ad

ad

Pope kutawazwa rasmi Jumanne

Kanisa Katoliki linatarajiwa kuwakaribisha viongozi mbalimbali duniani watakaohudhuria misa ya  kutawazwa kwa Papa Francis, wakati akianza wadhifa wake rasmi hapo kesho, Jumanne. 
Hafla hiyo inatarajiwa kuwa kinyume na hali ambayo kwa kawaida inahusiana na matukio makubwa katika  Kanisa hilo, kutokana na kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki alivyojionyesha katika siku chache za  kwanza kuwa mtu wa kawaida, akiwa papa wa kwanza kutoka eneo la Amerika ya Kusini.

Kansela Angela Merkel wa Ujerumani, Waziri Mkuu Mariano Rajoy wa Uhispania na mwenzake kutoka  Ufaransa, Jean-Marc Ayrault, ni miongoni mwa viongozi wa juu wa Ulaya wanaotarajiwa kuhudhuria, pamoja na Rais wa Umoja wa Ulaya Herman Van Rompuy na Rais wa Halmashauri ya Umoja huo, Jose Manuel Barosso. Makamu wa Rais wa Marekani, Joe Biden, ambaye ni  Mkatoliki, amewasili   jana kuiwakilisha nchi yake katika sherehe hizo. Jana mchana, Papa Francis  aliwahutubia watu  150,000 waliokusanyika katika uwanja wa Mtakatifu Petro.
Powered by Blogger.