ad

ad

AMANDA: MWAKA 2013 ULIKUWA MAJANGA KWANGU

 MWANADADA kutoka kiwanda cha filamu Bongo, Tamrina Poshi ‘Amanda’ amefunguka kuwa mwaka 2013 ulikuwa majanga kwake kwani ulikuwa mgumu sana na mambo yake hayakumwendea vizuri.
 
Akichonga Amanda alisema bora mwaka huu upite, kwani ulikuwa mgumu sana kwa upande wake  katika mambo f’lani ambayo hakutaka kuyataja ila anaamini kuwa mwaka ujao utakuwa mzuri kwake kwani ameshaanza kuona dalili za mafanikio mapema.

“Mwaka 2013 ulikuwa mgumu kwangu, ila nashukuru unaisha, ninaamini huo ujao utakuwa mzuri na wa mafanikio kwangu kwani nimeshaanza kuona dalili nzuri, suala la kuolewa halipo kichwani kwani hata sina mwanaume kwa sasa, ninawaza tu jinsi ya kupata fedha kwa kufanya kazi kwa bidii,” alisema Amanda.


AMANDA POSHY KATIKA POZI
Powered by Blogger.