikuwa akiwaza sana njia ya kujiua! Ni njia gani hiyo? Hakuwa na majibu,
lakini ilikuwa lazima ipatikane.
* * * * *
Watu walikuwa
wamezunguka gari la Tom wakisikiliza mzozo uliokuwa ukiendelea kati yake na
Juliana, tayari Juliana alishaanza kuleta fujo baada ya kumuona Mariam,
alilalamika kwamba eti alikuwa akidhalilishwa!
“Nimekwambia ni
msichana wangu wa zamani, kwani kuna tatizo gani?”
“Wewe huoni tatizo?”
“Lipi? Sioni tatizo
mimi!”
“Sasa sikiliza, wakati
mwingine sipendi na sitaki unifanyie ujinga kama wa leo, tafadhali sana Tom, na
kama hunitaki ni bora ukaniambia ukweli ili nijue moja!”
“Usiseme hivyo mpenzi
wangu!”
“Kumbe nisemeje?”
“Sikiliza tuachana na
haya mambo, tunaonyesha picha mbaya, nenda kwenye gari lako tuondoke!”
“Siendi kabla haya
mambo hayajaisha!”
“Unataka yaisheje?”
“Kwani wewe
unafikiriaje?”
“Basi twende
tutazungumza nyumbani!”
“Sawa!” Juliana
akajibu kwa hasira kisha akatoka na kwenda kwenye gari lake.
Kila jicho la watu
waliokuwepo mahali pale lilikuwa likimwangalia Juliana. Alikuwa mwanamke mzuri
sana kwa mwanaume yeyote rijali. Alikuwa mrefu, mwenye hips pana, makalio ya
kumtosha na mwendo wake ulizidi kuwakosha raha wanaume.
“Mh! Huyu msichana
mzuri sana jamani!” Mmoja wa watu waliomuona akipita alisema.
“Ni kweli kaka! Kweli
pesa ni kila kitu, yaani ukiwa na pesa unaweza kuwa na mwanamke yeyote
umtakaye!”
“Hivi umemuona vizuri
usoni?”
“Ndiyo, ana macho mazuri
ajabu, halafu anajua kuyatumia! Hakyanani huyu nikimpata chumbani, hakuna
kulala yaani usiku mzima ni kupeana maraha tu!”
“Mh! Mshkaji sasa wewe
umefika mbali!”
“Hakuna umbali wowote,
ni mambo ya kawaida sana kwa mwanaume yeyote mwenye viungo vyote vizima
mwilini!”
“Umeshinda kaka!” Hayo
yalikuwa mazungumzo ya vijana wawili waliokuwa wakimtizama Juliana aliyekuwa
akitembea kwa maringo akielea gari lililokuwa limeegeshwa karibu na la Tom.
Alipolifikia akafungua
mlango na kuingia, Tom akafunga mlango wa gari, kisha akamwambia dereva aondoe
gari! Tom akaondoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
******
Utajiri wa Tom ukawa
gumzo kwa wanafunzi wa chuo, stori zote siku hiyo zilikuwa zikimhusu Tom! Kila
mtu alikuwa akimmiminia sifa kutokana na uwezo mkubwa kifedha aliokuwa nao. Tom
alikuwa mfano wa kuigwa.
“Lakini ana maendeleo
sana!” Mmoja wa wasichana waliokuwa wakijadiliana kuhusu Tom alisema.
“Sana, halafu ana
mwanamke mzuri sana!”
“Yaani acha tu, yaani
ndiyo upate bahati ya kuwa na boyfriend kama yeye mh! Yaani mji mbona
ungechimbika?”
“Lakini hapana bwana,
watu wenye fedha wana matatizo yao bwana, waone hivyo hivyo!”
“Matatizo gani?”
“Kufungua zipu!”
“Tena ni viboko ile
mbaya!”
“Ukiamua kuwa naye,
lazima ukubali kuteswa, kutukanwa na kuchangia na wengine, lakini ukiwa na yale
mambo ya kupenda umependa utake kuwa mwenyewe, thubutu haiwezi kutokea! Wanaume
wenye pesa zao tabu tupu, asikudanganye mtu!” Walizungumza kwa muda mrefu sana
wasichana hao, lakini baadaye mmojawao akamkumbuka Mariam.
“Halafu nilimuona kama
Mariam akimfuata mbele wakati jamaa akitoa mada!”
“Eti alikuwa
anamwambia anamkumbuka!”
“Mh! Mie sikuona
jamani, ikawaje?”
“Jamaa akamtolea nje!”
“Si nilisikia baadaye
alipotoka nje alimfuata tena?”
“Enhee! Lakini
yaliyomkuta huko balaa!”
“Ilikuwaje?”
“Alimfuata jamaa,
akamfungulia mlango, baadaye Tom akamuita mwanamke wake! Mzuri huyo asikuambie
mtu. Basi bwana, sijui walikuwa wakizungumza nini, nikashangaa Mariam akitoka
kwa hasira na kuondoka zake!” Lilian, mmoja wa wasichana hao alisema.
“Akaenda wapi?” Pamela
akauliza.
“Kakimbilia huko
chini!”
“Wapi?”
“Mtoni!”
“Alikuwa katika hali
gani?”
“Kama amekasirika
hivi, maana inaonekana aliambia kitu kilichomuuza sana!”
“Mungu wangu!”
“Mbona umeshtuka?”
“Yaani mnaona ni jambo
dogo hilo, tunaweza kumpoteza mwenzetu kwa mzaha hivi hivi!” Pamela akasema
huku akikimbia.
Wenzake nao walimfuata
wakikimbia hadi mtoni. Baada ya kutafuta kwa muda, walifanikiwa kumuona Mariam
akiwa amelala chini akilia. Wakati mwingine alikuwa akjipigiza chini kwa
hasira.
“Mariam vipi?” Pamela
akamuuliza.
“Niache rafiki yangu!”
“Kwanini nikuache,
niambie kuna nini?”
“Nina matatizo makubwa
sana!”
“Matatizo gani tena?”
“Si unakumbuka
niliwahi kukusimulia kuhusu maisha yangu?”
“Nakumbuka sana!”
“Unakumbuka kwamba
nililala kuitandani kwa zaidi ya miaka minne nikiwa nimepoteza fahamu!”
“Nakumbuka!”
“Sijui kama unakumbuka
sababu iliyonisababuishia matatizo yote hayo!”
“Ulisema...nakumbuka
Mariam!”
“Ilikuwa ni nini?”
“Mapenzi...” Pamela
akasema kwa sauti ya taratibu sana.
“Mwanaume mwenyewe ni
Tom!”
“Tom?!”
“Ndiyo! Tom ndiyo
chanzo cha matatizo yote hayo, lakini leo hii naambulia matusi!”
“Tom amekutukana?”
“Siyo yeye!”
“Sasa mbona umesema ni
Tom?”
“Ni Juliana!”
“Juliana ndiyo nani?”
“Mwanamke wake, yule
aliyekuja naye!”
“Mbona siamini kama
anaweza kukutukana? Amekuambiaje?”
“Eti mimi mbaya, sina
hadhi ya kuwa na Tom, yaani mimi mbaya...mimi mbaya? Sina hadhi ya kuwa na Tom?
Siamini macho yangu, siamini kabisa, naona ni bora nife!” Mariam alipomaliza
kusema maneno hayo akaanguka chini kama mzigo!
Akapoteza fahamu.
Wakajaribu kumtingisha lakini hakushtuka, macho yake yakaanza kulegea pole pole
kisha akayafumba kabisa, ute mwepesi ukaanza kumtoka kinywani mwake, shingo
yake ikalegea kabisa. Mariam hakujigusa tena.
Wakapiga kelele za
kuomba msaada.
Je,nini kitatokea? Mariam amekufa? Mapenzi ya Tom na
Juliana yatafikia wapi? Vipi kuhusu mama yake Tom huko kijijijini?
Beyond Love- 17
Kitendo cha mwanamke wa Tom,
Juliana kumtukana Mariam, kilimuumiza sana! Alijikuta akijiona hana thamani
tena, hakuyatamani maisha. Akatoka mbio akielekea mtoni chini ya daraja ambapo
alianza kuwaza huku akilia machozi.
Baadaye Pamela na wenzake
wanamfuata mtoni alipokuwa amekimbilia ambapo wanamkuta akiwa katika hali mbaya
sana akilia kwa uchungu. Baadaye Mariam alilegea na kuanza kutokwa na mapovu
mdomoni kabla ya kupoteza fahamu.
Je, nini kitatokea? SONGA
NAYO...
Dakika kumi tu baadaye tayari
watu walikuwa wameshajaa katika eneo lile. Hawakuwa na sababu ya kuuliza
kilichotokea kwani hali aliyokuwa nayo Mariam pale chini iliwahuzunisha sana,
mara moja akabebwa juu juu na kupelekwa eneo la Utawala.
