MASSACRE (MAUAJI YA HALAIKI) SEHEMU 02
Judith akaanza kupiga
hatua kukifuata kiti cha wageni na kisha kutulia huku kikiwa mbele ya meza ile pale
ofisini. Judith hakuongea kitu chochote kile, alibaki akimwangalia mchungaji
kwa kutumia macho ambayo yalionyesha mshtuo mkubwa kwa mchungaji Matimya.
Mchungaji Matimya akasimama na kuanza kumsogelea Judith ambaye alibaki kimya
akijifikiria namna ya kufanya kile ambacho alitakiwa kukifanya kwa wakati ule.
“Kuna nini tena judith?” Mchungaji Matimya
alimuuliza Judith.
“Nina kiu mchungaji” Judith alijibu.
“Kiu ya Neno la Mungu au?”
“Hapana. Nina kiu ya penzi lako” Judith alijibu huku akionekana kutokujiamini.
Mchungaji Matimya akapigwa na mshtuko, jibu
ambalo lilitoka mdomoni mwa Judith lilionekana kumshtua kupita kawaida. Hakujua
kama masikio yake yalikuwa yamesikia vibaya au yalikuwa yamesikia kitu halisi
ambacho kilikuwa kimetoka mdomoni mwa Judith.
Akaanza kumwangalia Judith mara mbili mbili
kana kwamba hakuwa amekielewa kile ambacho alikuwa amekisikia kutoka mdomoni
mwa Judith. Uso wa Judith haukuonekana kutania hata kidogo, alionekana
kumaanisha kile ambacho alikuwa akikiongea kwa wakati ule.
Huku akionekana kutokujua ni kitu gani
ambacho alitakiwa kufanya kwa wakati ule, akashtuka mara baada ya kumuona
Judith akianza kuvua nguo zake katika kasi ambayo ilionekana kumshangaza.
Mikono ya Judith ikapata nguvu ya ziada,
akamvuta mchungaji Matimya na kisha kuanza kulivua shati lake ambapo
likafunguka huku baadhi ya vifungo viking’oka. Mchungaji Matimya alijaribu
kuleta purukushani za kutaka kujiondoa mikononi mwa Judith lakini hakufanikiwa.
“Niachie…niach…..” Mchungaji Matimya
alimwambia Judith lakini hata kabla hajamalizia sentensi yake, akasukumwa na
Judith ambaye alianza kupiga kelele za kuomba msaada huku akiifungua blauzi
yake na kuyaacha matiti yake nje. Judith hakuona kuridhika, akaanza kuipandisha
sketi yake juu ya kuyaacha mapaja yake wazi.
“Ananibakaaaaaa…..ananibakaaaaa…..” Judith
alipiga kelele huku akimsogelea mchungaji ambaye alionekana kuwa kama mtu
aliyechanganyikiwa. Kwa kasi kubwa Judith akamvuta mchungaji na kisha kumuweka
katikati ya mapaja yake na kisha kuibana miguu yake huku kelele za kubakwa
zikiendelea kusikika.
Ghafla mlango wa ofisi ile ukafunguliwa na
wazee wa kanisa kuingia. Picha ambayo ilionekana ndani ya ofisi ile ilionekana
kumshtua kila mtu. Judith alikuwa amelala juu ya meza huku mchungaji Matimya
akiwa katikati ya mapaja yake yaliyokuwa wazi.
“Yesu wangu!” Mzee kiongozi wa kanisa hilo,
Bwana Onesmo alijikuta akisema huku akiiweka mikono yake kichwani. Mara baada
ya Judith kuona kwamba wazee wa kanisa walikuwa wamefika ndani ya ofisi ile na
kuliona tukio lile, hapo hapo akajitoa na kuelekea pembeni huku akijitahidi
kuyafunika matiti yake.
“Mchungaji! Umefanya nini?” Mzee Sule
aliuliza kwa mshtuko.
Mchungaji Matimya hakutoa jibu lolote lile,
alibaki kimya huku akimwangalia Judith usoni. Judith alikuwa akilia huku
mashavu yake yakiwa yameloanishwa na machozi ambayo yalikuwa yakimtoka.
