YAYA TOURE ARUDI NA MKWARA KWA MANCHESTER UNITED
MANCHESTER, ENGLAND
KIUNGO wa kimataifa wa Ivory Coast, Yaya Toure, amesema kuwa amerudi kuizuia Manchester United kutwaa ubingwa wa Premier League.
Toure jana usiku amewaonya wapinzani wao wakubwa, United akisema “mbio za ubingwa bado sana kufika mwisho.”
Staa
huyo wa Manchester City amerejea kutoka Kombe la Mataifa ya Afrika
akiapa kuisaidia timu yake kufuta pengo la pointi tisa kati yao na
vinara United.
City
ilitoka nyuma pointi nane msimu uliopita na kutwaa ubingwa mbele ya
United, na sasa staa huyo anaitumia kumbukumbu hiyo akisisitiza: “Nina
hakika tutarudi.
"United
ina kikosi madhubuti na kweny egazeti wana safari nyepesi kuliko sisi,
lakini mbio za ubingwa ni safari ndefu kufika mwisho.”
Alisema kuwa matokeo mazuri ndiyo yatawarudisha kwenye mstari, na kwamba sasa wanarudi katika hilo.

Post a Comment