ad

ad

BARCELONA SI LOLOTE KWA REAL MADRID

Sergio Ramos amefunga la dakika ya 82 kufuatia kona ya Luka Modric na kuipa Real Madrid ushindi wa 2-1 dhidi ya Barcelona katika mechi kali ya ligi kuu ya Hispania.
Huo unakuwa ni ushindi wa pili wa Real Madrid dhidi ya Barcelona ndani ya siku tano.
Karim Benzima alikuwa wa kwanza kuitanguliza mbele Real Madrid kwa bao lake la dakika ya 6 kabla ya Lionel Messi hajasawazisha dakika ya 18 likiwa ni goli lake la 18 katika mechi dhidi ya Real Madrid.
                            Benzima baada ya kufunga bao la kwanza
Kwa bao hilo Messi sasa amefikia rekodi ya mkongwe wa Real Madrid Alfredo Di Stefano ambaye nae alitupia magoli 18 katika mechi zilizozikutanisha timu hizo.
Wakiwa wanajiandaa na mechi ya ligi ya Mabingwa dhidi ya Manchester United Jumanne ijayo, Real Madrid ilimpuzisha nyota wake Cristiano Ronaldo hadi dakika ya 58 alipoingizwa ili kuongeza nguvu.
Baada ya mchezo kipa Victor Valdes alilimwa kadi nyekundu baada ya kutoa lugha chafu kwa mwamuzi.
Powered by Blogger.