Mchungaji Matimya hakuelewa ni kitu gani ambacho alitakiwa kuongea ili aeleweke
kwa wazee wa kanisa kwamba hakuwa amefanya kile kitu ambacho Judith alikuwa
akikisema kwa wakati ule.
Muonekano wa Judith ambao alikuwa nao ndio
ambao ulikuwa ukiwahakikishia wazee wa kanisa kwamba mchungaji Matimya alikuwa
amefanya kile ambacho Judith alikuwa akikisema kwa wakati huo.
Sketi yake ilikuwa imechanika na kuyafanya
mapaja yake kuwa nje. Blauzi yake ambayo alikuwa ameivaa ilikuwa imeng’olewa
vifungo na kuyafanya matiti yake kuwa nje. Kila mtu alimwamini Judith juu ya
kile ambacho alikuwa akikisema kwa wakati ule.
Muda wote huo mchungaji Matimya alibaki
kimya huku akiwa hafahamu ni kitu gani ambacho alitakiwa kufanya. Alionekana
kuchanganyikiwa.
****
Katika kipindi chote mchungaji Matimya
hakuonekana kuwa na furaha, kila wakati alikuwa mtu wa majonzi tu. Skendo ya
kutaka kubaka ambayo ilikuwa imemkuta ndio ambayo ilichangia kuwa katika hali
hiyo ya majonzi. Katika vipindi vyote ambavyo alipitia katika maisha yake,
kipindi hicho ndicho kilionekana kuwa kuwa kipindi kigumu kuliko vipindi vyote
maishani mwake.
Mara kwa mara alikuwa akijifungua chumbani
akisali, alijiona kuwa kama mtu mwenye dhambi mbele za Mungu. Shetani
alionekana kupewa nafasi ya kumjaribu.
Kila wakati alikuwa akisali huku machozi yakimtiririka, alilia kupita
kiasi, hakuona msaada wowote mbele yake, alijiona kuwa kama mtu aliyetengwa
pasipo msaada wowote ule.
Marafiki zake wote aliokuwa nao walionekana
kuwa kama kumtenga. Familia yake ndio ambayo ilionekana kuwa kila kitu katika
maisha yake, hiyo ndio ilikuwa furaha yake, upendo wake na faraja yake kuu.
Mchungaji Matimya hakupewa nafasi yoyote ya kujitetea, kila mtu alimuona kuwa
mtu maalum ambaye aliitwa kanisani kwa ajili ya kuliharibu kanisa.
Kanisani akawa akikaa katika viti vya nyuma
pamoja na familia yake. Washirika wa kanisa hilo hawakuwaonyeshea upendo tena,
kila mtu alionekana kuichukia familia hiyo. Tukio ambalo lilikuwa limetokea
katika maisha yake lilionekana kutaka kuiyumbisha imani yake siku za usoni.
Kila ibada ilipokuwa ikiisha, hakutaka
kubaki kanisani hapo zaidi ya kuingia ndani ya gari na kuondoka pamoja na
familia yake.
Kila siku moyo wake ulikuwa na majonzi,
furaha kwake ikapotea, majonzi yakautawala moyo wake. Mara kwa mara alikuwa
akifikiria sababu zilizompelekea Judith kufanya kitendo kama kle ndani ya ofisi
yake. Hakufikiria hata mara moja kama mchungaji Mwakipesile alikuwa nyuma ya
tukio zima.
Ndani ya gari kila mtu alikuwa kimya huku
wote wakionekana kuwa na mawazo vichwani mwao. Vitendo ambavyo vilikuwa
vikifanywa na washirika wa kanisa lile ndivyo ambavyo vilikuwa vikiwaumiza.
Ukaribu ambao ulikuwepo kati yao na washirika wa kanisa lile ukaonekana
kupotea. Familia nzima ilionekana kutenda dhambi isiyoweza kusameheka mbele za
Mungu.
“Siamini kama kanisa linaweza kufanya kitu
kama hiki, yaani upendo wao wote umepotea, upendo ambao walikuwa nao kabla
umepotea kabisa” Mzee Matimya alisema huku akionekana kuwa na majonzi.
