JE WAJUA MADHARA YA MITANDAO YA KIJAMII?
Leo nimerudi na mada nyingine ya mahusiano, na katika mada
yetu ya leo sio ndefu ila ina swali mengi
yasiyo na majibu.kwamba “je unajua kuwa
mitandao ya kijamii inaongoza kwa uvunjani wa mahusiano ya kimapenzi?”
Mitandaoya kijamii inatajwa kuwa ndio inayoongoza kwa
kuvunja ndoa na mahusiano yasiyo rasmi ya kimapenzi,
Uchunguzi uliofanywa na watafiti unaonyeshwa mitandao hiyo
huvunja mahusiano hayo kutokana na Ama MKE AU MUME, Girlfriend au
Boyfriend kuitumia mitandao hiyo kwa
kuweka picha zao za nusu utupu, je? Ni nani unataka aone maungo hayo? Au ni
sehemu ya kujitangaza kibiashara binafsi?
Kati ya picha hizo mbaya zaidi ni za wadada,ambazo maungo
yake yanamshawishi mwanaume kumtumia Friend Request. Utafiti unaonyesha kuwa mtu anaetumia
mitandao hiyo yaani Facebook, Twiter, Waasap, na kadhalika huwa wakali wapenzi
wao wanapotaka kusoma sms zake hasa za inbox unakuwa ugomvi mkubwa. Jiulize je
picha unazoziweka zina mtazamo mzuri kwa
jamii?
Moja ya wanaotajwa kutia fora kuweka picha hizo au kuvaa
nguo za utupu na kupiga picha kisha kuziweka kwenye mitandao hiyo wakiwemo waigizaji wetu wa filamu na muziki wa kizazi
kipya.
Je ni kweli kwamba hatujui kuwa nguo tunazovaa ni nusu uchi
au ni maonyesho ya nguo zenu za ndani ili tuzione? Familia zenu zinaichukuliaje hali hiyo,
Wanajamii wanawapenda kwa mavazi hayo au inawatazama kwa jicho la kingono?
NINI MAANA YA MAADILI? HIVI HAKUNA SHERIA
INAYOZUIA MTU KUONYESHA NUSU YA SEHEMU NYETI?
BADILIKENI:

Post a Comment