“Nini kimetokea?” Mmoja wa
wanafunzi aliuliza.
“Hayo siyo maswali
kinachotakiwa sasa hivi ni kumuwahisha hospitali kwanza!”
“Lakini ni vizuri
tukafahamu!”
“Ndiyo maana nimesema
tumpeleke kwanza hospitali!” Pamela akaendelea kusisitiza.
Pamela na wenzake wakaongoza
moja kwa moja hadi ofisini kwa Mkuu wa
Chuo ambapo alitoa taarifa na gari
likatolewa mara moja. Muda mfupi baadaye safari ya kwenda Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili ikaanza. Hawakuchukua muda mrefu sana kufika hospitalini hapo
wakitumia Barabara ya Sam Nujoma baadaye Ali Hassan Mwinyi kisha walipofika
eneo la Daraja la Salender wakakata kulia wakielekea Hospitali ya Muhimbili.
Hawakuwa na sababu ya kukaa
mapokezi, moja kwa moja aliweka juu ya
machela na kusukumwa kuelekea wodini.
“Nini kimempata?” Mmoja wa
wauguzi aliuliza.
“Alianguka!”
“Kwanini?”
“Alipatwa na mshtuko!”
“Wa?”
“Ni mambo ya uhusiano!”
“Kawaida ya wasichana!”
“Naomba utusaidie apone!”
“Usijali hii ndio kazi yetu,
mmesema mnatokea wapi?’
“Chuo Kikuu!”
“Tulisikia Papaa Bill alikuwa
anatoa semina ya Ujasiriamali pale!”
“Ndiyo, tena yeye ndiye amesababisha yote haya!”
“Kivipi?”
“Aliwahi kuwa mpenzi wa
Mariam!”
“Mungu wangu!”
“Kwa hiyo alivyokuja pale
alikuja na mwanamke mwingine anayeitwa Juliana. Hata hivyo Mariam alivyomfuata
alimtambulisha kwamba ana mpenzi mwingine, mbaya zaidi Juliana alimtukana
Mariam hiyo ndiyo sababu iliyosababisha matatizo yote haya!”
“Poleni sana, kwani Papaa
Bill alikuwa hajui kwamba Mariam alikuwepo chuoni?”
“Alikuwa hajui!”
“Mbona sielewi kivipi?”
“Walipotezana muda mrefu sana
na hata hivyo Papaa Bill alivyokuja Mariam hakujua kama ndiye mpenzi wake wa
zamani!”
“Kwanini asijue?”
“Papaa Bill siyo jina lake
halisi!”
“Kumbe anaitwa nani?”
“Tom!”
“Ok nimeanza kuelewa, tupeni
nafasi kidogo tufanye kazi yetu!”
Pamela na wenzake wakatoka
nje na kuwaachia wauguzi waendelee na kazi ya kumpatia matibabu Mariam. Jopo la
madaktari watatu walikuwa bize kuhakikisha hali ya Mariam inakuwa nzuri. Kazi ya kupandisha mapigo yake ya moyo ilianza mara moja na matumaini yakaanza
kuonekana.
Baadaye Muuguzi aliyekuwa
akizungumza na akina Pamela alitoka nje
uso wake ukionyesha alikuwa na jambo la kuzungumza nao. Macho yake yalionyesha
wasiwasi mwingi jambo ambalo liliwazidishia hofu Pamela na wanafunzi wengine
waliokuwepo.
“Muuguzi nini kinaendelea
huko ndani?” Pamela alikuwa wa kwanza kuuliza.
“Punguzeni hofu, Mariam anaendelea
vizuri!”
“Ameamka?”
“Bado lakini hali si mbaya!”
“Ahsante Mungu!”
“Mnaweza kwenda na kurejea kesho asubuhi!”
“Ahsante sana na Mungu
akubariki!”
“Nanyi pia!”
****
Majina ya Tom na Mariam
yalikuwa gumzo chuo kizima, kila kona
walikuwa wakizungumziwa wao, hakuna hata
mmoja aliyeelewa siri iliyokuwepo kati yao. Wengi walimwonea huruma sana Mariam
lakini kuna ambao walimwona kama mtumwa wa mapenzi anayemng’ang’ania Tom kwa
sababu ya fedha alizokuwa nazo.
Kilichokuwa nyuma ya pazia
hakuna aliyekifahamu kwani ilikuwa ni siri kubwa iliyojificha katikati ya moyo
wa Mariam ambaye alimweleza siri hiyo rafiki yake pekee Pamela.
“Hivi anaendeleaje Mariam?”
“Hajambo!”
“Ametoka?”
“Bado ila ameshapata fahamu!”
“Mh!”
“Mbona unaguna?”
“Sababu iliyompeleka
hospitali!”
“Sasa hiyo ni ya kuuliza?’
“Ndiyo kila mtu anajua
alianguka lakini sababu ya kuanguka kwake ndiyo inayonitatiza!”
“Si mapenzi?” Mwingine
akadakia.
“Ishu sio mapenzi bali ni
nani anayempenda!”
“Jamani huyu naye si Papaa
Bill!”
“Sasa haoni kama hawaendani
naye?”
“Msiingilie mambo ya watu
hivi mnajua nguvu ya mapenzi ninyi?” Pamela aliuliza kwa ukali.
“Rafiki yako naye amezidi
kujipendekeza kwa watu wenye fedha zao,
halafu anajifanya mgumu utafikiri binti mlokole, hajawahi kusimama na
mwanaume hata siku moja lakini hii inashangaza mpaka akazimia?”
“Ndiyo maana nasema hamfahamu
kitu kinachoendelea hivyo kaeni kimya!”
“Sasa kama unajua si utuambie?”
“Ya ngoswe muachie ngoswe
mwenyewe mmekuja kusoma au kujua ya watu?”
“Mh! Na wewe una
majibu...shauri yako wewe mwendekeze tu huyo shoga yako!”
“Fyuuuu bakini na umbea wenu!” Pamela akasema huku akisonya
na kuondoka zake.
***
Siku tatu baadaye Muuguzi
aliyekuwa akipita raundi ya asubuhi
alishangazwa na hali ya Mariam ambaye alikuwa ameanza kufumbua macho na kupepesa
huku na kule. Mara moja muuguzi akasogea
katika kitanda cha Mariam kisha akaketi.
“Pole!”
“Ahsante!”
“Unajisikiaje sasa?”
“Sijambo, kwani hapa ni
wapi?”
“Hospitali!”
“Hospitali?”
“Ndiyo!”
“Nililetwa hapa kufanya
nini?”
“Uliletwa hapa ukiwa
hujitambui umepoteza fahamu!”
“Mungu wangu!” Akili ya
Mariam ikafanya kazi kwa haraka. Akavuta kumbukumbu tataribu.
Nataka kwenda kwa Tom...
Napanda kwenye gari lake...
Namkumbusha mimi ni nani...
Ananiambia ana mchumba...
Baadaye anamwita...
Ni mwanamke mrembo sana...
Anaonekana ana dharau...
Anavuta midomo yake...
Ananiambia mimi ni mwanamke
mbaya...
Mimi mbaya?...
Nakimbilia chini ya daraja,
nalia...
Pamela
“No! Haiwezekani Tom kwanini
unanitesa kiasi hiki Tom? Mimi ni mwanamke mbaya kiasi hicho? Nimelala hospitali
kwa miaka mitano kwa sababu ya kukuokoa uhai wa baba yako lakini haukujali yote
hayo unaniletea mwanamke anitusi. Tom! Kwanini mimi?” Pale pale Mariam alianza
kulia baada ya kukumbuka picha nzima ya tukio lote lilivyokuwa.
“Pole sana binti haya ndiyo
maisha!”
“Lakini inaniuma sana!”
“Najua lakini usijali, Mungu
atakupa mwanaume mwingine!”
“Dada, si kama Tom wangu
niliyempenda na kujitoa kwake!”
“Jitahidi tu!”
“Siwezi, siwezi nimekaa miaka yote hiyo nikimsubiri
yeye, sikujua alipoelekea sasa amerudi namhitaji!”
“Mariam!”
“Bee!”
“Wewe hivi sasa ni mgonjwa
unahitaji kutulia na kufikiria afya yako kwanza!”
“Najua, lakini inaniuma
sana!”
“Pole sana!”
“Ahsante!” Muda huo huo
Pamela akaingia akiwa na maua mkononi mwake.
“Mariam umezinduka?” Pamela
aliuliza kwa mshangao.
“Ndiyo namshukuru Mungu!”
“Pole, unaendeleaje sasa?”
“Nasikia vizuri!”
“Utapona usijali!”
Walizungumza mambo mengi na Mariam kuhusu tukio zima lilivyokuwa na
jinsi wanafunzi wanavyomchukulia. Pamela alitumia muda mwingi sana kumshauri na
kumfanya ajisikie kawaida. Ilikuwa kazi
ngumu lakini aliimudu ipasavyo.
