ad

ad

NYOTA 9 WAYEYUKA MAZOEZINI SIMBA


WACHEZAJI tisa wa Simba walishindwa kufika mazoezini kwenye Uwanja wa Kinesi, Shekilango jijini Dar, jana kutokana na sababu tofauti ikiwemo ya majeraha na matatizo ya kifamilia.
 
Donald Musoti.
Wachezaji hao ni Amissi Tambwe ambaye ana jeraha kichwani, Zahoro Pazzi ambaye ana tatizo la enka na Gilbert Kaze anayesumbuliwa na goti.
Wengine ambao ni majeruhi ni: Donald Musoti, Betram Mwombeki, Said Ndemla, Abubakari Hashimu, Uhuru Selemani na Abdulhalim Humud ambapo wote hawa wawili wana matatizo ya kifamilia.
 
Uhuru Selemani.
Kocha Mkuu wa Simba, Zdravok Logarusic, amesema asilimia kubwa ya kikosi chake ni majeruhi ndiyo maana hawaonekani mazoezini hapo kwa siku kadhaa.
“Ninaamini wachezaji wote hao tutakuwa nao pamoja tutakapoanza mazoezi Jumatatu,” alisema Loga.
Powered by Blogger.