ad

ad

Watu 50 wauawa katika milipuko kadhaa Iraq

Maafisa wa usalama na tiba wa Iraq wamesema kuwa, karibu watu 50 wameuawa na wengine 200 kujeruhiwa kufuatia milipuko kadhaa iliyotokea leo kwenye maeneo tofauti ya nchi hiyo.

Katika mji mkuu Baghdad, milipuko 6 ya kutegwa kwenye magari iliyolipuka katika vitongoji vitano vya mji huo imeua watu 8 na kujeruhi wengine karibu 50. 

Katika mji wa Tuz Khurmatu ulioko kilometa 175 kaskazini mwa Baghdad magari matatu yalilipuka na kuua watu 6 huku wengine 60 wakijeruhiwa. Milipuko kama hiyo imetokea pia kwenye miji ya Kirkuk, Hilla na Nasiriyah.
Milipuko hiyo imetokea nchini Iraq huku nchi hiyo ikijitayarisha nkwa ajili ya uchaguzi wa Bunge unaotarahiwa kufanyika tarehe 20 Aprili katika majimbo 12 kati ya 18 ya nchi hiyo. 
Powered by Blogger.