Wiki moja baadaye ikiwa ni baada ya Mariam kupata Ushauri Nasaha
kwa madaktari hali yake ilirejea vizuri
na alikuwa tayari kuishi bila Tom.
Akarejea chuoni na kuendelea na masomo kama kawaida.
***
Mapenzi ya Tom na Juliana
yalipamba moto huku mipango ya ndoa ikiwa katika hatua za mwisho kabisa. Tayari
ndoa yao ilishaandikishwa Kanisani na ilitarajiwa kufungwa wiki moja baadaye.
Tom akapata safari ya ghafla kikazi ya kwenda Arusha. Alishindwa ni jinsi gani
angemweleza Juliana akamwelewa juu ya safari hiyo lakini ilikuwa ni lazima
amweleze.
Alichokifanya ni kuwahi
nyumbani kisha akaoga pamoja na mpenzi wake baadaye wakaungana pamoja mezani
kwa chakula cha usiku. Tom aliona hiyo ndiyo ilikuwa nafasi pekee ya kumweleza
mchumba wake juu ya safari iliyokuwa mbele yake. Hata hivyo alisita.
“Darling inaonekana kuna kitu kinakutatiza leo!”
“Ahaaa, hapana usijali mpenzi
nipo sawa tu!”
“Nakujua vizuri sana mpenzi
wangu si kawaida yako kuwa hivyo!”
“Ni kweli mpenzi lakini
nafikiria ni namna gani utakavypokea ujumbe ninaotaka kukueleza!”
“Ni ujumbe gani, hata kama ni
mbaya nieleze tu!”
“Nimepata safari ya ghafla ya
kwenda Arusha kesho mchana!”
“Kuna nini tena?”
“Akina Jamali wameniita, kuna
tatizo kidogo kule kwenye ofisi yangu ya kule sina budi kwenda ili nikalitatue,
hata hivyo kesho kutwa tu nitakuwa hapa!”
“Mh! Darling nitabaki na
nani? Kumbuka zimebaki siku chache tu
kabla ya ndoa yetu!”
“Sasa?”
“Siyo vizuri kusafiri!”
“Hizo ni imani tu, ondoa
shaka mpenzi wangu wewe umeshakuwa wangu tayari!”
“Sawa, lakini usizidishe
kesho kutwa!”
“Usijali”
Siku iliyofuata Tom alijiandaa kwa safari ya
kwenda Arusha na baadaye akiwa safarini kuelekea Uwanja wa Ndege akapigiwa simu
na kufahamishwa kwamba tatizo lilishatatuliwa,
kwa maana hiyo hakuhitajika tena kwenda huko. Tom alifurahi lakini
aliamua kumshtukiza mkewe.
Akaondoka na kwenda kwa marafiki zake Msasani, alikaa huko mpaka saa tano za usiku ndipo
aliporejea nyumbani. Baada ya mlinzi kumfungulia aliegesha gari mahali pazuri
kisha akafungua mlango mkubwa na kwenda moja kwa moja chumbani kwake. Macho
yake hayakutaka kumeza yalichokiona mbele yake.
Juliana alikuwa na mwanaume
kitandani, tena rafiki mkubwa wa Tom aliyeitwa Joseph. Tom aliyatoa macho bila kuamini
alichokiona, akafikiria siku ya ndoa yake, akafikiria jinsi alivyoalika wageni wengi, akawaza juu
ya gharama alizozitumia kuandaa sherehe hiyo,
akachanganyikiwa.
“Juliana...Joseph, mnanifanyia hivi?” Tom alisema maneno hayo
akitetemeka. Ghafla akaanguka chini kama mzigo, puuu!
Picha ya Mariam ikamjia
kichwani mwake. Akapoteza fahamu.
Je, nini kitaendelea?
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
Beyond Love- 18
Wiki moja kabla ya Tom kufunga ndoa na Juliana, Tom
anamfumania Juliana akifanya mapenzi na rafiki yake wa karibu aitwaye Joseph.
Tom haamini kilichotokea, anajikuta akianguka chini na kupoteza fahamu. Je,
nini kitaendelea? SONGA NAYO...
Kilikuwa chumba kizuri kuliko
kawaida, dari lilikuwa limepigwa rangi nyeupe, chini kukiwa na zulia la manyoya
laini lenye rangi nyeupe, ukuta ulikuwa umepigwa rangi nyeupe, mashuka nayo
yalikuwa meupe kabisa huku feni iliyokuwa juu ikisambaza hewa nzuri chumbani
mle ikiwa nyeupe!
Kila kitu kilikuwa cheupe!
Macho yake yalikuwa yakizunguka kila kona ndani ya chumba hicho bila kujua
alikuwa mahali gani, baadaye akataka kuamka, lakini akashindwa! Alishindwa
kwasababu alihisi maumivu katika mkono wake wa kuume, ni hapo alipogundua
kwamba mkono wake ulikuwa umetobolewa na dawa iliyokuwa ikitokea kwenye drip
ilikuwa ikiingia katika mishipa yake ya damu!
Huyu ni Tom au Papaa Bill
kama alivyojulikana na wengi, hapo akili yake ikafanya kazi ipasavyo. Akagundua
kwamba alikuwa hospitalini! Anaumwa nini? Ni swali ambalo alijiuliza bila
kupata jibu sahihi. Baadaye alipogeuza uso wake akamuona Muuguzi akiwa
amesimama mbele yake. Akatabasamu.
“Pole sana kaka!”
“Ahsante sana!”
“Unajisikiaje sasa?”
“Vizuri, kuna nini?”
“Unaumwa!”
“Na nini?”
“Huwezi kukumbuka, ulipoteza
fahamu!”
“Hapa ni hospitali gani?”
“Ocean Road!”
“Umesema Ocean Road?”
“Ndiyo!”
“Nani alinileta?”
“Juliana!”
“Nani?”
“Juliana!”
“Umesema Juliana?”
“Ndiyo!”
Hapo picha nzima ikamjia,
akakumbuka tukio zima la fumanizi kati ya Juliana na Joseph, moyo wake ulisononeka
sana. Machozi yakaanza kutiririka machoni mwake kama maji yatiririkavyo katika
kijito kilichopo mlimani. Moyo wake ulipata majeraha makubwa sana, hakuwa
tayari kupata maumivu makali kiasi kile, akamchukia sana Juliana.
“Kwani vipi kaka?”
“Dada dunia hii...dunia
dada!”
“Imefanya nini? Kwanza ni
nini kilitokea?”
“Dada nimeamini unaweza kuwa
na fedha nyingi sana lakini ukakosa mapenzi ya dhati kutoka kwa mtu mwenye
penzi la dhati!”
“Unamaanisha nini kaka
yangu?”
“Dada ninavyokuambia wiki
ijayo nilitakiwa kufunga ndoa na mpenzi wangu wa moyo Juliana, lakini
alichonifanyia siwezi kusahau katika maisha yangu yote!”
“Amefanya nini?”
“Si ulisema Juliana ndiye
aliyenileta hapa?”
“Ndiyo!”
“Basi huyo mwanamke ndiye
ambaye nilikuwa natarajia kufunga naye ndoa wiki ijayo, lakini nimemfumania na
mwanaume mwingine, mbaya zaidi ni rafiki yangu wa karibu ambaye ninamsaidia
vitu vingi ikiwemo pesa!”
“Pole sana Mungu
atakusaidia!”
“Nashukuru sana dada yangu!
Hivi, nilizimia kwa muda mrefu sana?”
“Siyo sana, uliletwa jana usiku
na sasa ni saa saba na nusu mchana!”
“Yaani nimepoteza fahamu kwa
masaa yote hayo?”
“Ndiyo, lakini usijali hali
yako sasa inaendelea vizuri na utapata nafuu, usijali!”
“Nashukuru sana!”
Yule Muuguzi akaondoka na
kumuacha Tom akiwa amelala peke yake kitandani, akili yake ikiwachambua
wanawake wawili; Juliana na Mariam! Moyo wake ulikuwa unamuuma sana kwa makosa
aliyomfanyia mpenzi wake wa zamani Mariam, hakuona kama alistahili kufanyiwa
yale. Alishanza kuamini kwamba laana ya Mariam ndiyo iliyokuwa ikiusambaratisha
uhusiano wake na Juliana.
Ilikuwa lazima atumie akili
nyingi sana, ndivyo alivyofanya. Hakutakiwa kuwa na papara katika hali ngumu
aliyokuwa nayo, alipaswa kuwa makini, mwenye mawazo endelevu katika matatizo
aliyokuwa nayo. Busara zake zilikuwa zinahitajika sana kwa wakati.
