KOCHA RAIA WA UINGEREZA AIPA YANGA MBINU ZA KUING’OA AL AHLY
ALIYEKUWA Kocha Mkuu wa Azam, Stewart Hall, raia wa Uingereza, ameibuka na kuielekeza Yanga cha kufanya kama kweli inataka kuiondoa Al Ahly ya Misri kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Yanga inatarajiwa kuumana na mabingwa hao watetezi kwenye mchezo wa hatua ya pili ya michuano hiyo baada ya kuifunga Komorozine ya Comoro kwa jumla ya mabao 12-2.
Hall alisema kwamba ni lazima Yanga ishinde kwenye mchezo wa kwanza utakaopigwa Uwanja wa Taifa, Dar kwa idadi nyingi ya mabao kwa ajili ya kupunguza mzigo watakapokwenda kwenye mechi ya marudiano.
Alisema kuwa endapo Yanga itafanikiwa kufanya hivyo itakuwa na faida kwa kuwa mara nyingi Waarabu hao ni wagumu kuwafunga wakiwa kwao, hivyo hata wakijitahidi kupata matokeo ya sare yoyote itaweza kuwasaidia.
Aidha, aliwasihi pia kuwa waangalifu na makini kwa timu hiyo ambayo ni ngumu hapa Afrika huku akiwataka watumie nafasi hiyo kwa ajili ya kujitangaza zaidi hapa Afrika na sehemu nyingine duniani kote.
“Yanga wanakutana na timu ngumu, cha msingi ni kujipanga zaidi kwenye mechi hii ya kwanza ya nyumbani, inabidi wapate ushindi mzuri kwa sababu kila mtu analijua hilo kwamba Al Ahly ni wagumu kuwafunga kwao, wakiweza kufanya hivyo watakuwa na faida kubwa.
“Lakini pia wawe makini kwa vitu viwili, kwanza wawe makini sana na hawa jamaa kwani hawatabiriki kabisa wanapokuwa uwanjani, lakini pia ni muda wao muafaka wa kujitangaza kwa sababu hizi timu za Kaskazini mwa Afrika huwa zinafuatiliwa sana Ulaya, hivyo endapo itafanya vema itakuwa faida nyingine tena kwao na mchezaji mmoja-mmoja,” alisema Hall.
Yanga inatarajiwa kuumana na mabingwa hao watetezi kwenye mchezo wa hatua ya pili ya michuano hiyo baada ya kuifunga Komorozine ya Comoro kwa jumla ya mabao 12-2.
Hall alisema kwamba ni lazima Yanga ishinde kwenye mchezo wa kwanza utakaopigwa Uwanja wa Taifa, Dar kwa idadi nyingi ya mabao kwa ajili ya kupunguza mzigo watakapokwenda kwenye mechi ya marudiano.
Alisema kuwa endapo Yanga itafanikiwa kufanya hivyo itakuwa na faida kwa kuwa mara nyingi Waarabu hao ni wagumu kuwafunga wakiwa kwao, hivyo hata wakijitahidi kupata matokeo ya sare yoyote itaweza kuwasaidia.
Aidha, aliwasihi pia kuwa waangalifu na makini kwa timu hiyo ambayo ni ngumu hapa Afrika huku akiwataka watumie nafasi hiyo kwa ajili ya kujitangaza zaidi hapa Afrika na sehemu nyingine duniani kote.
“Yanga wanakutana na timu ngumu, cha msingi ni kujipanga zaidi kwenye mechi hii ya kwanza ya nyumbani, inabidi wapate ushindi mzuri kwa sababu kila mtu analijua hilo kwamba Al Ahly ni wagumu kuwafunga kwao, wakiweza kufanya hivyo watakuwa na faida kubwa.
“Lakini pia wawe makini kwa vitu viwili, kwanza wawe makini sana na hawa jamaa kwani hawatabiriki kabisa wanapokuwa uwanjani, lakini pia ni muda wao muafaka wa kujitangaza kwa sababu hizi timu za Kaskazini mwa Afrika huwa zinafuatiliwa sana Ulaya, hivyo endapo itafanya vema itakuwa faida nyingine tena kwao na mchezaji mmoja-mmoja,” alisema Hall.

Post a Comment