ad

ad

RAYUU: SIMU IMEVUJISHA PICHA ZANGU CHAFU.

Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Alice Bugenzi ‘Rayuu’ amejutia kitendo chake cha kupiga picha za utupu kwenye simu yake ya mkononi na kueleza kuwa, kuibiwa kwa simu hiyo ndiko kulikosababisha matatizo kwake na kwa familia yake.

Akifungukia suala hilo juzikati kupitia mtandao wa Facebook kwa lengo la kuomba msamaha kwa mashabiki, Rayuu alisema hakuwa na nia ya kujipiga picha hizo na kuzisambaza kwa lengo la kutafuta umaarufu ila ilitokea hivyo baada ya kupoteza simu yake ya mkononi.
 
“Mashabiki wangu naombeni msamaha kutokana na kusambaa kwa picha zangu chafu, tambueni kuwa haikuwa dhamira yangu bali ilitokea baada ya simu yangu ya mkononi kupotea,” alisema Rayuu.
Powered by Blogger.