“Ndiyo...lazima niwe makini
sana hapa, nikicheza hapa naweza kupoteza muelekeo wa maisha yangu! Napaswa
kuwa mjanja huku nikiiacha akili yangu ichanganue mambo kwa nafasi, vinginevyo
nitakuwa nakaribisha machozi tena katika maisha yangu, jambo ambalo napingana
nalo kwa nguvu zote!” Aliwaza Tom.
“Lakini hapa sina ujanja
tena, nimeamini hakuna mapenzi ya kweli, ni bora nikarudiana na Mariam wangu,
ambaye ana mapenzi ya dhati na mimi, kwanza alinipenda kabla sijawa na kitu,
kwanini nisiamini kama ananipenda?
“Nisidanganyike na hawa
wasichana wa mjini, watanipotezea mwelekeo wa maisha yangu, nitakuja kulia
halafu niishie kuchekwa na wabaya wangu. Mariam...Mariam wangu, tafadhali sikia
kilio changu, ni kweli nimekukosea, lakini lazima ukumbuke hii dunia ina
vishawishi vingi sana.
“Nilipoteza mawasiliano na
wewe mpenzi wangu, sikujua kama ulipata matatizo makubwa kiasi ulichonieleza.
Akili yangu ilinituma kwamba umeamua kunisusa na kumuacha baba yangu afe wakati
wewe ukiwa katika matatizo makubwa.
“Nisamehe tafadhali, nisamehe
mpenzi wangu na ninakuomba unikaribishe katika himaya ya mapenzi yako tena.
Nisamehe mpenzi wangu, kukosea ni ukamilifu wa binadamu...tafadhali....nipo
chini ya miguu yako....” akiwa anawaza hayo, ghafla mlango wa wodi aliyokuwa
amelazwa ukafunguliwa.
Macho yake yakakutana na ya
Juliana akimwangalia kwa huzuni huku machozi yakianza kumlengalenga! Mikononi
mwake alikuwa amebeba maua mazuri yenye rangi nyeupe. Akasogea hadi kitandani
alipokuwa amelala Tom, akapiga magoti chini huku mikono yake iliyobeba maua
akiwa ameielekeza kwa Tom. Muda wote huo Tom alikuwa kimya akimtizama,
hakunyanyua mdomo wake wala kufanya jambo lolote zaidi ya kumwangalia.
“Najua nimekukosea sana
mpenzi wangu, kumbuka kwamba mimi ni binadamu, naomba unisamehe!” Juliana
akasema akilia kwa uchungu.
“Nikusamehe?” Tom akauliza
kwa sauti ya upole sana.
“Ndiyo naomba unisamehe
mpenzi wangu, kwanza kumbuka kwamba Joseph alinilazimisha, nilipoona anazidi
kuning’ang’ania nikamwacha!”
“Kwahiyo kila mtu akija
kukulazimisha wakati mimi sipo utakuwa tayari kufanya naye uchafu kama
mliofanya na Joseph siyo?”
“Sina maana hiyo mpenzi
wangu!”
“Kumbe una maana gani?”
“Nilipitiwa mpenzi wangu,
naomba unisamehe tafadhali!”
“Naomba kukuuliza swali moja
la msingi sana!”
“Nakusikia!”
“Unafahamu kwamba wiki ijayo
tutatakiwa kupanda madhabahuni kufunga ndoa?”
“Najua!”
“Sasa kuna ndoa gani ambayo
kabla hata haijafungwa imeshaanza kuwa na usaliti?”
“Mpenzi wangu kumbuka
tutaingia aibu sana kama tusipofunga, tumealika watu wengi sana na isitoshe
wanatuheshimu sana, sasa tutaficha wapi nyuso zetu mpenzi wangu?”
“Jiulize wewe utauficha wapi
uso wako siyo mimi!”
“Najua sweetie ndiyo maana
nakuomba msamaha! Kumbuka wazazi wangu wananipenda na kuniamini sana, wakisikia
nimefanya mambo haya itakuwa aibu kubwa sana kwangu na kwa familia nzima kwa
ujumla, naomba unisamehe tafadhali!”
“Sawa, nimeshakusamehe!” Tom
akasema huku akilia, maumivu aliyokuwa nayo moyoni mwake yalikuwa makali sana.
“Kweli Tom? Umenisamehe kweli
mpenzi wangu?”
“Niamini mpenzi, ni kweli
nimekusamehe!”
“Nashukuru sana kusikia
hivyo!”
“Hata mimi pia, lakini lazima
uwe makini na jambo moja!”
“Nakusikia mpenzi wangu!”
“Siku nikukufumania kwa mara
nyingine, ujue itakuwa ndiyo mwisho wa penzi letu!”
“Nimekuelewa!”
“Siyo uelewe pekee, uweke
akilini mwako na uhakikishe hurudii kosa hilo tena!”
“Nakuahidi mpenzi wangu!”
Juliana akaondoka hospitalini pale akiwa na furaha sana.
Taratibu za sherehe
zikaendelea kama kawaida, Juliana
alikuwa na hamu sana ya kufunga ndoa na Tom, alikuwa kijana mwenye mafanikio
makubwa sana. Ndoa yao ilipangwa kufungwa kifahari sana, kwanza ingefungiwa
katikati ya bahari wakiwa kwenye meli na sherehe nzima ya ndoa yao
ingemalizikia huko. Furaha yake ikarejea kwa mara ya pili.
“Nashukuru sana Mungu
amenisaidia, Tom wangu amenisamehe, nilikuwa na mashaka sana juu ya mpenzi
wangu, sikuwa na uhakika wa kurudi tena katika himaya yake, hasa ndoa ambayo
ilitaka kuingia dosari.
“Lakini na mimi nimezidi
tamaa, Joseph ana nini kiasi cha kunichanganya akili yangu kiasi kile? Hata
hivyo, sina sababu ya kuwaza mambo yaliyopita, acha niyaache yaliyopita yaende
zake na mimi nibaki na maisha yangu nikisubiria ndoa yangu iliyopo mbele
yangu!” Juliana akawaza huku akitabsamu.
*****
Siku iliyofuata Tom aliruhusiwa
kurudi nyumbani baada ya afya yake kutengemaa, Juliana ndiye aliyeenda
kumchukua hospitalini na kumrudisha nyumbani, njiani wakizungumza mambo mengi
yaliyohusu ndoa yao.
Kila mmoja alionekana kuwa na
hamu sana na ndoa yao, wakawa wanakwenda Kanisani kwa ajili ya Mafundisho ya
Ndoa kama kawaida, wageni wengi walikuwa wamealikwa kwa ajili ya kwenda
kushuhudia ndoa hiyo ya aina yake iliyopangwa kufanyika kwenye meli.
Kila kitu kilikwenda sawa
ingawa Tom alikuwa na maumivu makali sana katika moyo wake, alikuwa akiwaza
sana juu ya mabaya aliyofanyiwa na Juliana. Siku aliyomkuta Joseph ambaye
alikuwa rafiki yake kipenzi kifuani mwa Juliana, ilijirudia akilini mwake kila
wakati huku akihisi maumivu makali sana ya mapenzi.
Walishirikiana kwa kila kitu,
lakini Tom alikataa kufanya mapenzi na Juliana kwa kisingizio kwamba anasubiri
hadi siku ya ndoa.
“Lakini mbona tumekuwa
tukifanya siku zote hizo?”
“Siyo sababu!”
“Ni sababu!”
“Siyo sababu mpenzi wangu,
unajua hata kama tumemkosea Mungu kwa siku zote hizo, halafu tumekuja kugundua
baadaye kwamba tulikuwa tunamkosea ni vizuri tukabadilika!”
“Hapana...!”
“Nataka niwe na wewe mpenzi
wangu, kumbuka siku ya ndoa huwa na mshawasha wake, isitoshe tutakwenda
fungate, huoni kwamba itakuwa siku nzuri kwa sisi kufanya mapenzi tena, halafu isitoshe wakati huo tutaita tendo la
ndoa nadhani itakuwa nzuri sana!”
“Sawa lakini moyo wangu bado
una maswali mengi sana!”
“Maswali ya nini?”
“Nahisi kama kuna kitu
kinaendelea moyoni mwako!”
“Acha wasiwasi wako mpenzi
wangu, nini hicho kinaendelea moyoni mwangu?”
“Basi tuachane na hayo!”
“Sawa basi, tulale!”
“Mwaaa!” Wakapeana mabusu
motomoto na kulala.
*******
Zikiwa zimebaki siku tatu tu
kabla ya ndoa ya Tom na Juliana, huku vyombo mbalimbali vya habari vikitangaza
na kuandika juu ya ndoa hiyo ya aina yake nchini Tanzania, Tom alikuwa mwenye
mawazo mengi sana. Ni kweli alikuwa akimpenda sana mpenzi wake Juliana, lakini
kitendo cha usaliti kiliendelea kusafiri akilini mwake siku zote tangu siku ya
tukio lile na baadaye kulazwa.
