ad

ad

ROBIN VAN PERSIE KUZEEKEA MANCHESTER UNITED

ROBIN VAN PERSIE anataka kuichezea Manchester United kwa maisha yake yote yaliyobaki katika soka.

Mholanzi huyo alihamia Old Trafford kutoka Arsenal kiangazi kilichopita baada ya miaka nane akiwa na timu hiyo ya London Kaskazini.
Van Persie amekuwa na mwanzo wa kishindo United, akifunga mabao 23 katika mechi 31 za kwanza kukisaidia kikosi chake kuongoza Premier League.

Shabaha ya nyota huyo wa miaka 29 ilipotea katika mechi saba za mwisho akiwa na United, lakini ‘alifufuka’ na kuipigia mabao matatu Uholanzi katika mechi mbili za hivi karibuni na kumpita gwiji Johan Cruyff katika chati ya vinara wa kucheka na nyavu wa muda wote kwa timu hiyo ya taifa.
Van Persie aliliambia gazeti la Voetbal: “Miaka ijayo ni Manchester United. Na labda muda mrefu. United itakuwa klabu yangu ya mwisho.”

Amesema kila siku anakutana na changamoto mpya United, huku maendeleo yake yakizidi kusonga.
Mkataba wa sasa wa Van Persie utafika mwisho akifikisha umri wa miaka 33, lakini akiwatumia Giggs mwenye miaka 39 na Scholes, 38 kama kigezo, mshambuliaji huyo nae anaweza kuongeza maisha yake Old Trafford.
CHANZO CHA HABARI NI SALUTI 5
Powered by Blogger.