ad

ad

LUIZER MBUTU KUZALIWA UPYA JUMAMOSI MANGO GARDEN

BENDI ya African Stars “Twanga Pepeta” imemwandalia kiongozi wa bendi hiyo, Luizer Mbutu sherehe kubwa ya siku yake ya kuzaliwa (Birthday Party) itakayofanyika Jumamosi tarehe 09-02-2013 katika ukumbi wa Mango Garden uliopo Kinondoni jijini Dar es salaam.
Luizer Mbutu hii ni mara ya pili kufanyiwa sherehe hiyo ambapo kwa mara ya kwanza ilikuwa ni mwaka jana ndani ya Club ya Maisha, Oysterbay jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa mmoja wa wasenaji wa Twanga Pepeta, Hassan Rehani ASET imeamua kumfanyia Luizer Mbutu sherehe hiyo kwa mara ya pili mfululizo kwa kutambua mchango wake mkubwa alioutoa katika bendi ya Twanga Pepeta kwa kudumu kwa muda mrefu bila kuhama na kwa kufanya kazi kwa kujituma bila ya kuchoka.


Sambamba na sherehe hiyo, Rehani amesema Twanga Pepeta kama ilivyo kawaida yao watainogesha sherehe hiyo ya Kiongozi wao kwa masebene matamu yatayoendana na nyimbo nzuri zilizo na meseji zilizojitosheleza kutoka kwa wanamuziki wenye vipaji vya viwango vya hali ya juu.
Hassan Rehani ameongeza kuwa wadau mbalimbali wamealikwa kuhudhuria sherehe hiyo ili kutoa sapoti kwa Kiongozi huyo wa Bendi katika siku yake ya kuzaliwa kwa kuwa utatumika utaratibu kama wa mwaka jana wa kulishwa keki kwa wadau na marafiki walio karibu na bendi ya Twanga Pepeta.
Powered by Blogger.