Alihisi moyo wake ulikuwa
unakosa kitu muhimu sana, alimhitaji sana Mariam wake hata kama asingemuoa.
Alichokifanya ni kuandaa kadi kwa ajili ya Mariam kisha akampigia simu na
kumtaka aonane naye.
“Umesema unaitwa nani?”
“Thomas!”
“Tom?”
“Ndiyo!”
“Unataka kuonana na mimi?”
“Ndiyo!”
“Kuna nini?”
“Ni vizuri tuonane, siwezi
kuzungumza kwenye simu!”
“Namba yangu ni nani
amekupa?”
“Hilo siyo la muhimu kujua
kama ambalo linanifanya nikuite!”
“Tukutane wapi sasa?”
“Nitakuja Mlimani City!”
“Wapi sasa?”
“Samaki Samaki!”
“Sawa, saa ngapi?”
“Saa mbili kamili usiku
nitakuwa hapo!”
“Huwezi kufanya mapema
zaidi?”
“Muda huo ni mzuri zaidi
kutokana na aina ya maongezi niliyonayo!”
“Ok!”
“Kazi njema!”
Moyo wa Mariam ulilipuka
sana, hakujua Tom alikuwa na kitu gani cha kumwambia hasa ukizingatia alikuwa
akisikia kila kukicha juu ya maandalizi ya ndoa yake. Hata hivyo, aliisubiri
jioni hiyo kwa hamu kubwa sana, alihisi kama mshale wa sekunde hautembei
ipasavyo. Ikawa saa la kwanza, la pili hatimaye saa moja na nusu ilipofika
alikuwa kwenye teksi akielekea Mlimani City kukutana na Tom.
Alifika Mlimani City saa 1:48
za usiku, akiamini alikuwa amewahi sana lakini cha ajabu alimkuta Tom akiwa
anamsubiri kwa hamu kubwa sana. Mariam akamsogelea sehemu aliyokuwa amekaa
akitetemeka kwa woga, hakuamini kama aliyekuwa amekaa mbele yake alikuwa Tom.
“Habari yako mrembo?” Tom
akamsalimia.
“Nzuri! Mbona tumekaa sehemu
ya wazi kiasi hiki? Kumbuka wewe ni mtu maarufu na isitoshe ndoa yako ipo
mbioni kufungwa, huogopi wapiga picha wa udaku?”
“Wapo wanaosimamia hilo, siyo
rahisi kupigwa picha, vijana wangu wapo kazini!”
“Sawa basi, sema ulikuwa
unasemaje?” Mariam akauliza akiwa mtulivu sana.
Tom hakuongea chochote zaidi
ya kutoa kadi na kumkabidhi. Mariam akaifungua na kuisoma, ilikuwa ni kadi ya
mwaliko wa harusi yake ambayo ilikuwa inafanyika siku tatu zilizofuata.
“Umeamua kuja kunitukana?
Hujatosheka na mateso uliyonipa?”
“Tulia mrembo huwezi kujua
nina maana gani, lakini naomba usiache kuja, nina bonge la surprise kwa ajili
yako!”
“Surprise?”
“Ndiyo, niamini tafadhali,
naomba usipuuze!”
“Lakini wewe siku hiyo ndiyo
unaoa na unafahamu kabisa ni kiasi gani nakupenda, unataka niumie moyo wangu
kwa mara nyingine?”
“Sina maana hiyo Mariam,
nakuomba uje halafu nakuhakikishia furaha. Amini siku hiyo itakuwa ya furaha
kuliko zote zilizowahi kutokea katika maisha yako!” Tom alitumia kila aina ya
maneno matamu kumshawishi, mwishowe akakubali.
Akatoa bahasha ya khaki
ambayo ndani ilikuwa na milioni moja, akamkabidhi kama nauli. Mariam akakubali
kufika kwenye harusi ya Tom.
******
Watu walikuwa wamefurika
ndani ya meli, wakisubiria kwa hamu kubwa sana ndoa ya Julina na Tom ambayo
ilikuwa ya aina yake. Ibada iliendelea kama kawaida, baadaye Mchungaji akawaita
Tom na Juliana mbele kwa ajili ya kuwafungisha ndoa. Watu walipiga vigelegele
na makofi wakiwashangilia.
“Je, Bi. Juliana David
Mongara, umekubali kuolewa na Bw. Thomas Chacha, awe mumeo, kwenye shida na
raha, taabu na matatizo? Umpende, kumtunza na kumheshimu siku zote za maisha
yako, hadi kifo kiwatenganishe?” Mchungaji Samwel Kiswele aliuliza.
“Ndiyo Mungu anisaidie!”
Juliana akajibu akimtizama Tom machoni mwake, moyo wake bado ulikuwa na
wasiwasi mwingi.
Baada ya hapo Mchungaji
Kiswele akamgeukia Tom na kumuuliza; “Je, Bw. Thomas Chacha, umekubali kumuoa
Bi. Juliana David Mongara, awe mkeo,
kwenye shida na raha, taabu na matatizo? Umpende, kumtunza na kumheshimu siku
zote za maisha yako, hadi kifo kiwatenganishe?” Hilo lilikuwa swali gumu sana
kwa Tom, akamwangalia Juliana usoni kisha akarudisha macho yake kwa waalikwa,
yakagongana na ya Mariam.
Machozi yakaanza kumtoka.
“HAPANA MCHUNGAJI SIPO
TAYARI!” Watu wote wakapingwa na butwaa. Juliana akiwa haamini alichokisikia,
Tom akatoka mbio na kwenda kumshika Mariam mkono, ambaye mpaka wakati huo
alikuwa haelewi kinachoendelea, akamwongoza hadi mbele. Akatoa pete iliyokuwa
mfukoni mwake, kisha akachukua kidole cha Mariam na kumvalisha.
“Kuanzia sasa, wewe ndiye
mchumba wangu na ninakuahidi sitakutesa katika siku zote za maisha yako!
Tumuombe Mungu siku ya ndoa yetu ifike. Sherehe hii ni kwa ajili ya kumvalisha
mchumba wangu Mariam pete ya uchumba, aliyonifanyia Juliana yanatosha!” maneno
hayo yalipenya moja kwa moja masikioni mwa Juliana, hakuamini alichosikia,
Ghafla akahisi kizunguzungu,
akaanza kuporomoka taratibu, mwisho akaanguka chini kama mzigo.
Je, nini kitaendelea? Nini
kitampata Juliana?
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
Beyond Love- 19
Ikiwa imebaki
wiki moja tu kabla ya ndoa ya Juliana na Tom, Juliana anamsaliti Tom kwa
kutembea na rafiki yake wa karibu sana aitwaye Joseph! Tom anashuhudia kwa
macho yake jinsi mpenzi wake aliyempenda Juliana akifanya uchafu katika kitanda
chao.
Haikuwa rahisi
kuvumilika, Tom akaanguka chini kama mzigo! Baadaye akazinduka akiwa katika Hospitali
ya Ocean Road jijini Dar es Salaam. Muda mfupi baadaye anatoekea Juliana ambaye
analia na kuomba msamaha.
Tom anakubali
kumsamehe na wanakubalina kufungua ukurasa mpya! Taratibu za ndoa zinaendelea
kama kawaida, ingawa akilini mwa Tom kulikuwa na kitu kingine zaidi, alipanga
kumuumiza Juliana siku ya ndoa yao.
Alichokifanya
ni kukutana na mpenzi wake wa zamani Mariam ambapo alimuomba sana asiache
kuhudhuria hasuri yake ambayo ilipangwa kufanyikiwa ndani ya meli katikati ya
Bahari ya Hindi. Mariam anakataa lakini baada ya kumshawishi kwa muda mrefu
akakubali.
Siku ya ndoa,
Juliana alipoulizwa na Mchungaji kama alikuwa tayari kuolewa na Tom alikubali,
lakini Tom alipoulizwa kama alikuwa tayari kumuoa Juliana alikataa. Muda mfupi
baadaye akamwita Mariam mbele na kumvalisha pete ya uchumba mbele za wageni
waalikwa.
Watu
walishangaa sana, Juliana akashikwa na uchungu mwingi sana, akashindwa kuzuia
hisia zake, akaanguka chini na kupoteza fahamu. Je, nini kitatokea? SONGA
NAYO....
Ukumbi mzima
ulikuwa kelele tupu, utulivu uliokuwepo awali ulitoweka ghafla. Kulikuwa na
makundi mawili katika kelele zile, wapo waliokuwa wakimsapoti Tom na wengine
waliokuwa wakipingana naye. Waliokubaliana na Tom ni wale waliokuwa wakifahamu
vizuri historia yake na Mariam.
Mama yake Tom
hakuamini kilichotokea, akaenda mbele haraka akimfuata mwanaye. Wakati huo huo
wengine walikuwa wakimchukua Juliana na kumpeleka kwenye chumba cha Huduma ya
Kwanza kwa ajili ya kumhudumia.
