MANCHESTER CITY YAFA KIFO CHA MENDE YAPIGWA 2-0 NA EVERTON
LONDON, ENGLAND
EVERTON
imeifanyia kitu mbaya Manchester City katika harakati zao za kutetea
ubingwa wa Premier League baada ya kuichabanga mabao 2-0 kwenye Uwanja
wa Goodison Park.
Osman akiandika bao la kwanza
Everton waliodhibiti eneo la kiungo walipata goli la kwanza kupitia mkwaju wa mbali wa Leon Othman katika dakika ya 32.
Dakika ya 62 Everton wakapata pigo baada ya kiungo wake Steven Pienaar kutolewa nje kwa kadi ya pili ya njano.
Steven Pienaar akilambishwa kadi nyekundu
City
walitafuta goli la kusawazisha kwa udi na uvumba huku wachezaji wake
Carlos Teves, Dzeko, Silva na baadae Nasir wakihaha huku na kule.
Lakini
wenyeji hao waliopata mzuka wa kumaliza kwenye timu nne za juu baada ya
kupata pointi tatu, walicheza ‘jihadi’ huku kipa wa akiba, Jan Mucha
akiokoa mabao ya wazi kabla shuti la mwisho kutoka kwa Jelavic
kuwahakikishia ushindi.
City
walinyimwa penalti dakika za mwisho baada ya refa Lee Probert kutoa nje
ya eneo la hatari mpira na kuamuru adhabu ya ‘frikiki’ baada ya
Marouane Fellaini kuushika, ingawa tukio hilo lilitokea ndani ya boksi.
Dakika 90 za kawaida zikamalizika na kuingia dakika 3 za nyongeza.
Katika dakika ya mwisho kabisa ya muda huo wa nyongeza, Marouane
Fellaini akachukua mpira kwenye eneo la goli lake akikiambia nao hadi
jirani na 18 ya City, akammegea pasi Nikica Jelavic.
Jelavic akijikunjua na kufunga bao la pili
Jelavic
aliyeingia dakika ya 90 kuchukua nafasi ya Anichebe, hakufanya ajizi
akaiahadaa beki ya City na kuachia mkwaju wa juu uliokwenda moja kwa
moja wavuni.
Post a Comment