ad

ad

MANCHESTER UNITED YATANGULIA NA BAISKELI YA MBAO.

WAKICHEZA soka bovu, Manchester United wameshindwa kulinda magoli yao mawili ya kipindi cha kwanza na kuruhusu Chelsea kuyakomboa kipindi cha pili katika mechi ya robo fainali ya kombe la FA.
Dakika ya 5 ya mchezo Javier Hernandez anakimbilia pasi ndefu ya Michael Carrick na kuupiga kichwa, mpira unakwenda moja moja wavuni na kuandika bao la kwanza.
Wayne Rooney akatupia bao la pili dakika ya 11 baada ya kupiga mpira wa adhabu ulioambaa ambaa juu ya vichwa vya mabeki wa Chelsea na kumfanya kipa Cech achelewe kuchukua hatua na kuacha mpira ukitinga wavuni.
Javier Hernandez salutes his opener
Hernandez akishangilia goli la kwanza la United
Wayne Rooney slots Man Utd 2-0 up
Wayne Rooney anapiga la pili
Adhabu hiyo ilitokea baada ya mshambuliaji Victor Moses kumpiga kibega Luis Nani.
Baada ya hapo Manchester ilipata nafasi chache za kufunga lakini umakini mbovu wa washambuliaji wake ukafanya matokeo yabakie 2-0 hadi mpumziko.
Wayne Rooney celebrates his goal
Rooney akisherehekea goli lake
Kipindi cha pili Chelsea waliendelea kuwabana United na kuwalazimisha warudi nyuma kuhami lango lao.
Mabadiliko yaliyofanywa na kocha Rafa Benitez katika dakika ya 52 yaliinufaisha Chelesea.
Benitez aliwatoa Frank Lampard na Victor Moses nafasi zao zikichukuliwa na Eden Hazard na John Obi Mikel.
Hazard akiwa upande wa kushoto akapokea pasi ya Juan Mata, akauchonga mpira uliokwenda kwenye nyuzi 90 upande wa kulia na kuandika bao la kwanza.
Mabadiliko ya Manchester kumtoa Hernandez na kumwingiza Van Persie dakika ya 62 hayakuizuia Chelea kuandika bao la kusawazisha.
David Luiz alichukua mpira na katikati ya uwanja na haraka haraka akampa pasi Demba Ba aliyempatia mpita Hazard aliyezunguka na kumpelekea mpira Ramires aliyekuwa kando ya beki John Evans.
Eden Hazard takes the plaudits after his goal
Hazard akipewa tano na wachezaji wenzanke ngoma 2-1 hiyo
Ramires akageuka na kuachia mkwaju wa chini chini wa yadi 16 uliompita kipa De Gea na kufanya matokeo yawe 2-2.
Ramires levels for Chelsea
Ramiressssssss 2-2
Dakika za lala salama United walinusurika mara mbili baada ya De Gea kupangua mashuti ya Mata na Ashley Cole.
Mshindi wa mechi yao ya marudiano atakutana na Manchester City katika hatua ya nusu fainali.
Man Utd: De Gea, Da Silva, Evans, Ferdinand, Evra, Carrick, Cleverley, Nani (Valencia 45), Kagawa (Welbeck 76), Rooney, Hernandez (van Persie 62).
Chelsea: Cech, Azpilicueta, Luiz, Cahill, Cole, Ramires, Lampard (Mikel 52), Moses (Hazard 52), Mata, Oscar, Ba (Torres 77).
Powered by Blogger.