“Nafikiri Mungu anataka kuipima imani y….”
Bi Meriana alisema lakini hata kabla hajamalizia sentensi yake, Benedict
akaingilia.
“Silifikirii hilo mama. Hapa kuna kitu, ni
lazima kutakuwa na mtu aliyefanya mpango huu” Benedict alisema huku mikono yake
ikiwa imeshikiria usukani.
“Hakuna mpango wowote Bened…..”
“Usiseme hivyo baba. Sisi kama binadamu tuna
udhaifu. Unaweza kukuta hata wachungaji wengine wamehusika katika hili” Benedict
alisema huku akionekana kukasirika.
“Usiseme maneno hayo juu ya watumishi wa
Mungu, Benedict”
Benedict hakutaka kuendelea kuongea kitu
chochote kile kwani kila alipokuwa akiongea na ndivyo ambavyo hasira
zilivyozidi kumpanda. Hakutaka kuwa na mapenzi yoyote na washirika wa kanisa la
Praise And Worship. Alimchukia kila mtu kanisani. Akili yake haikukubaliana na
kanisa kama kweli baba yake aliweza kufanya kitu kama kile. Alijua fika kwamba
Judith alikuwa amefanya kitu kile kwa sababu ya kitu fulani.
“Kuna mtu nyuma ya Judith” Benedict alisema
mara baada ya ukimya kutawala kwa muda mrefu garini mule.
Kila mtu akabaki akimwangalia Benedict
ambaye alikuwa akitingisha kichwa chake juu na chini kuashiria kwamba alikuwa
na uhakika juu ya kile ambacho alikuwa akikiongea katika kipindi kile.
“Kuna
mtu? Mtu gani?” Bi Meriana aliuliza huku akionekana kushangaa.
“Simfahamu ni mtu gani lakini nafikiri mtu
huyo atakuwa miongoni mwa wachun…”
“Benedict…..” Mzee Matimya aliita kwa sauti
iliyojaa hasira ambayo ilimfanya Benedict kunyamaza.
*****
Mzee Matimya alibaki katika chumba chake cha
kusalia. Macho yake yalikuwa yakiiangalia Biblia yake iliyokuwa juu ya meza.
Aliiangalia kwa kipindi kirefu bila kufanya kitu chochote kile. Alitamani
kuanza sala yake kama siku nyingine ambavyo alivyokuwa akifanya lakini kila
alipojaribu kupiga magoti chini, aliiona miguu yake ikiishiwa nguvu.
Aliendelea kutulia juu ya kiti ndani ya
chumba kile. Alijikuta akipata nguvu mpya, akaipeleka mikono juu ya meza ile,
akaichukua Biblia ile na kuifungua. Akaanza kusoma baadhi ya maandiko ambayo
aliyaona yakimfariji. Ghafla macho yake yakaanza kujaa machozi ambayo baada ya
muda fulani yakaanza kutiririka mashavuni mwake.
Nguvu za kuendelea kusoma Biblia zikatoweka.
Akaifunika Biblia na kuyaelekeza macho yake darini. Alijiona kuwa peke yake,
tumaini lote likatoweka, hasira zikaanza kumpanda kila kila alipokuwa
akimfikiria Judith.
Aliendelea kubaki katika hali ile kwa dakika
kadhaa, mara akashtuka baada ya simu yake kuanza kuita. Akaupeleka mkono wake
mfukoni na kuitoa simu ile na kuanza kukiangalia kioo cha simu ile. Namba
ambazo zilionekana katika kioo cha simu ile zilikuwa ngeni machoni mwake.
Hakutaka kujali sana, alichoifanya ni kuipeleka simu ile sikioni na kuanza
kuongea.
“Bwana Yesu Asifiwe mchungaji” Sauti ya
upande wa pili ilisikika.
Mzee Matimya hakuitikia chochote kile.
Kichwa chake kikaanza kujaza maswali juu ya mpigaji wa simu ile. Taarifa
zilijulikana Tanzania nzima kama katika
kipindi hicho hakuwa mchungaji tena mara baada ya kuvuliwa uongozi huo. Ni nani
alikuwa akiongea upande wa pili? Je alikuwa ni rafiki yake ambaye walipotezana
kipindi kirefu kilichopita au alikwa mtu mwingine?
