MRISHO MPOTO KUGOMBEA UBUNGE UCHAGUZI 2015
MSANII nyota wa mashairi, Mrisho Mpoto “Mjomba” amsema atagombea ubunge katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015.
Akiongea
na kipindi cha Hot Mix cha EATV jana jioni, Mpoto alisema baadhi ya
wabunge hawafanyi kazi yao ipasavyo na hivyo ameamua kuwafuata huko huko
mjengoni ili akawanyooshe.
“Tumekuwa tukipiga kelele sana na tungo zetu lakini haisadii, sasa ngoja niwafuate huko huko” alisema Mpoto.
Hata
hivyo Mpoto alikataa kutaja jimbo wala chama. “Kwa leo sitawaambia ni
jimbo gani au chama gani, hilo ntawaambia baadae, ila ukweli ni kwamba
lazima nikagombee ubunge” alisema Mpoto na kuongeza kuwa jimbo lolote
linalolegalega popote pale Tanzania, linaweza kuwa ndio jimbo lake.
Mrisho apoulizwa ataingia vipi bungeni na rasta alisema hilo atajua huko huko.

Post a Comment