ad

ad

Yanga, Azam kutimuana kileleni leo

Vinara wa msimamo wa Ligi Kuu Bara, Yanga wanashuka Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza leo kucheza na Toto African, huku Azam FC wanaoshika nafasi ya pili, nao wakiisubiri nyumbani Chamazi, Polisi Morogoro.
Mechi hizo zina ushindani mkali hasa ukizingatia kuwa, timu hizo zinashika nafasi ya kwanza na pili, hivyo mshindi atazidi kujiongezea matumaini ya kutwaa ubingwa.
Lakini kwa upande mwingine, wapinzani wa Yanga na Azam nao wana kibarua kigumu cha kujaribu kujinusuru na janga la kuporomoka daraja, hivyo ili kuepuka hali hiyo ushindi ni lazima.

Yanga iko kileleni na pointi 42 baada ya mechi 18 ikifutiwa na Azam yenye pointi 36. Polisi Moro ya tutu kutoka mikiani ikiwa na pointi 16, wakati Toto African iliyoshinda mechi mbili tangu Septemba 15 mwaka jana, inashika nafasi ya pili kutoka mkiani ikiwa na pointi 14. 
Katika mechi ya kwanza msimu huu kati ya Yanga na Toto zinazoelezwa kuwa 'ndugu', Wanajangwani waliibuka na ushindi wa mabao 3-1 yaliyofungwa na Jerryson Tegete, Mbuyu Titwe na Didier Kavumbagu.

Hivyo basi, Toto watashusha kikosi cha kutaka kulipa kisasi hasa ukizingatia watakuwa Uwanja wa nyumbani na vilevile kuepuka kushuka daraja.
Kocha wa Yangam, Ernest Brandts amesema mchezo huo utakuwa mgumu kwa vile Toto wamepata nguvu zaidi baada ya kuwa na uhakika wa huduma kutoka serikali ya mkoa tofauti na awali.

Hofu kubwa ya Yanga ni kumkosa kipa namba moja, Ally Mustapha ëBarthezí aliyekuwa mgonjwa, lakini jana aliweza kufanya mazoezi mepesi na bado haijajulikana kama ataweza kucheza

Kocha wa Toto Africans, John Tegete amesema amekiandaa vizuri kikosi chake kupata ushindi kwenye mechi ya leo.
"Tumejipanga kuhakikisha tunashinda mechi hiyo na vijana wangu wataingia uwanjani kwa kazi moja tu ya kusaka ushindi kwa nguvu zote bila ya kujali uhusiano wetu na Yanga," alisema Tegete.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa mechi moja itikayopigwa Uwanja wa Taifa kati ya Mabingwa watetezi, Simba dhidi ya Coastal Union ya Tanga.
Powered by Blogger.