“Mchungaji……” Sauti ya upande wa pili iliita
mara baada ya kuona ukimya umetawala kwa kipindi kirefu.
“Amen….Amen…Nani anaongea?” Mchungaji
aliitikia na kuuliza swali huku akionekana dhahiri kutokumjua mpigaji wa simu
ile.
“Ni mimi Patrick. Patrick Chonya. Umenisahau
mchungaji?”Sauti ya upande wa pili ilisikika
Mzee Matimya akaonekana kupatwa na mshtuko,
ghafla tabasamu likaanza kuonekana usoni mwake. Kila kitu ambacho kilitokea
katika maisha yak kilionekana kusahaulika kwa muda. Alimfahamu sana Patrick,
kijana ambaye alikuwa mshirika wake kabla ya kuhamia jijini Mwanza. Alisafiri
miaka miwili iliyopita kuelekea nchini Marekani kwa ajili ya kusomea udaktari
wa mifupa.
“Mungu wangu! Umerudi lini kutoka Marekani?”
Mzee Matimya aliuliza huku akionekana tabasamu likiendelea kuwepo usoni mwake.
“Leo hii ndio nimekanyaga ardhi ya Tanzania.
Njoo hapa uwanja wa ndege mchungaji. Nataka kukuachia mizigo yako kutoka kwa
mchungaji Macbeth Lewis. Nataka kuchukua ndege kuelekea Mwanza” Sauti ya upande
wa pili ilisikika.
Tabasamu likaongezeka zaidi na zaidi usoni
mwa mzee Matimya. Hakuamini kama mchungaji Macbeth kutoka nchini Marekani ndani
ya jiji la Atlanta angeweza kumkumbuka kwa kumletea zawadi kwani kilipita
kipindi kirefu sana tangu mchungaji Macbeth aje nchini Tanzania na kuhubiri
ndani ya kanisa lake.
Kwa haraka haraka akakata simu na kuanza
kujiandaa. Moyo wake ulirejewa na furaha, kila kitu ambacho kilikuwa
kinaendelea katika maisha yake alikiona kuwa kama mpango wa Mungu katika
kudhihirisha kwamba bado alikuwa pamoja nae. Mara baada ya kumaliza kujiandaa,
akatoka na kuanza kuelekea uwanja wa ndege huku tayari ikiwa imetimia saa kumi
na mbili jioni.
*****
Muda ulizidi kwenda mbele lakini wala
mchungaji Matimya hakurudi nyumbani. Kila mtu alionekana kuwa na wasiwasi kwani
hali ile haikuonekana kuwa ya kawaida kutokea. Mara kwa mara Bi Meriana
alijaribu kumpigia simu mchungaji Matimya lakini simu haikupatikana.
Bi Meriana hakukata tamaa, bado aliendelea
kumpigia simu mume wake lakini majibu yalikuwa yale yale, simu haikupatikana.
Amani ikatoweka moyoni mwake, mashaka yakaanza kumjaa, mara kwa mara Bi Meriana
alikuwa akiikodolea macho saa yake, masaa yalikuwa yakiendelea kusonga mbele
lakini wala mzee Matimya hakurudi nyumbani.
Bi Meriana akashindwa kuvumilia, akasimama
na kuanza kuelekea sebuleni, alipofika, akatulia kochini huku macho yake
yakiangalia darini hali iliyoonyesha kwamba alikuwa na mawazo katika kipindi
hicho. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo alizidi kuwa na
wasiwasi zaidi.
“Mungu wangu! Saa sita!” Bi Meriana aliasema
hali iliyofanya Benedict ambaye alikuwa sebuleni pale kushtuka.
“Mbona umeshtuka hivyo?” Benedict
alimuuliza.
“Baba yako”
“Amefanya nini?”
“Hajarudi”
“Toka aliyoondoka saa kumi na mbili?”
