Marais wa Iran na Pakistan wazindua bomba la gesi
Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na
mwenzake wa Pakistan Asif Ali Zardari wamezindua rasmi awamu ya kwanza
ya ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi utakaogharimu mabilioni ya dola.
Marais hao wawili wamehudhuria hafla ya uzinduzi huo iliyofanyika
mpakani mwa nchi mbili na kuhudhuriwa pia na Waziri wa Mafuta wa Iran
Rostam Qasemi na Waziri wa Mambo ya
Nje Ali Akbar Salehi. Bomba hilo
litasafirisha gesi asilia kutoka Iran kuelekea nchini Pakistan na
viongozi wa nchi hizi mbili wamesema kuwa mradi huo utaimarisha amani,
usalama na maendeleo ya Iran, Pakistan pamoja na mataifa mengine ya eneo
hili.
Bomba hilo la gesi litakalokuwa na urefu wa kilometa 1,600
litapunguza uhaba wa nishati nchini Pakistan kwa kusafirisha kila siku
mita mraba milioni 21.5 za gesi asilia ya Iran hadi Pakistan.

Post a Comment