ad

ad

SIR ALEX FERGUSON ALIMWAGA MACHOZI WAKATI ANAWAAMBIA WACHEZAJI WAKE KUSTAAFU KUWAFUNDISHA!



Sir Alex anatajwa kuwa ndiye meneja mwenye mafanikio makubwa katika historia ya soka la Uingereza.
Mabingwa wa Ligi Kuu nchini England, Manchester United wametangaza kwamba, Sir Alex Ferguson atastaafu kama meneja wa klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.

Tangu alipojiunga na klabu hiyo mnamo mwaka 1986, ameshinda mataji mawili (2) ya Klabu Bingwa Barani Ulaya, mataji kumi na tatu(13) ya Ligi Kuu ya England na Kombe la FA mara tano(5).

Katika taarifa yake, Sir Alex amesema ni muda muafaka kwake kustaafu wakati klabu ikiwa imejizatiti katika nafasi nzuri.
Ferguson atabakia Manchester United kama mmoja wa wakurugenzi na balozi.

Watu mbalimbali wamekuwa wakitoa salamu za kumtakia kheri, miongoni mwao akiwemo Waziri Mkuu wa Uingereza,David Cameron na wanasiasa mbalimbali pamoja na mashabiki na wachezaji wa zamani wa Uingereza na Manchester United. 

Hofu imetanda miongoni mwa mashabiki wa Manchester United ambao wamekuwa wakijiuliza maisha yatakuwaje bila ya Sir Alex Ferguson kwenye klabu hiyo yenye mashabiki wengi Ulimwenguni.


MAFANIKIO YA ALEX FERGUSON
MATAJI 49 YA FERGIE…
Sir Alex Ferguson ameshinda mataji 49 akiwa kocha mwenye mafanikio zaidi Uingereza…
ST MIRREN
Daraja la Kwanza Scotland (1): 1976-77.
ABERDEEN
Ligi Kuu Scotland (3): 1979-80, 1983-84, 1984-85.
Kombe la Scotland (4): 1981-82, 1982-83, 1983-84, 1985-86.
Kombe la Ligi Scotland (1): 1985-86.
Kombe la Washindi Ulaya(1): 1982-83.
Super Cup ya Ulaya (1): 1983.Ferguson cradles the FA Cup in 1990. He would get his hands on many more trophies...
Ferguson kisses the European Cup-Winners' Cup after victory in 1991
Eric Cantona (right) was possibly Ferguson's most important acquisition
MANCHESTER UNITED
Ligi Kuu England (13): 1992-93, 1993-94, 1995-96, 1996-97, 1998-99, 1999-2000, 2000-01, 2002-03, 2006-07, 2007-08, 2008-09, 2010-11, 2012-13.
Kombe la FA (5): 1989-90, 1993-94, 1995-96, 1998-99, 2003-04.
Kombe la Ligi Cup (4): 1991-92, 2005-06, 2008-09, 2009-10.
Ngao ya Jamii/Hisani (10): 1990 (shared), 1993, 1994, 1996, 1997, 2003, 2007, 2008, 2010, 2011.
Ligi ya Mabingwa Ulaya (2): 1998-99, 2007-08.
Kombe la Washindi Ulaya (1): 1990-91.
Super Cup ya Ulaya(1): 1991.
Kombe la Mabara(1): 1999.
Klabu Bingwa ya Dunia (1): 2008.


Ferguson watches his first United game, a defeat by Oxford in 1986
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 71 anajiandaa kuaga umati wa mashabiki Uwanja wa Old Trafford Jumapili baada ya mechi ya United dhidi ya Swansea, wakati watakapokabidhiwa taji la ubingwa wa Ligi Kuu England, hilo likiwa la 13 chini ya Ferguson.
Mazungumzo yanaendelea kumsaka mrithi wake na kocha wa Everton, David Moyes ni miongoni mwa wanaopewa nafasi. 

CRISTIANO RONALDO APANDIWA NDEGE NA DAVID GILL SPAIN.


Christiano Ronaldo akiwa ameshika Kombe enzi akiichezea Manchester United.
Mtendaji mkuu wa klabu ya Man Utd David Gill ameshindwa kuficha hisia na kuamua kumpandia ndege kwenda kuzungumza na Ajenti wake huko Hispania juu ya mshambuliaji kutoka nchini Ureno Cristiano Ronaldo ambaye bado anaendelea kuhusishwa na mpango wa kurejea old Trafford.

David Gill ameshindwa kuficha hisia za kumuona mshambuliaji huyo akirejea katika himaya ya Mashtamni wekundu, alipohojiwa na kituo cha televisheni cha Sky Sports ambapo amesema si vibaya endapo ronaldo atarejea katika utawala wao. 

Amesema Cristiano Ronaldo ni mchezaji mzuri na mwenye hadhi ya kuitumikia klabu ya Man Utd ambayo ilimuuza mwaka 2009, baada ya kuonyesha uwezo mzuri ambao uliwavutia Real Madrid na kukubalia kutoa kiasi cha paund million 80 kama adayake ya uhamisho. 

Gill amesema hatoshangazwa na mpango wa Ronaldo endapo utatua mezani kwake kwa ajili ya kusajiliwa kwa mara nyingine tena, hivyo amesisitiza suala hilo kuachwa na kuamini bado mshambuliaji huyo ni bora kati ya wachezaji walio bora. 
Powered by Blogger.