Dakika moja
baadaye mama Tom alikuwa ameshafika mbele baada ya kujipenyeza katikati ya watu
waliokuwa wakizozana kutokana na tukio lililokuwa limetokea siku hiyo. Tom
hakuwa na habari kabisa na mama yake, aliendelea kumkumbatia Marima huku
machozi yakimtoka.
Mariam
hakuamini kabisa kilichokuwa kikitokea, alihisi kama alikuwa katika njozi kali
na pengine baada ya muda mfupi angezinduka. Hata hivyo baada ya kutingisha
kichwa chake kwa nguvu aligundua kwamba hakuwa anaota kama alivyokuwa
akifikiria.
“Tom mwananu,
umefanya nini?” Mama Tom akamuuliza mwanaye.
“Unaaminisha
nini mama?”
“Kwanini
unatuharibia sherehe?”
“Sijaharibu
sherehe mama, sherehe iliyopo hapa ni ya kumvalisha pete ya uchumba Mariam,
hiyo ndoa yangu na Juliana haipo na wala sitaki kuisikia!”
“Kwanini
hukusema mapema kuliko kuja kumuaibisha mwenzio na familia yake?”
“Ilikuwa lazima
nifanye mama!”
“Kwanini
unasema hivyo?”
“Naomba MC
anipe kipaza sauti nitoe sababu za msingi za mimi kukataa kumuoa Juliana dakika
za mwisho, najua mnanihukumu bure na hiyo ni kwasababu hamjui kilichotokea.
Nipeni nafasi niseme ukweli!” Tom akasema akimtizama mama yake kwa makini sana.
Mama Tom
akatoka na kumfuata MC ambapo alimuomba kipaza sauti na kumpelekea Tom ambaye
bila kuchelewa alianza kuzungumza.
“Najua wengi
mnanilaumu kwa kitendo changu cha kukataa kumuoa Juliana, lakini naamini
nikiwapa sababu za msingi mtanionea huruma. Hata wewe mama yangu ambaye umekuja
hapa mbele na kunisema kwamba nimekuabisha, utagundua kuwa Juliana ndiye
aliyekuabisha.
“Naamini hata
wazazi wa Juliana na ndugu zake wote watajua wazi kwamba mtoto wao ndiye
aliyeleta aibu hii katika hii sherehe. Juliana hafai kabisa, ni mwanamke mwenye
sura ya kike lakini siyo mke.
“Nilimpenda
sana Juliana, moyo wangu nikamkabidhi yeye
nikiamini kwamba angekuwa furaha ya maisha yangu, lakini imekuja kuwa
tofauti. Juliana ameniumiza sana, amenitesa na nina uhakika alidhamiria
kuniua,” Tom alikuwa akizungumza kwa hisia sana huku ukumbi mzima ukiwa makini
kumsikiliza atakachokiongea.
Mpaka wakati
huo, bado Tom alikuwa hajataja sababu ya msingi ya kuachana na Juliana, hivyo
watu walikuwa na shauku kubwa sana ya kutaka kujua atakachokiongea.
“Wengi wenu
mnafahamu kwamba wiki moja iliyopita nilikuwa nimelazwa, lakini hamjui sababu
ya mimi kulazwa, ila leo nataka kuwaelezeni ukweli kwamba Juliana ndiyo cha
mimi kulazwa. Nilianguka na kupoteza fahamu baada ya kumfumania Juliana
akifanya mapenzi na rafiki yangu wa karibu sana Joseph!” Tom aliposema hivyo
ukumbi mzima ulipigwa na butwaa.
“Aaaaaah!” Wati
wote walisikika wakiguna.
“Ni maumivu
kiasi gani aliyonipa Juliana? Ni nani ambaye angeweza kuvumilia maumivu hayo?
Baada ya mambo hayo kutokea, niliamua kutulia, nikawaza kwa makini sana hatua
ya kuchukua. Nilijua hakuna atakayenielewa kama ningehairisha ndoa.
“Kitu cha
msingi ambacho kilikuwa kichwani mwangu ni kuacha taratibu zote ziendelee
lakini akilini nikijua kwamba itakuwa ni sherehe ya kumvalisha Mariam pete ya
uchumba na siyo ya ndoa yangu na Juliana. Nilikumbuka mengi aliyonifanyia
Mariam, nikasikia uchungu sana.
“Mariam
alinisaidia sana wakati nikiwa na shida, aliiba gari lao na kumpeleka baba
yangu hospitalini akiwa hoi usiku wa manane. Kwa bahati mbaya wakati
anarudi nyumbani, alipata ajali mbaya na
kulala kitandani akiwa hajitambui kwa zaidi ya miaka minne!
“Yote hayo
alifanya kwa ajili yangu, sikuwa na zawadi nyingine ya kumpa zaidi ya penzi la
kweli kwake. Hiyo ndiyo zawadi ya pekee ambayo naona inamfaa kwa wema wote
alionitendea. Mariam alikuwa katika hatari ya kufa, kupoteza fahamu kwa zaidi
ya miaka minne ni nusu ya kufa, inawapasa wote mfahamu kwamba Mariam alikuwa
katika hatari hiyo kwa ajili ya penzi lake kwangu!
“Kwanini
nimuumize tena? kwanini nimtese tena? Pamoja na utajiri nilionao sasa, usaliti
wa Juliana ulinifanya nikumbuke maisha yangu ya dhiki na taabu. Ni kitu gani
alichokikosa kwangu hadi aanze kutembea na Joseph? Huyo Joseph ana nini ambacho
mimi sina? Kwa hakika Juliana alinipa kidonda kikubwa sana katika moyo wangu
lakini sasa nimeshapata tiba.
“Mariam ni tiba
tosha katika maisha yangu. Naomba sherehe iendelee lakini ikumbukwe kwamba ni
sherehe ya kumvalisha mchumba wangu Mariam pete, ni matumaini yangu kwamba siku
chache zijazo, mtashuhudia ndoa yetu nzuri sana, itakayopendeza!” Tom alisema
watu wakiwa kimya kabisa kumsikiliza.
Maneno
aliyoongea yalikuwa makali san, watu wote walimwonea huruma, lakini wapo
waliompongeza kwa ujasiri wake.
“Ana moyo sana
huyu mtoto!” Mama mmoja aliyealikwa alimwambia mwenzake.
“Ni kweli, kama
ni mtu mwingine asingeweza kuvumilia!”
“Lakini kuna
kitu nahisi!”
“Kitu gani?”
“Unajua kwa
jinsi Mariam alivyomsaidia, ilikuwa lazima arudiane naye siku moja!”
“Kwanini
unasema hivyo?”
“Mapenzi yana
nguvu sana ndugu yangu, kama mtu aliweza kuhatarisha uhai wake kwa sababu ya
mapenzi, unadhani uhusiano wa aina hiyo unaweza kufa hivyo?”
“Kweli kabisa,
mwacheni Mungu aitwe Mungu!”
“Yeye ni kila
kitu, akisema iwe na inakuwa hivyo, akisema hapana, inakuwa hapana. Hakika yeye
ni mwema!” Kila mtu alikuwa akiongea lake latika ukumbi huo uliokuwa kwenye
Meli.
Sherehe
ikaendelea kama kawaida, ingawa utaratibu haukuwepo na hakuwa na utaratibu wa
kutoa zawadi. Walishauriwa warudi nazo kwanza hadi siku ya ndoa ya Mariam na
Tom. Watu walikunywa, kula na kusaza.
“Tom!” Mariam
alimwita walipokuwa wamejibanza kwenye eneo lenye giza totoro.
“Nakusikiliza
mpenzi!”
“Umenishangaza
sana!”
“Kwanini?”
“Sikutegemea!”
“Hata mimi pia,
lakini leo nimeamini kwamba Mungu yupo na akipanga lake hakuna yeyote chini ya
jua anayeweza kupangua. Nakuhakikishia Mariam, Mungu alipanga mimi niishi na
wewe!”
“Ni kweli
mpenzi wangu, tumetoka mbali!”
“Kweli kabisa,
nakuhakikishia utafurahia maisha siku zote za uhai wako ukiwa na mimi. nataka
kulipa fadhila zote kwako, nataka kukuonyesha kulala kwako kitandani kwa zaidi
ya miaka minne ukiwa huna kumbukumbu ya chochote kinachoendele haikuwa bure!”
“Nitashukuru
sana mpenzi wangu!”
“Mariam
mpenzi!” Tom akaita kwa sauti iliyojaa mahaba.
“Naomba
unifanyie kitu kimoja....”
“Sema tu,
mpenzi!”
“Naomba
unibusu!”
“Hilo tu, sema
lingine!”
“Siyo zaidi ya
busu lako!”
“Haya bwana!
