ad

ad

Ivory Coast yaiomba UN iipatie ndege zisizo na rubani

Ivory Coast imeuomba Umoja wa Mataifa utumie ndege zisizo na rubani katika mpaka wa nchi hiyo na Liberia. Youssoufou Bamba, Balozi wa Ivory Coast katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa serikali ya nchi hiyo inauomba Umoja wa Mataifa utumie ndege zisizo na rubani ili kufuatilia harakati za makundi yenye silaha kwenye mpaka wa nchi hiyo na Liberia.


 Bamba amesema utumiaji wa ndege zisizo na rubani katika maeneo ya mpaka wa Ivory Coast na Liberia utawazidishia uwezo askari jeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wa kukabiliana na harakati za makundi yenye silaha katika maeneo hayo. Hivi karibuni Ivory Coast iliongeza idadi ya wanajeshi wake katika mpaka wa nchi hiyo na Liberia kwa ajili ya kukabiliana na mashambulizi ya makundi yenye silaha yanayoendesha hujuma katika maeneo ya mpaka wa nchi mbili hizo.

Powered by Blogger.