MUME WA FLORA MBASHA ASAKWA KWA UBAKAJI
Mume wa mwimbaji maarufu wa nyimbo za Injili nchini, Flora Mbasha,
Emmanuel Mbasha anayetafutwa na polisi kwa kosa la ubakaji.
JESHI la Polisi Mkoa wa Ilala jijini Dar es Salaam linamsaka kwa udi na uvumba
Emmanuel Mbasha (pichani) ambaye ni mume wa mwimbaji maarufu wa nyimbo za
Injili nchini, Flora Mbasha kwa madai ya kumbaka shemeji yake mwenye miaka 17 (jina tunalo) ambaye ni yatima.
Taarifa zilizopatikana ndani ya jeshi hilo kupitia vyanzo vyetu makini zinadai kwamba
mlalamikaji huyo alifika kituoni hapo Jumatatu iliyopita muda wa mchana na kufungua kesi
yenye Kumbukumbu Na. TBT/RB/3191/2014 na ya Jalada la
Uchunguzi Na. TBT/IR/1865/2014 akidai kufanyiwa unyama huo
kwa siku mbili (Ijumaa na Jumapili) wiki iliyopita nyumbani kwa Mbasha,
Tabata-Kimanga, Dar.
Ilidaiwa kuwa, Ijumaa iliyopita mlalamikiwa alifanya kitendo hicho sebuleni nyumbani
na Jumapili ilidaiwa alitekeleza ukatili wake huo ndani ya gari lake hali ambayo ilimfanya mlalamikaji kutoa taarifa Kituo cha Polisi, Tabara-Aroma jijini Dar.
Iliendelea kudaiwa kuwa, kufuatia maumivu makali aliyoyapata
mlalamikaji huyo ilibidi aende Hospitali ya Amana na kugundulika
kuwa aliingiliwa kimapenzi na kumsababishia michubuko sehemu za siri.
HISTORIA YA MLALAMIKAJI
Mlalamikaji ni kati ya watoto mapacha waliozaliwa jijini Mwanza
na mama ambaye jina lake halikupatikana mara moja.
Mama wa mtoto huyo (kwa sasa ni marehemu pamoja na mume wake) akiwa
muumini wa Kanisa la Evangelical Assemblies of God (EAGT) aliamua
kumtoa mtoto mmoja kwa mama mzazi wa Flora Mbasha kwa lengo la kumlea,
wakati huo mtoto huyo alikuwa na miezi mitatu.
Ikaelezwa kuwa, mama wa Flora alikaa na mtoto huyo akimsomesha hadi
alipofika darasa la saba ambapo alimkabidhi kwa Flora na kuishi naye hadi
alipofikwa na janga hilo.
Maelezo zaidi yanasema Mbasha aliweza kufanya kitendo hicho kwa sababu
mkewe (Flora) ameondoka nyumbani na kwenda kuishi hotelini kwa kile
kilichodaiwa kwamba kuna ugomvi mkubwa ndani ya ndoa yao.
Taarifa zaidi zinadai kwa sasa Mbasha naye hayupo nyumbani kwake huku
mlalamikaji yuko Hospitali ya Amana akiendelea kufanyiwa uchunguzi wa kiafya
ili kubaini kama ana maambukizi ya magonjwa ya zinaa au la!
Kwa upande wake mlalamikaji huyo alipopigiwa simu juzi kwa lengo la
kuthibitisha kuhusiana na sakata hilo alikiri na kusema amekwishatoa taarifa
polisi kwa kitendo alichofanyiwa na mwenye nyumba huyo huyo.
Emmanuel Mbasha anayetafutwa na polisi kwa kosa la ubakaji.
JESHI la Polisi Mkoa wa Ilala jijini Dar es Salaam linamsaka kwa udi na uvumba
Emmanuel Mbasha (pichani) ambaye ni mume wa mwimbaji maarufu wa nyimbo za
Injili nchini, Flora Mbasha kwa madai ya kumbaka shemeji yake mwenye miaka 17 (jina tunalo) ambaye ni yatima.
Taarifa zilizopatikana ndani ya jeshi hilo kupitia vyanzo vyetu makini zinadai kwamba
mlalamikaji huyo alifika kituoni hapo Jumatatu iliyopita muda wa mchana na kufungua kesi
yenye Kumbukumbu Na. TBT/RB/3191/2014 na ya Jalada la
Uchunguzi Na. TBT/IR/1865/2014 akidai kufanyiwa unyama huo
kwa siku mbili (Ijumaa na Jumapili) wiki iliyopita nyumbani kwa Mbasha,
Tabata-Kimanga, Dar.
Ilidaiwa kuwa, Ijumaa iliyopita mlalamikiwa alifanya kitendo hicho sebuleni nyumbani
na Jumapili ilidaiwa alitekeleza ukatili wake huo ndani ya gari lake hali ambayo ilimfanya mlalamikaji kutoa taarifa Kituo cha Polisi, Tabara-Aroma jijini Dar.
HISTORIA YA MLALAMIKAJI
Mlalamikaji ni kati ya watoto mapacha waliozaliwa jijini Mwanza
na mama ambaye jina lake halikupatikana mara moja.
Mama wa mtoto huyo (kwa sasa ni marehemu pamoja na mume wake) akiwa
muumini wa Kanisa la Evangelical Assemblies of God (EAGT) aliamua
kumtoa mtoto mmoja kwa mama mzazi wa Flora Mbasha kwa lengo la kumlea,
wakati huo mtoto huyo alikuwa na miezi mitatu.
Ikaelezwa kuwa, mama wa Flora alikaa na mtoto huyo akimsomesha hadi
alipofika darasa la saba ambapo alimkabidhi kwa Flora na kuishi naye hadi
alipofikwa na janga hilo.
Maelezo zaidi yanasema Mbasha aliweza kufanya kitendo hicho kwa sababu
mkewe (Flora) ameondoka nyumbani na kwenda kuishi hotelini kwa kile
kilichodaiwa kwamba kuna ugomvi mkubwa ndani ya ndoa yao.
Taarifa zaidi zinadai kwa sasa Mbasha naye hayupo nyumbani kwake huku
mlalamikaji yuko Hospitali ya Amana akiendelea kufanyiwa uchunguzi wa kiafya
ili kubaini kama ana maambukizi ya magonjwa ya zinaa au la!
Kwa upande wake mlalamikaji huyo alipopigiwa simu juzi kwa lengo la
kuthibitisha kuhusiana na sakata hilo alikiri na kusema amekwishatoa taarifa
polisi kwa kitendo alichofanyiwa na mwenye nyumba huyo huyo.
CHANZO NI GPL
Post a Comment