Makao makuu ya soka Misri yateketezwa moto
Waandamanaji waliokuwa na hasira wameteketeza moto makao makuu ya Shirikisho la Soka Misri mjini Cairo.
Aidha mtu moja anaripotiwa kuuawa baada ya kupigwa risasi na vikosi vya polisi karibu na Medani ya Tahriri mjini Cairo.
Machafuko hayo yameibuka Jumamosi baada ya Mahakama ya Jinai Cairo
kuidhinisha hukumu ya kifo iliyotolewa dhidi ya watu 21 mwaka 2012
katika kesi ya machafuko yaliyojiri baada ya mechi ya soka mjini Port
Said. Mahakama hiyo pia ilitoa hukumu ya kifungo cha maisha dhidi ya
watu wa tano. Waliohukumiwa wamepatikana na hatia ya kuwaua watu 74
katika ghasia zilizoibuka mjini Port Said baada ya timu ya mji huo,
Al-Masry kuifunga Al
Ahly ya Cairo mabao matatu kwa moja mapema mwaka
2012. Wakaazi wa Port Said wamekasirishwa na hukumu ya mahakama
iliyowapata na hatia wakaazi wa mji huo. Maandamano yameripotiwa katika
mji huo wa Mfereji wa Suez na tokea Machi 3 ambapo watu wapatao saba
wameuawa. Wamisri wanasema hukumu iliyotolewa na mahakama ni ya kisiasa
na inaipendelea timu ya Al Ahly ambayo ni kati ya timu zenye ushawishi
mkubwa zaidi nchini Misri.

Post a Comment