“Ndio”
Benedict akaacha kufanya kazi ambayo alikuwa
akiifanya na kisha kuanza kumsogelea mama yake. Alipomfikia, akajiweka karibu
nae na kuchomoa simu yake na kisha kuanza kumpigia baba yake, mzee Matimya.
Simu ilikuwa vile vile, mawasiliano hayakupatikana kabisa hali ambayo ikaanza
kuibua wasiwasi moyoni mwa Benedict.
Simu mbalimbali zikaanza kupigwa kwenda kwa
ndugu, jamaa na marafiki ili kujua kama mzee Matimya alikuwa huko lakini
hawakufanikiwa kumpata. Wasiwasi ukaongezeka maradufu mioyoni mwao, kitu cha
hatari kilionekana kumtokea mzee Matimya kwani halikuwa jambo la kawaida kitu
kama hicho kutokea.
“Kwa hiyo tufanye nini?” Benedict alimuuliza
mama yake.
“Labda tupige simu pol….” Bi Meriana alisema
lakini hata kabla hajamalizia sentensi yake, simu yake ya mkononi ikaanza
kuita. Kwa haraka haraka akayapeleka macho yake katika kioo cha simu ile. Mara
ya kwanza alifikiri kwamba mpigaji wa simu ile alikuwa mumewe, lakini mara baada
ya kuangalia kioo cha simu yake, namba ilikuwa ngeni.
“Hallooo…! Wewe ni mke wa mchungaji?” Sauti
ya upande wa pili ilisikika ikiuliza swali kwa sauti ya juu hata kabla ya
salamu. Bi Meriana hakujibu chochote kile, alibaki kimya kwa muda kama mtu
ambaye alikuwa akijifikiria namna ya kulijibu swali lile.
“Haloo..! Upo hewani?”
“Ndio”
“Basi njoo hapa kituo cha polisi haraka
iwezekanavyo”
“Kituo gani?” Bi Meriana aliuliza huku
akionekana kuwa na wasiwasi.
“Mbezi kwa Yusufu” Sauti ya upande wa pili
ilijibu na simu kukatwa.
Bi Meriana akabaki kimya huku simu
ikiendelea kuwa masikioni mwake japokuwa simu ile ilikuwa imekatwa. Mwili wake
ukaanza kumtetemeka huku miguu yake akiiona ikifa ganzi. Hakuendelea kubaki
katika hali hiyo zaidi, machozi yakaanza kumtoka.
“Mama. Nini tena?” Benedict aliuliza mara
baada ya kumuona mama yake akiwa kimya muda mrefu.
“Kituo cha polisi Mbezi kwa Yusufu”
“Kimefanya nini?” Benedict aliuliza huku
akionekana kushangaa.
“Twende” Bi Meriana alisema.
Hakukuwa na sababu yoote kubaki mahali hapo,
kwa haraka haraka wakachomoka kutoka ndani na moja kwa moja kuelekea nje ambako
wakaingia ndani ya gari na kuanza safari ya kuelekea katika kituo cha polisi
cha Mbezi kwa Yusufu. Machozi yakaanza kumtoka Bi Meriana huku sauti ya kilio
cha chini chini kikianza kusikikika.
Simu ile ambayo aliipokea muda mchache
uliopita ilionekana kumchanganya, tayari alikwishajua kwamba kulikuwa na kitu
ambacho kilikuwa kimetokea. Maswali mfululizo yakaanza kumiminika kichwani
mwake. Katika kipindi cha nyuma mzee Matimya aliaga kwamba alikuwa akielekea
uwanja wa ndege ambako alikuwa akihitajika, kwa nini simu ilipigwa kutoka
Mbezi? Tena mbaya zaidi katika kituo cha polisi.
Kutokana na kutokuwa na foleni ya magari, walitumia
dakika thelathini mpaka kufika Mbezi kwa Yusufu. Moja kwa moja wasimamisha gari
lao nje ya kituo kile cha polisi na kisha kuelekea katika kituo hicho.
“Karibuni” Polisi mmoja ambaye alikuwa zamu
aliwakaribisha mara baada ya kuwaona.
“Kuna nini afande?” Mume wangu yuko wapi?”