Mmwaaaaaaaaa...” Mariama akamuangushia Tom busu maridhawa kabisa.
“Ahsante sana
mpenzi!”
Baada ya
sherehe kuisha, meli ilirudi hadi Bandarini na kutia nanga, watu wakashuka na
kutawanyika. Tom akampeleka Mariam Hotelini kwake. Mapenzi yao yakarudi upya,
yalikuwa motomoto.
******
Mwezi mmoja
baadaye taratibu zote zilikuwa zimeshakamilika. Tom alitambulishwa rasmi
nyumbani kwa akina Mariam kama mchumba wa Mariam, wazazi wa Mariam hawakuwa na
kipingimizi. Waliruhusu watoto wao waendelee na mapenzi yao kutoakana na ukweli
kwamba walianza kupendana muda mrefu kabla wakati wanasoma.
Mipango ya ndoa
ikafanyika haraka sana, ilipangwa kufanyika ndoa ya kifahari kuliko kawaida.
Kama ilivyokuwa wakati akitaka kufunga ndoa na Juliana ndivyo alivyofanya pia
safari hii, aliamua kufunga ndoa yake katikati ya Bahari ya Hindi, wakiwa
kwenye meli.
Ndivyo
ilivyokuwa, siku ya harusi ambayo ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa ilifika,
waalikwa walikuwa ni wengi sana. Mariam na Tom walikuwa haamini kabisa
kilichotokea, walikuwa na nyuso za furaha sana kufunga ndoa yao.
Mchungaji
akawaita mbele wakiwa na wapambe wao, ambapo mara moja shughuli ya kuwafungisha
ndoa ikaanza.
“Je,
Bw. Thomas Chacha, umekubali kumuoa Bi.
Mariam Isaya, awe mkeo, kwenye shida na raha, taabu na matatizo?
Umpende, kumtunza na kumheshimu siku zote za maisha yako, hadi kifo
kiwatenganishe?” Hilo lilikuwa swali rahisi sana kwa Tom, akamwangalia Mariam
usoni kisha akarudisha macho yake kwa waalikwa, baada ya hapo akajibu.
“Ndiyo, Mungu anisaidie!”
Ukumbi mzima ukapiga vigelegele na makofi kwa furaha.
Baada ya Tom kujibu,
Mchungaji aliyekuwa akifungisha ndoa akamgeukia Mariam na kumuuliza; “Je, Bi.
Mariam Isaya, umekubali kuolewa na Bw. Thomas Chacha, awe mumeo, kwenye shida
na raha, taabu na matatizo? Umpende, kumtunza na kumheshimu siku zote za maisha
yako, hadi kifo kiwatenganishe?” Mchungaji akamuuliza lakini Mariam hakujibu.
Mchungaji
akaamua kuuliza kwa mara ya pili, bado Mariam alikuwa kimya. Ghafla Mariam
akaanza kutoa miguno ya taratibu, baadaye akashindwa kujizuia na kuanza kuangua
kilio. Tom akashtuka sana, hata waalikwa nao walipigwa na butwaa.
“Mariam kuna
nini?”
“Hakuna!”
“Mbona hujibu
maswali ya Mchungaji!”
“Hapana...”
“Hapana nini?”
Tom akazidi kumuuliza akiwa haelewi kinachoendelea. Mariam alizidi kulia.
Je, kuna nini? Kwanini Mariam analia?
Beyond Love- 20
Tom haamini macho yake
alipomkuta mpenzi wake ambaye walikuwa na mipango ya kufunga ndoa, Juliana
akimsaliti, tena na rafiki yake wa karibu aliyeitwa Joseph.
Lilikuwa tukio lililomsononesha
sana, hali iliyomsababishia simanzi, kabla ya kuanguka chini na kupoteza
fahamu. Baadaye anazinduka akiwa katika Hospitali ya Ocean Road, ambapo Juliana
anakuwa wa kwanza kuonana naye na kumuomba msamaha.
Tom anakubali kumsamehe na wanakubaliana kufungua
ukurasa mpya! Taratibu za ndoa zinaendelea kama kawaida, ingawa akilini mwa Tom
kulikuwa na kitu kingine zaidi, alipanga kumuumiza Juliana siku ya ndoa yao.
Akafanya mpango wa kukutana na mpenzi wake wa
zamani Mariam ambapo alimuomba sana asiache kuhudhuria harusi yake ambayo
ilipangwa kufanyikiwa ndani ya meli katikati ya Bahari ya Hindi. Mariam
anakataa lakini baada ya kumshawishi kwa muda mrefu akakubali.
Siku ya ndoa, Juliana alipoulizwa na Mchungaji kama
alikuwa tayari kuolewa na Tom alikubali, lakini Tom alipoulizwa kama alikuwa
tayari kumuoa Juliana alikataa. Muda mfupi baadaye akamwita Mariam mbele na
kumvalisha pete ya uchumba mbele za wageni waalikwa.
Siku chache mbele, Mariam na Tom wakaamua kufunga
ndoa! Kama ilivyokuwa awali, ndoa yao
ilifungwa katikati ya bahari, kwenye meli. Kitu cha kushangaza, Mariam
alipoulizwa na Mchungaji kama alikuwa tayari kuolewa na Tom, alinyamaza.
Baadaye akaanza kulia kabisa. Tom alipomuuliza kama
kulikuwa na tatizo lolote, Mariam hakujibu. Je, nini kitatokea? SONGA NAYO....
Kitendo cha Mariam kukataa kujibu swali la
Mchungaji kama alikuwa tayari kuolewa na Tom au lah, kilimchanganya sana Tom,
alishaanza kuhisi mchezo mchafu ulikuwa ukichezwa nyuma ya pazia. Ukimya wa
Mariam ukazidi kumchanganya.
Hata hivyo alikosa raha zaidi baada ya kushangaa
Mariam akianza kulia, hapo akili yake ikaenda mbali zaidi, alianza kufikiria
kwamba, inawezekana Mariam alilazimishwa kumuumiza siku ya ndoa yao ili ampe
maumivu lakini yeye hakuwa tayari.
Zote hizo zilikuwa hisia zilizoutawala ubongo wake,
lakini mwenye majibu sahihi alikuwa ni Mariam pekee, alitakiwa kutumia kila
njia anayoifahamu ili aweze kujua kilichokuwa kikiendelea. Akamgeukia Mariam
wake ili amuulize kwa ajili ya kupata uhakika zaidi, tayari akili yake
ilishabadilika, alipoteza matumaini ya kuwa na Mariam tena.
“Kuna nini Mariam?”
“Nishakujibu Tom.”
“Kwamba?”
“Sina tatizo.”
“Mbona unashindwa kumjibu Mchungaji, hujui kwamba
ni wewe ndiye unayesubiriwa ili ndoa iweze kufungwa?”
“Najua...”
“Sasa?”
“Nashindwa kuamini kabisa.” Marim akasema
akionekana kuwa na hofu sana na maneno aliyokuwa akiyaongea.
“Huamini nini tena? Kwani kuna nini?”
“Nashindwa kuzuia hisia zangu Tom, nimeshindwa
kabisa.”
“Hisia za nini tena?”
“Machozi Tom, unajua wewe ndiye mwanaume pekee
ambaye nilikukabidhi moyo wangu, siamini kabisa kwamba nimeweza kuwa na wewe
tena katika ndoa!” Mariam akasema machozi yakizidi kumtoka.
“Amini mpenzi wangu...mwambie basi Mchungaji
aendelee kwanza, haya mambo mengine tutazungumza wenyewe baadaye,” Tom alisema
akiwa haamini kama Mariam hatamkataa, akili yake ilimtuma moja kwa moja kwamba
lazima Marim angemkataa ili amuumize kama ambavyo yeye alivyomuumiza siku
alipokutana naye Chuo Kikuu alipokwenda kutoa semina ya Ujasiriamali.
“Mchungaji unaweza kuendelea....” Mariam akamwambia
Mchungaji.
“Nini kilitokea?” Mchungaji akauliza.
“Hakuna...” Mariam akajibu.
“Hpana...kuna kitu mnanificha. Kama kuna tatizo
liwekeni wazi.”
“Hakuna Mchungaji, niamini mimi, hakuna kitu
kingine zaidi ya furaha. Siamini kabisa kwamba leo naolewa na Thomas.”
“Hilo tu.”
“Kwani dogo Mchungaji? Kuolewa na mwanaume ambaye
unampenda kwa moyo wako wote, nafikiri ni jambo la baraka sana!”
“Ni kweli kabisa, sasa naweza kuendelea Mariam?’
“Bila shaka.” Maram akajibu akionyesha tabasamu
pana kabisa lililochanua vyema usoni mwake.
Muda wote huo Kanisa lilikuwa kimya kabisa,
wakisubiri kitakachoendelea. Baadaye Mchungaji akamgeukia Mariam, ambaye sasa
machozi yake yalishafutika na alikuwa akitabasamu muda wote kwa furaha.
