Bodi ya Ligi yaionya Yanga
Dar es Salaam.
Bodi ya Ligi Kuu imewapiga mkwara uongozi na wanachama wa
Klabu ya Yanga kutothubutu kufanya hujuma kwenye mitambo ya Kituo cha
Televisheni cha Azam.
Mkurugenzi wa Bodi hiyo, Silas Mwakibinga
alisema kuwa atakayehusika kwa namna yoyote kufanya vurugu au hujuma,
hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.
Mwakibinga alisema vyombo vya
usalama vimejiandaa kutoa ulinzi mkali uwanjani hapo na kwamba
wataofanya vurugu watakamatwa na kufikishwa mahakamani.


Post a Comment