Bi Meriana aliuliza maswali mawili mfululizo hata kabla ya salamu. Sauti ya
kilio cha chini ikaanza kusikika kutoka kwa Bi Meriana. Kitendo cha swali lake
kutokujibiwa ndicho ambacho kilionekana kumtia wasiwasi.
“Nini kinaendelea?” Benedict alivunja ukimya
kwa kuuliza swali.
“Ni taarifa za masikitiko sana. Kitu ambacho
kimetokea kimeonekana kumshangaza kila mtu” Polisi alisema mara baada ya
kuchukua maelezo ya Benedict na Bi Meriana na kisha kuendelea.
“Mlisema aliondoka toka saa kumi na mbili
kuelekea uwanja wa ndege?” Polisi aliuliza.
“Ndio”
“Alirudi baada ya kuondoka?”
“Hapana”
Polisi hakutaka kuendelea kuuliza maswali,
akainuka kutoka pale kaunta na kuanza kuelekea katika chumba kimojawapo kati ya
vyumba ambavyo vilikuwa ndani ya kituo kile ambapo baada ya sekunde kadhaa,
polisi mwingine ambaye alikuwa mahali pale nae kuingia ndani ya kile chumba.
“Nini kinaendelea afande?” Benedict aliuliza
mara baada ya polisi wale kurudi kaunta.
“Jambo hili bado linafanyiwa uchunguzi”
“Uchunguzi? Uchunguzi gani?”
“Uchunguzi juu ya kifo chake” Polisi alijibu
huku akionekana kuwa na wasiwasi.
Jibu lile likaonekana kumchanganya kila
mmoja, Bi Meriana akaanza kulia kwa uchungu. Neno ‘kifo’ ambalo lilitamkwa na polisi yule ndilo ambalo lilionekana
kumuumiza. Wala hakuchukua hata dakika moja kuwa katika hali ile, macho yake
yakaanza kuona giza ambapo baada ya sekunde chache akaanguka na kupoteza
fahamu.
****
Maturubai zaidi ya matano yalikuwa yamefungwa
katika eneo la nyumba ya mzee Matimya. Idadi ya watu ambao walikuwa
wamehudhuria msibani hapo wala haikuwa kubwa kama jinsi ambavyo ilitarajiwa.
Ingawa wachungaji mbalimbali kutoka katika makanisa tofauti tofauti walikuwa
wamehudhuria msiba huo lakini wala hakukuwa na zaidi ya washirika watano kutoka
katika kanisa la Praise And Worship la Mwenge.
Watu wengi ambao walikuwa wamehudhuria
msibani pale walikuwa watu ambao wala hawakutoka mbali na eneo lile pamoja na
waandishi wa habari. Kanisa likaonekana kupunguza ukaribu, kitendo cha waumini
watano kuhudhuria katika msiba ule kilidhihirisha wazi kwamba mapenzi makubwa
juu ya mzee Matimya hayakuwepo tena katika mioyo ya waumini wa kanisa lile.
Vilio vya ndugu wa marehemu vilikuwa
vikisikika kutoka kila kona msibani hapo. Sehemu kubwa ya mikeka iliyokuwa
mahali hapo ilikuwa wazi jambo ambalo lilionekana kumshangaza kila mtu.
“Mbona washirika wa kanisa la Praise and
Worship hawaonekani hapa msibani?” Mchungaji Melek aliuliza kwa mshangao huku
akiangalia katika kila kona msibani hapo kana kwamba alikuwa akimtafuta mtu
fulani.
“Wote walikasirishwa na kitendo
kilichotokea. Mapenzi yao yakapotea. Mbaya zaidi, mzee Matimya alijinyonga”
Kijana mmoja alimjibu mchungaji Melek.
“Mungu wangu! Kumbe alijinyonga?”
“Ndio. Nafikiri alijiona kuwa mkosaji mbele
za Mungu wake” kijana yule alijibu.
Benedict alikuwa ametulia pembeni kidogo mwa
mchungaji Melek. Maneno yote aliyoyaongea mchungaji Melek na yule kijana
yalionekana kumuumiza kupita kiasi. Hapo hapo akanyanyuka na kuanza kuelekea
ndani ya nyumba yao.
