ad

ad

Mawakili wa Kenyatta wataka kesi ifutwe

Mawakili wanaomuwakilisha rais mteule wa Kenya, Uhuru Kenyatta, kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, ICC, leo hii watawakilisha ombi la kuitaka Mahakama hiyo kufuta mashitaka dhidi ya kiongozi huyo. 

Kesi dhidi ya Kenyatta, kwa madai ya uhalifu dhidi ya ubinadamu kuhusiana  na mauaji baada ya uchaguzi nchini Kenya mwaka 2007, imeingia katika utata zaidi kutokana na  ushindi wake katika uchaguzi uliofanyika kwa amani mapema mwezi huu.

 Kesi hiyo pia ni mtihani mkubwa kwa Mahakama hiyo, ambayo iliundwa karibu muongo mmoja uliopita kama mahakamaya  kwanza ya kudumu duniani inayowahukumu wahalifu wa kivita, lakini hadi sasa ikiwa imeweza kutoa  hukumu moja tu. 

Kenyatta pamoja na mkuu wa zamani wa utumishi wa umma, Francis Muthaura,  walikuwa miongoni mwa watuhumiwa sita ambao awali walifunguliwa mashtaka na mwendesha  mashtaka mkuu wa ICC kwa uchochezi katika ghasia baada ya uchaguzi wa mwaka 2007, ambapo  karibu watu 1,200 wameuwawa. Jumatatu iliyopita, mwendesha mashitaka mkuu Fatou Bensouda, aliondoa mashitaka dhidi ya Muthaura, ingawa alisema kuwa uamuzi huo usingelikuwa na athari kwa kesi ya Kenyatta.
Powered by Blogger.