ad

ad

REAL MADRID YAITANDIKA BAYERN MUNICH 4-0 NA KUIVUA UBINGWA WA ULAYA


Wachezaji wa Real Madrid wakishangilia moja ya bao lao baada ya kuifua Bayern Munich katika Ligi ya Mabingwa Ulaya Uwanja wa nyumbani kwao, Allianz Arena mjini Munich, Ujerumani na kuivua ubingwa ulaya.
Sergio Ramos na Cristiano Ronaldo(wa pili kutoka kushoto) wakishangilia.
Cristiano Ronaldo akifunga bao la nne dakika ya 89.
Hivyo ndivyo unavyoweza kusema kuhusu Bayern Munich baada ya usiku huu kutandikwa mabao 4-0 na Real Madrid katika Nusu Fainali ya pili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Uwanja wa nyumbani kwao, Allianz Arena mjini Munich, Ujerumani.

Bayern wamevuliwa ubingwa wa Ulaya kwa kipigo cha jumla cha mabao 5-0, baada ya awali kuchapwa 1-0 Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid katika Nusu Fainali ya kwanza na Real inaingia Fainali kwa mara ya kwanza baada ya miaka 12, ambako itakutana na ama Chelsea au majirani zao Atletico Madrid ya Hispania pia.
Shujaa wa Real alikuwa ni Sergio Ramos aliyefunga mabao mawili, la kwanza dakika ya 16 pasi ya Luka Modric na la pili dakika ya 20 pasi ya Pepe kabla ya Mwanasoka wa Bora Dunia, Cristiano Ronaldo kumaliza kazi kwa kufunga mabao mawili dakika ya 34 pasi ya Gareth Bale na dakika ya 89.
Bayern Munich: Neuer, Lahm, Dante, Boateng, Alaba, Schweinsteiger, Kroos, Ribery/Gotze dk73, Muller/Pizarro dk73 na Robben, Mandzukic/Martinez dk46.
Real Madrid: Casillas, Carvajal, Pepe, Ramos/Varane dk75, Coentrao, Alonso, Modric, Di Maria/Casemiro dk84, Ronaldo, Bale na Benzema/Isco dk80.

No comments

Powered by Blogger.