Mchungaji akamuuliza; “Je, Bi. Mariam Isaya, umekubali kuolewa na Bw. Thomas
Chacha, awe mumeo, kwenye shida na raha, taabu na matatizo? Umpende, kumtunza
na kumheshimu siku zote za maisha yako, hadi kifo kiwatenganishe?” Mchungaji
akauliza, safari hii akiwa mtulivu sana.
“Ndiyo, Mungu anisaidie!” Mariam alipojibu jibu
hilo, ukumbi mzima ulilipuka kwa vigelegele, makofi na vifijo.
Tom hakuamini kama ni kweli Marim alikuwa ameamua
kuolewa naye. Aliendelea kuwa na mashaka hadi pale waliposaini pamoja katika
vyeti vya ndoa. Baada ya hapo sherehe iliendelea hadi usiku kabisa ambapo meli
ilirudi hadi Bandarini, ikatia nanga, wageni wakaanza kushuka na kwenda kuingia
moja kwa moja kwenye magari kwa safari ya kurudi majumbani mwao.
Ilikuwa sherehe iliyopendeza sana, huo ukawa mwanzo
wa maisha mapya ya ndoa, kati ya Tom na Mariam.
********
Maisha yao ya ndoa yalikuwa ya furaha sana, lakini
tatizo lilikuwa moja tu, Tom alikuwa mtu wa starehe sana. Kila siku alikuwa
haishi kwenda kwenye majumba ya starehe na kurudi usiku wa manane. Kisingizio
chake siku zote kikawa ni kazi nyingi alizonazo.
Ingawa Mariam alikuwa na elimu nzuri, lakini Tom
alimzuia kufanya kazi kwa kisingizio kwamba atamdharau. Siku zote Mariam
alikuwa akijitahidi sana kumuelewesha Tom juu ya hilo lakini hakumuelewa.
“Na kwanini unalazimisha sana kufanya kazi?”
“Napenda mume wangu.”
Kuna unachokosa kutoka kwangu?”
“Sina maana hiyo.”
“Sasa kwanini unang’ang’ania kufanya kazi? Mimi
nina uwezo na ninakutimizia kila kitu, nini kinachokufanya utafute kazi?”
“Ni vizuri kila mmoja akatoka, unajua ninapokaa
hapa ndani nalemaa.”
“Unalemazwa na nini?”
“Lakini kwanini nimesoma sasa kama nilikuwa sina
haja na kazi? Elimu yangu inanisaidia nini kama sitaitumikia jamii?”
“Hiyo jamii na mimi, ni nani mwenye umuhimu zaidi
kwako?”
“Ni wewe mume wangu.”
“Basi sihitaji ufanye kazi.”
“Nimekuelewa ila kuna kitu kingine nataka
tuzungumze.”
“Juu ya nini tena?”
“Tom mume wangu, umekuwa ukichelewa sana kurudi
nyumbai, wakatiu mwingine unanikuta nimeshalala kabisa, uwe unajitahidi basi
kuwahi kidogo!”
“Mariam una nini leo? Kwanza niwahi kuja kufanya
nini? Mimi napika?”
“Hupiki, lakini unatakiwa kuja kula na mimi, ndiyo
mapenzi hayo mume hayo mume wangu.”
“Nimekuelewa!” Tom akajibu kwa kifupi kisha akaondoka.
Maisha yao hayakuwa na furaha kama ilivyokuwa
mwanzo, Tom alikuwa hana muda maalum wa kurudi nyumbani. Mbaya zaidi alirudi
akiwa amelewa sana na hakutaka kula chakula cha mkewe. Jambo hilo lilimkosesha
sana raha Mariam lakini hakuwa na jinsi, aliamua kuvumilia akiamini siku moja
angebadilika.
*******
Ilikuwa siku ya Jumamosi usiku, ndani ya Ukumbi wa
56 Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam. Watu walikuwa wamejaa sana kushuhudia
uzinduzi wa albamu mpya ya Bendi ya Kigingi Music Band ambapo pia mbali na
uzinduzi wa albamu yao mpya, pia walikuwa wakiwatambulisha wanamuziki wapya
walionunuwa na Tom ambaye ambaye alikuwa akiitwa Papaa Bill.
Pesa haikuwa tatizo, Papaa Bill (Tom) aliwanunua
wanamuziki hao kutoka nchini Congo ambapo walikuwa wakifanya kazi katika bendi
kongwe za muziki nchini humo, lakini kwa fedha alizokuwa nazo Papaa Bill,
aliweza kuwaleta Tanzania na kuwalipa fedha nyingi sana.
Baadhi ya watu walikuwa wakimsikia tu Papaa Bill
kwenye vyombo vya habari hasa magazeti na redio, lakini walikuwa hawajawahi
kumuona. Kati ya hao alikuwa ni Mayasa. Msichana ambaye alikuwa na hamu kubwa
sana ya kumuona Tom.
Mayasa alikuwa na nia zaidi ya kumfahamu, yeye
alipanga kumuweka mkononi mwake. Pamoja na kusikia kwamba alikuwa na mke,
lakini kwake halikuwa tatizo, alishaandaa mbinu za kutosha kwa ajili ya kumsana
Tom. Huyu ni Mayasa wa Mbagala jijini Dar es Salaam.
Usiku huo alikuwa amevalia gauni jepesi sana
linaloonesha kila kitu ndani! Kwa mwanaume yeyote ambaye hana matatizo, ilikuwa
lazima ashtuke sana pindi atakapokutanisha uso wake na Mayasa. Kiasili alikuwa
maji ya kunde, lakini mkorogo ulifanya kazi yake ambapo alionekana mweupe sana
isipokuwa kwenye viungio vya ugoko wa miguuni na mikono, ambapo kutokana na
ngozi kuwa ngumu sana, haikuweza kuchunika kwa mkorogo!
“Leo lazima nimuone huyo Papaa Bill!” Rafiki yake
na Mayasa alisema.
“Bora wewe unayetaka kumuona, miye naondoka naye
kabisa...” Mayasa alisema akionyesha kuwa na nyodo za wazi kabisa.
“Haya tuone. Unafikiri Papaa Bill ni sawa na hao
wanaume wako wa Mbagala, huyu ni matawi ya juu.”
“Sasa nitajua kama Mbagala ipo Dar es Salaam au
Lindi?” Mayasa alisema akionyesha kujiamini sana.
Dakika chache baadaye, wakati wakiendelea na
mazungumzo yao, Mc wa siku hiyo, alisimamisha muziki kwanza kisha akamuomba
Papaa Bill atoke mbele ya jukwaa ili awatambulishe wanamuziki wapya. Papaa Bill
akatoka.
“Ninayo heshima kubwa sana, kumkaribisha Papaa Bill
a.k.a Tom ili aje awatambulishe wanamuziki wetu wapya. Kwa taarifa tu ni
kwamba, pamoja na kwamba yeye ndiye anayewalipa wanamuziki hao mishahara pamoja
na kuwanunua, pia ndiye aliyeenda kuwachukua mwenyewe Congo!” Mc aliposema
maneno hayo, ukumbi mzima ukashangilia.
Tom ‘Papaa Bill’ akapanda jukwaani kwa mbwebwe
sana, jioni hiyo alikuwa amevalia suruali yake ya jeans ya rangi ya blue na
fulana ya kubana ya rangi nyeupe. Mikononi na shingoni alichafuka cheni za
madini ya fedha!
“Sina mengi ya kuongea, naomba niwatambulishe
wanamuziki wetu wageni ambayo mimi mweny....” Tom alishindwa kumalizia sentesi
yake, baada ya kugonganisha macho yake na Mayasa.
“Haki ya nani tena, sijawahi kukutana na mwanamke
mzuri kiasi hiki! Mh...wa wapi huyu?” Tom aliwaza akiwa amezidiwa vilivyo na
hisia kali za mapenzi.
Kwa hali aliyokuwa nayo, alikuwa tayari kumsaliti
Mariam wake.
“Naitwa Tom....bila shaka mimi ni Tom a.k.a Papaa
Bill...namuhitaji huyu mwanamke, ni lazima nilale naye, lazima...” Tom akawaza
huku akimtizama kwa matamanio.
Wakati huo Mayasa ndiyo akazidisha vituko,
akapandisha gauni lake juu zaidi na kuacha sehemu kubwa ya mwili wake ikiwa
wazi. Tom akasikiza mwili wake ukipiga shoti!
Je, nini kitatokea? Tom amejikuta akimtamani Mayasa
ghafla bila kujua kwamba Mayasa naye alikuwa akimuwinda.
KUPATA SIMULIZI TAMU ZAIDI JIUNGE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie
LIKE HAPA >>>>>>>>www.facebook.com/2jiachie


Post a Comment