Idadi kubwa ya wanawake ilikuwa ndani ya
nyumba hiyo. Benedict hakutaka kuongea chochote kile, kitu alichokifanya ni
kupiga hatua kuelekea chumbani kwake.
Akajilaza kitandani huku macho yake yakiangalia
juu, machozi yakaanza kumtoka. Benedict akazidi kushikwa na hasira juu ya
washirika wa kanisa la Praise and Worship lililokuwa Mwenge. Kadri ambavyo
alivyokuwa akilikumbuka kanisa hilo na ndivyo ambavyo hasira zake zilivyozidi
kuongezeka zaidi.
Huku Benedict akiwa katika hali hiyo
chumbani, mara mlango ukafunguliwa na Angelina kuingia. Macho ya Angelina
yalikuwa mekundu huku mashavuni akiwa na alama za michirizi ya machozi hali
iliyoonyesha kwamba kipindi fulani kilichopita alikuwa akilia. Angelina akaanza
kupiga hatua mpaka pale kitandani alipokuwa amejilaza Benedict.
“Najiona kama tumetengwa” Angelina
alimwambia Benedict kwa sauti ya chini iliyojaa majonzi.
“Mapenzi yao yamepotea kabisa. Ukaribu wao
hauonekani, ni lazima nifanye kitu juu ya kanisa hili” Benedict alimwambia
Angelina huku akionekana kuwa na hasira.
“Kitu gani?”
“Niwaue. Ni lazima niwaue washirika wote wa
kanisa lile. Hasa Judith” Benedict alisema.
“Usifanye hivyo Benedict”
“Haina jinsi, nataka kurudisha furaha yangu
iiyopotea” Benedict alisema huku akichukua kitambaa chake cha mkononi na
kujifuta machozi yaliyokuwa yakimtoka.
Ukimya mrefu ukatawala mahali hapo huku kila
mtu akionekana kufikiria lake. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo
ambavyo hasira za Benedict zilivyozidi kumkamata. Hakulipenda kanisa la Praise
And Worship lililokuwa Mwenge, hakumpenda mshirika yeyote ndani ya kanisa lile,
kila mtu alionekana kuwa adui namba moja katika maisha yake.
Huku kila mmoja akifikiria lake, mara simu
ya mkononi ya Benedict ikaanza kuita, akaitoa kutoka mfukoni. Kabla hajapokea,
akayapeleka macho yake katika kioo cha simu ile, macho yake yakatua katika
namba ambayo ilikuwa ngeni machoni mwake. Akabonyeza kitufe cha kijani na kisha
kuipeleka sikioni.
“Upo wapi Benedict? Mbona sikuoni hapa nje?”
Sauti ya upande wa pili ilisikika ikiuliza.
“Wewe nani?” Benedict aliuliza.
“Mkuu wa polisi kitengo cha upelelezi”
Benedict hakutaka kuongea kitu chochote
kile, akakata simu, akainuka kitandani na kuanza kuelekea nje. Alipofika nje,
akaanza kuangalia katika kila upande. Macho yake yakatua katika uso wa mwanaume
mmoja aliyekuwa na ndevu nyingi ambaye alimuonyeshea ishara ya kumuita. Benedict
akaanza kupiga hatua kumfuata mwaname yule.
“Hebu tusogee pembeni kidogo” Mwanaume yule
alimwambia Benedict na kuanza kusogea pembeni. Hata kabla mzee yule hakuongea
chochote, akatoa kitambulisho chake na kumuonyeshea Benedict.
“Uchunguzi wenu umeishia wapi?” Benedict
aliuliza.
“Kwamba baba yako hakujinyonga”
“Unasemaje?”
“Huo ndio ukweli. Hakujinyonga bali
alinyongwa”
“Umejuaje?”
Unataka niwe nakutumia CHOMEZO watu 200 wa
kwanza kulike PAGE YA 2JIACHIE Mtatumiwa imbox chomezo LIKE PAGE YETU
HAPA ==>www.facebook.com/2jiachie
ITAENDELEA KESHO HAPA HAPA
Post a Comment