MANCHESTER UNITED YAANGUSHA KARAMU NZITO, CHELSEA YACHARUKA
MANCHESTER
UNITED ikiwa kwenye uwanja wake wa nyumbani, imeipa kipigo kizito
Norwich City na kuzidi kujiimarisha kileleni mwa ligi kuu ya Uingereza.
United
imevuna ushindi wa mabao 4-0 matatu kati yake yakiwa yamefungwa na
kiungo Shinji Kagawa huku bao la nne likiwekwa kimiani na Wayne Rooney.
Iliwachukua
United hadi dakika za majeruhi za kipindi cha kwanza kupata goli la
kwanza lililoanzia kwa Robin Van Persie kabla ya kumfikia mfungaji.
Kagawa akafunga tena katika dakika za 76, 82 na 87 kabla ya Rooney kuhitimisha karamu hiyo katika dakika ya 90.
Naye
mshambuliaji Demba Ba aliipatia Chelsea goli pekee katika dakika ya 28
na kuipa timu yake pointi tatu muhimu dhidi ya West Bromwich.
Matokeo mengine ya mechi zilizochezwa leo ni kama ifuatavyo:
Chelsea 1 - 0 West Bromwich A.
Everton 3 - 1 Reading
Manchester U. 4 - 0 Norwich C.
Southampton 1 - 2 Queens Park R.
Stoke C. 0 - 1 West Ham U.
Sunderland 2 - 2 Fulham
Swansea C. 1 - 0 Newcastle U.
Fellaini akishangilia moja ya mabao ya Everton dhidi ya Reading

Post a Comment